Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Afisa mkuu wa maadili anayehusika na uchunguzaji katika wa shirikisho la soka duniani FIFA ,Micheal Garcia amejiuzulu.
Bwana Garcia aliongoza uchunguzi wa FIFA kuhusu vile kandarasi za kombe la dunia la mwaka 2018 na 2022 yalivyotolewa kufuatia madai ya ufisadi.
Katika taarifa yake ya kujiuzulu Bwana Garcia amesema kuwa kuna ukosefu wa uongozi katika FIFA na kwamba alikuwa amepoteza imani na mwanachama mwenzake katika kamati hiyo jaji mjerumani ,Joachim Eckert ambaye alisema hakusema ukweli kuhusu matokeo ya uchunguzi wake.
Wanachama wa kamati hiyo ya maadili wameamua kutochapisha matokeo ya uchunguzi wa bwana Garcia.


Chapisha Maoni