Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




AZAM FC imefuzu kwa asilimia 100 Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya kushinda mechi yake ya tatu na ya mwisho ya Kundi C leo dhidi ya Adama City ya Ethiopia.
Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 5-0 katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam- mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche akifunga mawili, mengine Farid Mussa, Mudathir Yahya na Aggrey Morris.


Chapisha Maoni