Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Fifa-headquarters-in-Zuri-007
Polisi nchini Uswiss wamewakamata maafisa sita wa vyeo vya juu wa shirikisho la soka duniani (FIFA) kwa tuhuma za rushwa.Polisi hao wamewakamata maafisa hao leo asubuhi saa 12 kukiwa ndio kumekucha baada ya kuwavamia maafisa hao kwenye hoteli waliokuwa wakiishi.
Maafisa hao waliokamtwa ni pamoja na makamu wa Rais wa FIFA, Jeffrey Webb na FIFA wamethibitisha hilo.Polisi wamewakamata maafisa hao kufuatia ombi la Shirika la Upelelezi la Marekani (Federal Bureau of Investigation (FBI)) wakamatwe kwa kufanya na kupokea rushwa miaka ya 1990 kwenye mabara ya Amerika ya Kaskazini ikiwemo nchini Marekani ambapo mashindano ya soka yalifanyika ambapo malipo ya pesa yalifanyika kwenye benki za Marekani na pia kwenye bara la Amerika Kusini.
Mwanasheria Mkuu wa Marekani kutoka wilaya ya New York Mashariki ambaye aliongoza uchunguzi wa sakata hilo, aliiomba ofisi ya jaji Mkuu wa Uswizi aruhusu wakamatwe
maofisa hao.
Maofisa hao wanatuhumiwa pia kutakatisha pesa haramu.Maofisa hao sasa bado wapo chini ya mikono ya polisi wa Uswizi lakini wanaweza kusafirishwa kwenda Marekani kwa mamlaka za nchi hiyo kwa FBI kujibu masuala hayo ya rushwa na wanaweza kushtakiwa.
FIFA wamesema Rais wao Sepp Blatter hajakamatwa.Hilo ni pigo kubwa kwa FIFA ambao ijumaa ya wiki hii kesho kutwa watafanya uchaguzi wa Rais wa shirikisho hilo.Na imetikisa medani ya soka kwa ujumla.Maafisa hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi huku wakiulizwa jinsi kura zilivyopigwa kupata nchi zitakazoandaa kombe la dunia mwaka 2018 na 2022.
FIFA watafanya mkutano saa saba tano asubuhi kwa saa za Uswizi (kwetu saa 7 mchana) kuzungumzia tukio hilo na inasemekana wanapanga kuahirisha uchaguzi wa ijumaa.


Chapisha Maoni