Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



TIMU KAMILI:
-Mfumo 4-3-3
KIPA: Kevin Trapp (Paris Saint-Germain)
-Licha ya kukabiliwa na mashambulizi makali katika Kundi ambalo walikuwa na Real Madrid na Shakhtar Donetsk, PSG walifungwa Bao 1 tu katika Mechi 6 za Kundi lao huku Kipa kutoka Germany Trapp akitamba.
FULBEKI KULIA: Andrea Barzagli (Juventus)
-Akiwa Uwanjani na Juventus, Mchezaji huyu aliewahi kutwaa Kombe la Dunia na Italy, walifungwa Bao 1 tu na yeye ndie aliemtengenezea Alvaro Morata Bao walipoifunga Sevilla.
SENTAHAFU: Thiago Silva (Paris Saint-Germain)
-Licha ya kutemwa na Brazil hivi sasa, Silva ni nguzo imara kwa PSG na kuisaidia kufuzu.
SENTAHAFU: Diego Godin (Atletico Madrid)
-Ni Sentahafu ambae alisimama imara kwa Timu yake kuruhusu Bao 3 tu hatua ya Makundi.
FULBEKI KUSHOTO: David Alaba (Bayern Munich)
-Alicheza Mechi 4 tu za Kundi lao na kusaidia kupata ushindi wa kishindo katika Mechi 3 moja ikiwa dhidi ya Arsenal huku yeye akifunga Bao 1 na kutengeneza 1.
KIUNGO KULIA: Sven Kums (Gent)
-Kwa kufunga Bao 1 na kutengeneza 2, Kums amestahili kuwemo Kikosini.
KIUNGO KATI: Willian (Chelsea)
-Mbrazil huyu alipiga Bao 4 za Frikiki murua na kuisaidia Chelsea kufuzu.
KIUNGO KUSHOTO: Raheem Sterling (Manchester City)
-Aliifungia City Bao 3 na kutengeneza 1.
FOWADI KULIA: Thomas Muller (Bayern Munich)
-Alifunga Bao 5 hatua za Makundi.
SENTAFOWADI: Hulk (Zenit St Petersburg)
-Bao 3 na kutengeneza Bao 3 kumempa nafasi Kikosini.
FOWADI KUSHOTO: Cristiano Ronaldo (Real Madrid)
-Ameweka Rekodi ya kupiga Bao 11 hatua ya Makundi ikiwemo Hetitriki dhidi ya Shakhtar Donetsk na Bao 4 walipocheza na Malmo.



Chapisha Maoni