Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



 Bondia Francis Cheka (kushoto) akipambana na bondia Kiatchai Singwancha, kutoka China katika pambano lao lililokuwa na raundi 10, lililochezwa jana usiku kwenye ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es Salaam. Katika pambanohilo, Cheka alishinda kwa KO katika raundi ya saba.

Cheka jana alipanda ulingoni katika pambano lake la kwanza na kwa mara ya kwanza tangu alipohukumiwa kwenda jela kwa kumpiga aliyekuwa mfanyakazi wake huko mjini Morogoro na baadaye kupewa kifungo cha nje, ambacho bado anakitumikia hadi sasa.
 Cheka akiendelea kumuadabisha Mchina huyo,aliyeonekana kuzidiwa muda wote, huku akipiga ngumi za kushitukiza.
 Mchina akikubali yaishe kwa kukaa chini baada ya kupokea masumbwi ya kutosha na ya maana kutoka kwa mnyama Cheka aliyekuwa na hasira na mchezo huo ambao hajacheza tangu alipopatwa na matatizo ya kwenda jela.
Cheka akitangazwa mshindi mwisho wa raundi ya saba na mwanzo wa raundi ya nane, baada ya Mchina huyo kukubali yaishe mwenyeeeeeeewe, alipoamua kukaa chini alipozidiwa.


Chapisha Maoni