Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



KLABU bingwa ya Tanzania Bara, Azam FC imemuajiri Mkurugenzi wa zamani wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Saad Kawemba kuwa Mtendaji wake Mkuu.
Mwenyekiti wa Azam FC, Sheikh Said Muhammad amemtambulisha rasmi leo Kawemba mbele ya wachezaji na viongozi, makao makuu ya klabu Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, baada ya mazoezi ya asubuhi.
“Nafurahi kupata nafasi hii, ni fursa nyingine tena ya kupata uzoefu mwingine katika uongozi wa soka baada ya kufanya kazi kwa mafanikio TFF,”amesema Kawemba.
Bodi ya Ukurugenzi ya Azam FC imefikia hatua ya kuajiri Mtendaji Mkuu, ili kurahisisha uendeshaji ndani ya klabu kwa lengo la kutafuta ufanisi zaidi.
Kawemba amesema anatarajia kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wote wa klabu hiyo bingwa Tanzania Bara. “Nimekuja hapa kusaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo la Azam FC, natarajia ushirikiano wa wote,”amesema.


Chapisha Maoni