Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Inaonyesha alex.jpg



Inaonyesha alexx 1.jpg



Mbopa Luoga
Na Alex Mapunda.

Mbopa Luoga ni miongoni mwa mabeki imara kuwai kutokea hapa nchini alikuwa moja ya Beki Hatari ambaye aliumiza vichwa vya washambuliaji hapa nchini miaka ya 1992 hadi 2000 akiwa na Maji Maji ya Songea.

Luoga,Mzaliwa wa Litui Nyasa, alianza kucheza mpira tangu akiwa shule ya msingi Kibasila Jijini Dar es Salam ambako Baba yake aliajiriwa katika       wizara ya habari na utamabuni na baadae wakaamia songea Mjini ambapo alibahatika kujiunga na Maji Maji Kids.Amezungumza na Jelamba Viwanjani na kufafanua mengi:-.

“Nilianza kucheza Soka la ushindani nikiwa na RTC Songea timu ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja la pili ngazi ya Taifa mwaka 1887,sikukaa 

sana ndani ya mwaka huo huo  nikatimukia Urafiki ya Dar [timu ya kiwanda cha nguo] hapo nilidumu kwa kipindi cha miezi 4.


“Lakini kabla mwaka huo kumalizika tuliitwa na Timu ya Tanesco Songea wachezaji wote ambao tulienda Urafiki wote tukarudi na kukijenga kikosi cha Tanesco ambacho kilicheza kwa nidhamu ya hali ya juu na kufanikiwa kupanda ligi kuu toka ligi daraja la nne nikiwa kama kepteni wa timu.

“Timu hiyo ya Tanesco ambayo  ilikuwa ikiongozwa na kocha Ray Gama[marehemu] pamoja na Mdachi Kombo ilivyunjwa na Tanesco kwa sababu ambazo hazikutajwa ingwa ilikuwa imepanda ligi kuu.

“Mwaka 1991 kwa kuwa Tanesco ilivunjwa na uongozi wa timu hiyo ikabadilishwa jina na ikaitwa Zimanimoto ili kupata nafasi ya kushiriki ligi kuu badala ya Tanesco na tulifanikiwa kucheza na Yanga,Reli Pamoja na Maji Maji lakini baadae timu ikasambalatika kwa kuwa tulitakiwa kubaki kazini kama wafanyakazi wa Tanesco.

“Nilitua Maji Maji mwaka 1992,kipindi hicho nikuwa katika kiwango cha juu sana ambapo nikikuwa kiboko ya washambuliaji hapa nchini pindi walipokuwa wakikutana na timu yetu ya Maji Maji, hapo nilicheza kwa muda mrefu Sana na kipindi chote hicho nilikuwa nikiitwa katika timu ya mkoa wa Ruvuma, ambapo mwaka 2001 nikaachana na soka la ushindani na kubakia kama mchezaji wa Kambalage Veterani na mfanyakazi wa Tanesco.


Aligoma kujiunga na Yanga naTukuyu Stars.

“Ndugu mwandishi mtu yeyote hawezi  kuchezea ajira,ni ukweli usiopingika uwezo wangu wa kusakata kabumbu ulikuwa wa hali ya juu Sana Yanga waliwatuma wawakilishi wao kuja kunichuka Songea ili kuchezea timu yao kwa kweli sikuwapa nafasi ya kufanya mazungumzo kwa kuwa nilikuwa naeshimu sana ajira yangu ndani ya Tanesco.


“Vile vile Tukuyu Stars waliniitaji ili kukitumikia kikosi chao lakini mimi sikuwa tayari kujiunga na Timu yeyote Hapa nchini nje ya mkoa wa Ruvuma kwa kuwa niliogopa kuweka Rehani ajira yangu Toka Tanesco.


Awezi kusahau

“Nakumbuka mwaka 1998 mechi  kati ya CDA ya Dodoma na Maji Maji ya Songea ambayo ilichezwa mjini Dodoma kutokana na uimara wa timu yetu tulishinda bao 1-0 ambao ulichezwa kipindi waeshimiwa wabunge wakiwa Dodoma,bao ambalo lilifungwa na Maarimu  Salehe Romario dakika ya 72.


“Baada ya Mchezo kuna tukio ambalo alilifanya mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kipindi kile Mweshimiwa Anna Makinda siwezi kulisahau kwani baada ya kuizamisha CDA alitukaribishwa kwenye chakula cha mchana.


“Wakati wa chakula makinda alivua Viatu na akaweka pembeni na akajifunga kanga kiunoni akawa kama mhudumu, akachukua maji na Kutunawisha mikono wachezaji wote kama Yesu alivyo waosha miguu mitume wake na baadae akatuletea chakula na kumpa  kila mchezaji,  kwa kweli Tukio lile lilitushitua sana kwa uduma adhimu kama ile pia ilitupa morali ya hali ya juu sana.

