Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




ALI YUSUPH SULEMAN TIGANA ALIKUWA MCHEZAJI NYOTA HAPA NCHINI.

Ilipoishia jana,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

“Baada ya dili la kucheza mpira Afrika kusini kukwama mnamo 2008 mwishoni nilikwea pipa kuelekea bongo kutokana na kusota nchini Afrika Kusini kwa muda mrefu bila kupata mkataba licha ya kiwango changu kuwa juu niliamua kuachana kabisa na soka,anasimulia Ali Yusuph Tigana kisha Anaendelea:-

Itaendelea……………………..
Mvi Bukoba iliambatana na majonzi ndani ya Simba.
“siku ya Tukio la kuzama kwa meli ya Mvi Bukoba kila nilikumbuka napatwa na simazi kubwa sana kwa kuwa tukio lile liliambatana na matukio mengine mawili kwangu,kwanza siku hiyo simba tulitoka kupoteza mchezo wa kimataifa dhidi ya waarabu katika Mjini Alexandria nchini Misri,na tukatolewa.
“baada ya mchezo mishare ya jioni tulipata taarifa kupitia kwa shirika la habari la kimataifa,CNN kwamba Meli ya Mv Bukoba imezama na watanzania wengi wamepoteza maisha kiukweli majonzi yaliongezeka mara dufu kwa kuwa tayari tulikuwa na machungu ya kuaga mashindano hapo tukapeana taarifa huku tukijiandaa kurudi Tanzania.

“hiyo ni 9 lakini 10 wakati tuliposhuka uwanja wa ndege jiji Dar es lalam hapo tulinyong’onyea kabisa kwa kuwa tulipokea Taarifa ya kwamba mchezaji wa Mahili wa Soka Ramadhani Lemi alikuwa amefariki dunia’anavuta pumzi huku akifuta machozi kutokana na kukumbuka jinsi ilivyokuwa’kisha anaendelea kusimulia; kiukweli majonzi ambayo tulikuwa nayo ni makubwa sana basi moja kwa moja tukaenda kwenye mazishi ya mchezaji mwenzetu,mungu awaweke mahali pema peponi wale wote ambao walipoteza maisha………………………
Endelea kufuatilia historia ya maisha yake kesho tarehe 22 atasimulia jinsi alivyokimbia na laki moja ya Dewji.


Chapisha Maoni