Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



























































































































Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti alikataa kujibu maswali kuhusu hatima
 yake baada ya mabingwa hao watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kubanduliwa kwenye nusufainali na Juventus kwa kulazwa kwa jumla ya mabao 3-2 Jumatano. 
 

Mwitaliano huyo, aliyewahi kukufunza Juve, aliongoza Real kushinda taji lao la 10 Ulaya msimu uliopita lakini anaelekea kumaliza msimu huu bila taji lolote kubwa.
Hili haliwezi kukubalika katika klabu hiyo tajiri zaidi duniani, ambako kumbukumbu huwa fupi na hakuna subira, na ambapo rais wao Florentino Perez kwa kawaida hufuta makocha wakishindwa kushinda vikombe.
Kikao cha Jumatano cha baada ya mechi kilitawaliwa na maswali kuhusu hatima ya Ancelotti na iwapo atahudumu mkataba wake wote wa miaka mitatu, ambao unamalizika mwisho wa msimu ujao.
“Hakuna maana sana kuongea kuhusu siku zijazo leo,” Ancelotti aliambia wanahabari.
“Kawaida ninaweza kujipa alama 10 kati ya 10 kwa sababu najitolea sana kazini ingawa huwa sitaji kujipatia alama,” akaongeza mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 55, ambaye alipoteza fursa ya kuwa kocha wa kwanza kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara nne.
"Tulifanya kila tulichohitajika kufanya. Tulishambulia sana. Tukapata nafasi zetu. Ikiwa kuna jambo tunafaa kujilaumu kutokana nalo basi ni mechi ya mkondo wa kwanza.”
Juve walitoka nyuma na kutoka sare 1-1 uwanjani Bernabeu kupitia bao la fowadi wa zamani wa Real Alvaro Morata, baada ya kushinda mechi ya mkondo wa kwanza mjini Turin 2-1.
Real wamo alama nne nyuma ya viongozi wa La Liga Barcelona zikiwa zimesalia mechi mbili na walibanduliwa kutoka King's Cup na wapinzani wao wa jiji Atletico Madrid Januari.
"Hatukucheza kwa ukali sawa kama tulivyofanya wakati huu ambapo tulijitolea kabisa,” Ancelotti alisema.
Real wanahitaji kujiinua upesi na kujiandaa kwa mechi yao ya La Liga ugenini Espanyol Jumapili, siku ambayo Barca huenda wakatwaa taji lao la tano la La Liga katika miaka saba wakishinda Atletico.
Kubanduliwa kwao Jumatano kutawauma zaidi Real na mashabiki wao kwani Barca wamefuzu kwa fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya itakayochezewa Berlin Juni 6 na fainali ya King's Cup dhidi ya Athletic Bilbao.
Klabu hiyo ya Catalona imo mbioni kurudia ushindi wa mataji matatu makuu msimu mmoja sawa na ilivyofanya 2009, ilipoibuka timu ya kwanza, na ya pekee, kutoka Uhispania kufanikiwa kufanya hilo.


Chapisha Maoni