Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Na Alex Mapunda,Iringa
TIMU ya soka ya Maji Maji Maarufu kwa jina la wanalizombe toka mkoani Ruvuma imezidi kujikita kileleni baada ya kuendeleza wimbi la ushindi katika mechi zake za ligi Daraja la kwanza  baada ya kuizabua bila huruma African Lyon toka Jiji Dar es salam.
Mchezo huo ambao ulifanyika katika uwanja wa maji maji Songea Mjini,African Lyon walikuwa wa kwanza kupata bao lakini baadae Maji Maji walikuja juu na kujipatia mabao mawili kupitia kwa Ditram nchimbi Pamoja Maseri Vanventure na kufikisha pointi 15 katika msimamo wa kundi A.
Maji Maji ya msimu huu inacheza kwa kujituma sana kutoka na mshikamano uliopo ndani ya timu hiyo ambapo toka imeanza ligi imekuwa ikicheza kwa kujituma sana hali ambapo imepelekea timu hiyo kuongoza kundi A hadi kufikia hivi sasa wakifuatiwa na Friends Rangers toka jijini Dar es salam.
Akizungumza na Championi Ijumaa Meneja wa timu ya Maji Maji God Mvula amesema kuwa kwa sasa hakuna ubishi moja kwa moja ni kucheza ligi kuu.
“Maji Maji hoyeee!,mwakani tunacheza ligi kuu pia,tumejipanga kuimalisha zaidi kikosi chetu wakati wa dirisha dogo licha ya kufanya vizuri,mzunguko huu kikubwa na kucheza ligi kuu.



Chapisha Maoni