Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Mario Balotelli (right) was in disagreement with Liverpool team-mates Jordan Henderson and Daniel Sturridge


Nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard amemshutumu mchezaji mwenzake Mario Balotelli kwa kuonyesha utovu wa nidhamu pale alipolazimisha apige mkwaju wa penalti badala ya Jordan Henderson aliyekuwa tayari anakwenda kupiga adhabu hiyo dhidi ya timu ya Besiktas ya Uturuki.
Balotelli alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao 1-0 katika mchezo wa ligi ya Uropa unaozishirikisha timu 32 uliochezwa Alhamisi katika uwanja wa Anfield.
Hali hiyo ilijitokeza baada ya kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Steven Gerrard nahodha wa Liverpool
Gerrard amesema kuwa Balotelli alikuwa "kwa kiasi fulani kakosea" baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia kumnyang'anya mpira Henderson, ambaye alikuwa amejitayarisha kupiga penalti hiyo.
Henderson alikuwa nahodha wa Liverpool dhidi ya Besiktas, na Gerrard anaamini angekuwepo katika mchezo huo angepiga penalti hiyo.
"Sheria ni sheria," amesema. "pongezi kwa Mario, amefunga, lakini si vizuri kuona wachezaji wakibishana. Nafikiri Jordan alilichukua suala hilo vizuri."
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers baada ya mchezo huo hakufafanua nani 



RAUNDI YA MTOANO TIMU 32
MATOKEO
Alhamisi Februari 19
Young Boys 1 Everton 4
Torino 2 Athletic Bilbao 2
Wolsfburg 2 Sporting Lisbon 0
Aalborg 1 Club Brugge 3
Dnipro 2 Olympiakos 0
Trabzonspor 0 Napoli 4
AS Roma 1 Feyernoord 1
PSV Eindhoven 0 Zenit St Petersburg 1
Guingamp 2 Dynamo Kiev 1
Anderlecht 0 Dynamo Moscow 0
Ajax 1 Legia Warsaw 0
Sevilla 1 Borussia Monchedgladbach 0
Villarreal 2 FC Salzburg 1
Liverpool 1 Besiktas 0
Tottenham 1 Fiorentina 1
Celtic 3 Inter Milan 3
MARUDIANO
Alhamisi Februari 26         
20:00 Zenit St. Petersburg v PSV Eindhoven
20:00 Dinamo Moscow v RSC Anderlecht
21:00 ACF Fiorentina v Tottenham Hotspur
21:00 Red Bull Salzburg v Villarreal CF
21:00 Besiktas v Liverpool
21:00 Internazionale v Celtic
21:00 FC Dinamo Kiev v Guingamp
21:00 Legia Warsaw v Ajax Amsterdam
21:00 Borussia Mönchengladbach v Sevilla FC
23:05 Club Brugge KV v Aalborg BK
23:05 Athletic de Bilbao v Torino FC
23:05 SSC Napoli v Trabzonspor
23:05 Olympiacos CFP v FC Dnipro Dnipropetrovsk
23:05 Sporting Lisbon v VfL Wolfsburg
23:05 Feyenoord Rotterdam v AS Roma
23:05 Everton FC v BSC Young Boys


Chapisha Maoni