Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Katika kuhadhimisha siku ya waandishi wa Habari chuo kikuu cha Iringa ,leo ijumaa kuna Bonaza la michezo  litakaloshirikisha michezo  mbali mbali ambapo washiriki ni wanafunzi wote wanaosomea uandishi wa Habari chuoni hapo.
Michezo  hiyo ambayo imeaza asubuhi hii ni Pamoja na mchezo wa Kukuna Nazi,Mpira wa Miguu,wavu,Pete,Kikapu,Riadha,Kuvuta Kamba  Pamoja na Kuruka Kamba.
Vile Vile patakuwepo  na Mashindano ya Kucheza Mziki,kuimba ,kukimbia  Ndani ya Magunia,Kukimbiza Kuku,Kukimbia na yai kwenye kijiko  pamoja na Kunywa Soda.
 
Akizungumza na Jelamba viwanjani Mwenyekiti wa Mashindano hayo Shedrack Mgaya  amesema  lengo kubwa la Bonaza  ni kujenga  Umoja kwa wanafunzi wote pamoja na kuhamasisha michezo.
“,waandishi wa Habari lazima tutambue kwamba  ili kuendeleza michezo  lazima tuwe katika mstari wa mbele kuhamasisha michezo,  ni kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wetu wakati mwingine,inatulazimu kuandaa mabonza mara kwa mara ili kutoa elimu kwa jamii”Alisema Mgaya.
 

Katika Bonaza Hilo washindi watapata Soda,Peni,Biskuti pamoja na Soksi  kama motisha kwa kushiriki


Chapisha Maoni