Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Ali  yusuph Suleiman ‘Tigana’alikuwa mchezaji wa kimataifa toka Tanzania kachezea timu nyingi ikiwemo Yanga,Simba,oman,taifa Stars,chelsea ya bongo bila kusahau Malaysia sio makala ya kukosa.




kwa wadau na mashabiki wa soka hapa nchini hasa kwa wale wenye miaka kuanzia 25 na kuendelea ukipita katika kijiwe chochote na gafla ukasikia jina la ALI Yusuph Suleiman maarufu kama ‘Tigana’ likitajwa na usimkumbuke! wakati ni shabiki wa ukweli wa  soka,hakika itabidi tukushangae kwa kuwa tutakuwa na wasi wasi juu ya uwezo wako wa kufikiri,kutokana na uwezo mkubwa ambao Tigana alikuwa nao pindi alipokuwa akisakata gozi la ng’ombe hapa nchini.

Tigana mzaliwa wa Ilala jijini Dar es salam alianza kusakata kandanda mwaka 1880 mwaka ambao Tanzania ilipata nafsi ya kushiriki kwa mara ya kwanza na mwisho michuano ya mataifa ya afrika nchini Nigeria katika shule ya uhuru changaiko katika mazungumzo na gazeti hili anafafanua mengi kuhusu maisha yake ya soka:-

“Nilianza kucheza soka la ushindani katika timu ya Manyema Fc mwaka 1990 timu ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja la Tatu katika nafasi ya kiungo mshambuliaji ambapo baada ya kuonyesha uwezo mkubwa nyota nyekundu na Pan Afrika waliingia kwenye kinyang’anyiro cha kunisajili ambapo mwaka 1992 nikatua Pan Afrika timu ambayo nilichezea  kwa misimu miwili na hatimaye mwaka 1994 nikajiunga na Yanga Africans, kwa kipindi hicho nilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kucheza mpira.

“Umahili wangu na umakini hasa wakati wa kufunga pindi nikutanapo na timu pinzani uliwafanya simba wanitafute kama chakula pindi mtu awapo na njaa, toka nilipokuwa Pan na walifanikiwa kuinasa saini yangu mwaka 1996 baada ya kuniwinda kwa kitambo kirefu na nilifanikiwa kuwatumikia wekundu wa msimbazi hadi mwaka 1998 hapo nilipata nafsi ya kwenda Malayasia.

“Dili la kucheza mpira katika timu ya Malaysia  mimi pamoja na mwanamtwa  Kiwelo tulifanyiwa na moja ya viongozi ndani ya simba  na tulicheza kule hadi mwaka 2001 hapo nikarudi tena Simba,wakati narudi simba maelewano kati yangu na viongozi yalikuwa yameyumba kwa kuwa kipindi tupo Maylasia tulizurumiwa sana na baadhi ya viongizi ambao walitupeleka kule,ambapo dili la kwenda kule pesa zote walichukua huku tukilipwa mishaara ambayo haikufanana na uwezo wetu wa kusakata kandanda,kuna kipindi tuligoma kucheza adi walikuja viongozi wa simba kusuluhisha mgogoro ambapo mimi sikutaka kubaki kule lakini ilitulazimu kubaki kwa vile hati za kusafiria walikuwa nazo wao ikatulazimu kuendelea kucheza kinyonge.

“kiukweli Malaysia sisi tulitoa msaada mkubwa sana kwa timu yao ambapo kabla ya kutusajili sisi timu hiyo ilikaa bila kombe kwa takribani miaka 20 lakini baada ya kutua sisi tukachukua ubingwa wa nchi hiyo,baada ya kurudi simba uhusiano wangu na viongozi uliyumba kutakana na matatizo ya fedha ya dili la Malaysia hivyo nikacheza kwa msimu mmoja na baadae nikatimukia yanga na nikaitumikia timu hiyo toka 2002 adi 2003 apo nikarudi katika timu ya mtaani kwangu kipindi hicho ilikuwa imepanda ligi kuu nayo nikaitumikia kwa msimu mmoja na 2004 nikaenda kucheza soka la kulipwa uarabuni katika nchi ya Omani.

“Omani sikukaa sana kwa kuwa nilipewa mkataba wa mwaka mmoja ambapo ulipoisha mkataba nikarudi Bongo ambapo mwaka 2005 nilijiunga na Timu ya Moro United maarufu kama chelsea ya bongo kipindi hicho moro walifanikiwa kushika nafsi ya pili katika ligi kuu ya Tanzania na kuwakirisha Tanzania katika michuano ya kimataifa.

“nikiwa na moro United tulifanikiwa kucheza vizuri katika mechi za hawali katika kombe la shirikisho lakini kutokana na wachezaji wachache wazoefu katika kikosi chetu tulitolewa na timu ngumu ya Et’oe du Sael ya Tunisia kwa Jumla ya bao 6-1 ambapo kwao walituchabanga bao 4-1 huku nyumbani wakitushindilia bao 2 mtungi na tukaaga mashindano.

“mwaka 2008 niliamua kutimkia nchini Afrika kusini mara baada ya timu hiyo kukumbwa na ukata mkubwa ambapo Tajiri aliyekuwa akishikiria timu hiyo alijitoa kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi na wachezaji wengi nyota tuliamua kuondoka, nikiwa Nchini Afrika ya kusini nilisota sana kutafuta timu ya kuchezea kwa kuwa mfumo wa kujiunga na timu za nchini humo ni sawa na Barani Ulaya ambapo ili timu ikuchukue lazima uende na meneja.

“Mimi nilijaribu bahati yangu katika timu ya Mamelody Sanders pamoja na Santos lakini niligonga mwamba kwa kuwa sikuenda na Meneja,katika Timu ya Santos wakati nilipoenda kufanya maojiano na viongozi wa timu hiyo nilitanguzana na mdogo wangu wakaniuliza huyu ni Meneja? Nikakataa kwa kweli sikuweza kupata msaada ingawa nilichezea timu hiyo kwa kipindi Fulani.

“Baada ya dili la kucheza mpira Afrika kusini kukwama mnamo 2008 mwishoni nilikwea pipa kuelekea bongo kutokana na kusota nchini Afrika Kusini kwa muda mrefu bila kupata mkataba licha ya kiwango changu kuwa juu niliamua kuachana kabisa na soka,anasimulia Ali Yusuph Tigana kisha Anaendelea:-

Itaendelea……………………..
Kesho tarehe 21-4-2014 Atasimulia tukio la kuzama kwa Mv bukoba pamoja na simba kutolewa katika michuano ya kimataifa siku ya tukio hilo usikose jelamba viwanjani kila siku.


Chapisha Maoni