Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 
Na Alex Mapunda,Iringa

Timu ya soka ya Lipuli toka mkoani Iringa imedhiilisha kuwa mwaka huu imepania kupanda daraja baada ya hapo juzi kuifumua kimondo Fc Toka Mbozi mbeya bao 1-0 Katika mchezo mkali na wakuvutia wa ligi Daraja la kwanza uliopigwa katika uwanja wa samora mkoani hapa.
Katika mchezo huo timu ya Lipuli ilijipatia bao pekee kipindi cha pili kupitia kwa  mchezaji machachari Amburos Mbilo mnamo dakika ya 74 ya mchezo na kupanda hadi nafsi ya tatu katika msimamo wa kundi A ambapo kundi hilo linaongozwa na Maji Mji ya Songea,wakifuatiwa na Friendi Rangers zote zikiwa zimejikusajia pointi 12 baada ya kucheza mechi 6,huku Lipuli ikiwa na pointi 10.
Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI Katibu Msaidizi wa Timu ya Lipuli Ronjino Malambo alisema Jumatano hii hapo watavaana na timu ya Villa Squad toka jijini Dar es salam timu ambayo inashika nafsi ya 11 huku ndugu zao African Lyon wakiburuza mkia katika kundi hilo.
Kwa pande mwingine timu ya soka ya Kurugezi  ilitoshana nguvu na Maji Maji sc wanalizombe toka Songea  katika uwanja wao wa nyumbani ambapo hadi kufikia hivi sasa wanakamata nafsi ya 6 wakiwa na pointi 8 kibindoni baada ya kucheza michezo sita.
Ligi ya Mkoa Iringa sasa ni novemba 15


Chapisha Maoni