Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Na Alex Mapunda,Iringa
IMEELEZWA kuwa ili Lipuli iweze kupanda daraja zinaitajika shiringi Milioni 180 au 200  Fedha ambazo zitatumika kwaajili ya maitaji yote ya timu hiyo.



Akizungumza na Championi Ijumaa Katibu Msaidizi ya Lipuli Ronjino Malambo alisema bila kuwa na fedha za kutosha  ni ngumu sana kuendesha timu kwa kuwa toka kipindi cha usajili hadi mwisho wa ligi timu inatumia fedha muda wote.

“Mara nyingi tunaendesha timu kwa ahadi hewa bila fedha mfukoni hali ambayo inapelekea wasamaria wema kuiokoa timu dakika za mwisho kwaajili ya kusafiri au chakula, kimsingi viongozi tunapata shida jinsi ya kuudumia wachezaji,tunaitaji kushikamana kwa pamoja”

“Ili kupa hizo milioni 200 lazima tuungane wote; viongozi,wadau pia ndugu jamaa na marafiki wa Lipuli na kuhakikisha fedha zinapatikana kwa wakati, watu wanaweza wakahoji hizo pesa ambazo nimezitaja hapa ni nyingi la hasha! Tunaitaji kuweka kambi zuri,kusajili wachezaji wazuri na kuwalipa mishahara mizuri” alisema Malambo.

Pia Malambo aliongeza kuwa kwa sasa wameanza kukusanya vijana wenye vipaji ambao watakuwa chini ya mchezaji wa zamani wa timu hiyo  Bona Kidava ambao watuungana na wachezaji wengine watakaosajiliwa toka  maeneo tofauti hapa nchini kwaajili ya msimu mpya.

Timu ya lipuli imeshindwa kupanda daraja msimu huu baada ya kufanya vibaya katika raundi ya pili na kuipisha African Sports na Maji Maji  kupanda toka Kundi A  ligi daraja la kwanza ambayo imemalizika hivi karibuni.



Chapisha Maoni