Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




ALI YUSUPH SULEIMAN TIGANA, FAHAMU ASILI YA JINA TIGANA.
TIGANA ALIWIKA AKIWA NA SIMBA,YANGA PAMOJA NA TAIFA STARS.

Ilipoishia jana...................

“Mimi nadhani kucheza kwangu simba ilikuwa tatizo kwa Yanga kwa kuwa kipindi hicho pambano kati yetu na simba lilikuwa limekaribia,  mimi na mwenzangu walitutuumu kuwa tulipokea pesa Simba ili kufungisha Timu kitu ambacho mimi nilikishangaa sasa na wala sikuwai fanya ,na kwa bahati mbaya Simba walitufunga Bao 1-0.

Songa nayo………………..

Kutokea kwa ‘Tigana’

“wakati nilipokuwa Mdogo watu walikuwa wakiniita Ali Kanada kwa kuwa nilikuwa nikivaa Tsherti ambayo iliandikwa ‘Kanada’  mara kwa mara hasa pindi nilipokuwa nikicheza mpira katika timu yangu ya Utotoni ya Shauri Moyo Kids,lakini baada yakiwango changu kukua na kufanya vizuri watu wengi wakaanza kuniita jina la Tigana jina ambalo nililichukia sana kwa kuwa sikuelewa maana yake.

“na kadili nilivyokuwa nikilichukia na watu walizidi kuniita baada ya kuona kero nilimfuata mwalimu wetu wa timu na kumwambia kuhusu jina lile yeye alicheka sana alafu akaniambia kuwa jina la Tigana lina maana na akaniahidi kuwa tutaangalia mkanda ili kujua kuhusu jina hilo.

“Basi mwalimu aliniita pamoja na wezangu akatuwashia mkanda kati ya Blazil na Ufaransa ilikuwa ni mechi ambayo ilichezwa miaka ya nyuma,ilikuwa ni mechi zuri sana na kocha akanionyesha kiungo wa ufaransa  ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Jean Tigana kiukweli alikuwa mchezaji mzuri sana mimi awali sikuwai sikia kuhusu mchezaji huyo ambaye alikuwa mwembamba na sifa kama za mimi.

“Basi kuanzia siku ile nikawa nafanya mazoezi mara kwa mara na kusikiliza mafunzo ya kocha huku nikifuata nyayo zake na nilikuwa nikisikia jina hilo nilikuwa nafurahi sana kwa kuwa walikuwa wakinifananisha na yeye.



Red Stars walinizuia kucheza msimu mzima.



“mwaka 1992 nyota nyekundu pamoja na Pan Africa wote waliniwinda ili kunisajili,nyota nyekundu pamoja na Pan wote walituma watu wao kunitafuta, lakini mimi mwenyewe nilikuwa na mapenzi na pan na nilikuwa siipendi nyota nyekundu.

“kuna jamaa mmoja wa nyota nyekundu alikuwa akikaa mtaani kwetu alikuwa akinifuatilia sana akanichukua mimi na kaka yangu adi ofisini kwa timu yao, mimi nikamwambia kaka yangu kuwa tuwadanganye mimi nimesaini Timu nyingine hivyo nitashindwa kusaini kwao,kweli nikawaambi kuwa tayari nilikuwa na mkataba sehemu nyingine hivyo itaniwia vigumu kusaini kwao.

“ungozi wa Nyota nyekundu walinipa mkataba na wakaniambia kuwa wapo tayari kurudisha fedha za timu ambayo mimi nilikuwa nimechukua,kaka yangu baada ya kuona Nyota nyekundu wanatoa pesa alilainika akanishawishi kusaini mimi sikuwa na mtetezi nikasaini Mkataba.

“Baada ya kufanya mazoezi siku nne nikakutana na kiongozi wa Pan nikamweleza kuwa nimesaini Nyota akanichukua adi ofisini kwao na wakanipa mkataba na wao wakahaidi kurudisha fedha ambazo nilichukua toka Red Stars,kwa kuwa nilikuwa na mapenzi na Pan afrika nikasaini mkataba pia nikahama mtaa ambao nilikuwa na nikaa mara ya kwanza nikaamia mtaa wa Namanga msasani kwa mama mkubwa ili viongozi wa Nyota Nyekungu wasinione.
 “kitu ambacho kilinifanya nisicheze kwa msimu mzima ni kwamba viongozi wa Pan waliwafuata Nyota na kuwatukana huku wakiwakebei kuwa hawana pesa hivyo nyota nyekundu wakagoma kupokea pesa toka Pan na wakasema kuwa wanamtaka mchezaji wao,kwa hali hiyo ilinilazimu kusugua bechi adi timu ilipopanda ligi kuu hapo nikapata nafsi ya kuanza kuchezea Pan Afrika katika mechi za mashindano,pia kwa kipindi hicho pia nilikuwa nikichezea timu ya mtaani hapo ya Namanga Fc.


Timu ya taifa.

“sijisifii ila kutokana na uwezo wangu mkubwa wa kusakata kandanda nimefanikiwa kutumukia kikosi cha timu ya taifa kwa misimu mingi sana,ambapo ifuatayo ni baadhi ya miaka ambayo naikumbuka nimechezea timu ya Taifa,mwaka,1993,1994,1996,1998,2001 pamoja na mwaka 2005 ambao ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kuitwa timu ta Taifa.

 Itaendelea…………………

Kesho tarehe 27 usikose.


TULIZUIWA KUPIGA PENALTI ZIMBABWE



Chapisha Maoni