Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





 




Na Alex mapunda,Iringa
Mwili wa ailiyekuwa  mwasisi na mlezi wa timu ya Lipuli ya Iringa Jumanne Mwalwango, umezikwa kwa heshima zote katika  makaburi ya Mlolo Iringa manispaa.
Mwalwango ambaye allifariki dunia hivi karibuni akiwa na umri wa miaka 75,alikuwa na mchango mkubwa ndani ya Lipuli toka kipindi hicho ikifahamika kwa jina la Tahita na amekutwa na umahuti katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa kwa ugonjwa wa moyo.
Akizungumza na Jelamba Katibu msaidizi wa Timu hiyo bwana Ronjino Malambo alisema kuwa kumpoteza mzee Mwalwango ni pengo kubwa ndani ya timu kwa kuwa yeye alikuwa kama dira ndani ya timu hiyo na alikuwa kipaombele katika kutoa maamzi yenye tija ndani ya Lipuli.
“safari hii tumeondokewa na mtu muhimu sana ndani ya Lipuli,tungeweza kumrudisha tungefanya hivyo lakini hatuwezi kwa kuwa ni mapenzi ya mungu,mzee wetu alikuwa mshauri,mlezi pia muda mwingine alisimama kama kiongozi na baba wa timu, pengo lake ni kubwa sana”Alisema malambo huku akitokwa na machozi.
Lipuli ilianzishwa mwaka 1972 na mzee Jumanne mwalwango toka alipokuwa kijana akaanza kuitumika timu ya Lipuli,mungu amlaze mahali pema peponi ameni!. 
 IRINGA


Chapisha Maoni