“Mimi sijawai shuudia tukio kama lile naamini ilikuwa mwanzo na mwisho kutokea na mimi staacha kumwombia makinda kwa mungu kwa wema wake wote ambao aliufanya akiwa kama mkuu wa mkoa wa Ruvuma kwa Timu Ya Maji Maji.

Ubingwa wa Maji Maji mwaka 1998.

Inaonyesha alexx 2.jpg 
 “Mechi yetu ya mwisho kombe la Muungano na Prisons ya Mbeya ilikuwa ngumu sana na tulifanikiwa kupata ushindi kwa mbinde wa bao 2-1 na tukafankiwa kutawazwa mabingwa.


“Nakumbuka Yanga tuliwanyang’anya tonge mdomoni kwani walitakiwa wapate ushindi dhidi ya Kem kem ya Zanzibar ili wachukue ubingwa ambapo walipoteza mchezo kwa kufungwa bao 2-1 na kutuacha wanalizombe tukichekelea.

“Baada ya ushindi huo tulipangwa na timu ngumu Toka Misri ya National Alhaly katika roundi ya kwanza ya club Bingwa Afrika wakatukausha Nyumbani na ugenini ambapo dar tulifungwa bao 3-0 na Kairo tulichezea kipigo cha bao 2-0 Dakika 5 za mwisho.


“Kikosi cha Wanalizombe ambacho kilitwaa ubingwa mbele ya Tanzania prisons katika uwanja wa sokoine Mbeya wachezaji ambao walicheza alikuwepo Doi Moke,Ali Mopelo,Omari Husein,Amri Said,Willy Martin,Mbopa Luoga,Dello Ntumba,Twaha Omari[marehemu],Godfrey Kikumbizi,Said Mshamu Pamoja na David Mjanja. Garrincha pamoja na Omari Kapilima walikuwepo kwenye Timu ya Taifa.


Walikuwa wanasali.

“Kipindi sisi Tunacheza Maji Maji Ushirikina haukuwepo tulikuwa  zaidi Tukimtegemea Mungu na mazoezi ya uhakika ambayo tulikuwa tunayafanya.

“Nakumbuka Mimi,David Mjanja,Dello Ntumba [mkongomani] pamoja na Daktari wetu wa timu Mzee Chanangula tulikuwa tukisali pamoja siku moja kabla ya mechi, mara baada ya chakula cha jioni,mara nyingi ilikuwa kuanzia saa mbili usiku hadi saa Tano.


“Sijui kama viongozi walikuwa wakifanya mambo mengine kwa Siri lakini mimi walikuwa wakinifahamu kuwa ni mtu wa sala hivyo hawakuthubutu kuniambia kitu chochote kinyume na mwenyezi Mungu.


Wachezaji anaowapenda

“Nawakubali sana Frenk Domayo wa yanga Pamoja na Messi wa Barcelona wananikosha sana.

Timu ya Taifa

“Itengenezwe kuanzia chini ili kuweza kuwa na timu bora, wachezaji waliowengi hapa nchini hawana uwezo wa kukabiliana na wachezaji wa kutoka nje kwa kuwa uwezo wao ni mdogo,kuwaendeleza wachezaji wakiwa wamekomaa ni sawa na kumwagilia mmea kwenye majani.

“Bila kuwa na Timu za vijana tutachelewa sana kushiriki kombe la dunia,mimi nakumbuka nilianza kucheza kwenye timu ya Vijana ya maji Maji ali ambayo ilipelekea kuwa mchezaji mzuri.


Ushauri kwa Timu Ya Maji Maji.

“Wanaruvuma wote wawe kitu kimoja na viongozi ili kuiudumia timu kwa moyo mweupe na kama pesa itukepo katika timu tutakuwa na wachezaji wazuri.


Baada ya kustaafu

“Hadi leo bado ni Mfanyakazi wa Tanesco kazi ambayo ni msingi wa maisha yangu pia niliwai kuwa mwakirishi wa mkutano mkuu TFF toka nikiwa kama mjumbe kisha nikachaguliwa kama kocha msaidizi katika kikosi cha underseventeen cha mkoa wa Ruvuma ambacho kilichukua ubingwa wa Tanzania mwaka 2008 na kwa sasa nimetuliwa kuwa katibu wa kamati ya ufundi na Tiba katika Timu ya Maji Maji Fc.



“Kwa sasa nina umri wa miaka 49,nina mke na watoto 5,ambapo ni mchezaji wa kambalage Veterani pia nina timu yangu binafsi ya vijana ambayo inaitwa Matogoro Mabatini Fc,anaitimisha Mbopa Luoga ambaye wakati akicheza awezi kuwasahau mshambuliaji wa Jkt Mafinga Bwana Mwalami Pamoja na Sande Manala [Computer] ambao walikuwa na uwezo mkubwa uwanjani.
mwisho


Chapisha Maoni