Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Yanga imefanikiwa kuchanja mbuga katika michuano ya Kombe la Shirikisho kwa jumla ya mabao 5-2 ikiwa ugenini nchini Zimbabwe.

Yanga wamefuzu licha ya kufungwa kwa bao 1-0 dhidi ya FC Platnum katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Mandava ulio takribani Kilomita 200 kutoka mji wa Bulawayo.
Mechi hiyo kali na ya kuvutia, wenyeji walipania kufunga mabao manne ili wafuzu lakini ilishindikana.
Kocha Hans van der Pluijm alilazimika kumtoa mapema kinda Said Juma ‘Makapu’ kutokana na kuonekana kuzidiwa na nafasi yake kumuingiza Kelvin Yondani.
Kwa kuwa Yanga walifungwa katika kipindi cha kwanza, kipindi cha pili, Mholanzi huyo aliamua kujaza viungo wengi zaidi.
Wingi wa viungo wengi, kulionyesha kuwanyima nguvu Wazimbabwe hao hivyo kufanya Yanga icheze kwa kujiamini.
Pia kasi ya Platnum nayo ilipungua hivyo kuipa Yanga nafasi kucheza vizuri.

Ngassa na Simo Msuva, pia walipoteza nafasi kadhaa ambazo zingeiwezesha kupata mabao. hata hivyo walikuwa tishio kwa mabeki hao wa Platnum.


Chapisha Maoni