Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


12 kushiriki ligi daraja la nne Iringa
Na Alex Mapunda,Iringa
JUMLA ya timu 12 zinatarajia kuonyeshana kazi katika michuano ya ligi daraja la nne Manispaa ya Iringa ambayo yanatarajia kutimua vumbi tarehe 15 mwenzi huu.
Katibu  mkuu wa chama cha soka Manispaa ya Iringa Bakari kamtandi  amesema kuwa zaidi ya timu 12 zilichukua fomu za usajili kwaajili ya michuano hiyo ambapo timu kumi na mbili pekee zimerudisha fomu na zinatakiwa kufuata masharti yote  ya michuano hiyo.
“timu zote zinatakiwa kulipa ada ya mashindano  ambayo ni shiringi 66,000 na timu ambayo itashindwa kutoa pesa hizo itakuwa imejitoa katika mashindano,pia kila  timu inatakiwa ijiandae vizuri ili wachezaji waweze kuonyesha uwezo wao kwa  manufaa ya mkoa wa Iringa”alisema Kamtandi.
Kwa upande mwingine kamtandi amewataka mashabiki na wadau wa soka mkoani Iringa kuunga mkono michezo mbali mbali  ili kuleta ushindani hapa nchini ambapo kwa sasa mkoa wa Iringa upo nyuma kimichezo na mara ya mwisho ligi kuu kuchezwa mkoani Iringa ni miaka 14 iliyopita.


Chapisha Maoni