Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumapili Machi 8
Mgambo JKT v Ndanda FC
Mtibwa Suga v Mbeya City
Simba v Yanga

Jumanne Machi 10

Polisi Moro v Ruvu Shooting

Katika idadi hiyo Simba inaongoza kwa kushinda mara nne na Yanga ikipata ushindi mara tatu na mara nne zikienda sare lakini kizuri kwa Yanga ni kuwa na bahati kushinda Oktoba
OKTOBA 18 uwanja wa taifa Dar es Salaam kutawaka moto wakati miamba ya soka Tanzania klabu za Yanga na Simba zitakapomenyana kuwania pointi tatu muhimu ikiwa ni mara ya kwanza timu hizo kukutana tangu kuanza kwa msimu huu.

Timu hizo mbili zimekuwa na upinzani mkubwa tangu zilipoanzishwa miaka ya 1935 na 1936,kitu ambacho kimechangia kuwepo uhasama mkubwa na kusababisha kugawana bara bara.


MECHI 5 ZILIZOPITA ZA MISIMU MITATU:
Yanga 1-1 Simba 
Simba 0-2 Yanga
Simba  3-3 Yanga
Yanga 1-1 Simba 
Yanga 0-0 Simba 

Takwimu kuanzia timu hizo zilipoanza kukutana zinaonyesha Yanga ndiyo kinara kwa kupata ushindi mara nyingi zaidi ya Simba ambayo inafuatia kwa mbali.

Takwimu kama hizo kwenye upande wa kunyakua ubingwa wa Tanzania bara pia zinaibeba Yanga kwa kuchukua ubingwa huo mara 24 wakati Simba ikifanya hivyo mara 18 na kufuatiwa na klabu za Mtibwa Sugar na Coastal Union ya Tanga.


Rekodi nzuri kwa Simba katika mapambano yake na Yanga ni kupata ushindi wa mabao mengi kama ilivyofanya mwaka 1977 iliweza kuifunga Yanga mabao 6-0 na Mei 6 mwaka 2012 iliipa tena kipigo cha aibu cha mabao 5-0,uwanja wa taifa Dar es Salaam.

Simba imekuwa makini kwa kutumia vizuri madhaifu yawapinzani wao inapo wakuta wamechoka na kufunga mabao mengi yanayowapa rekodi nzuri kwenye historia za timu hizo.

Takwimu za Jelamba viwanjani za miaka mitano iliyopita kuanzia 2009 zinaonyesha Simba na Yanga zimekutana mara 11 ikiwa ni mechi maalumu pamoja na zile za Ligi Kuu ya Tanzania bara.

Katika idadi hiyo Simba inaongoza kwa kushinda mara nne na Yanga  ikipata ushindi mara tatu na mara nne zikienda sare lakini kizuri kwa Yanga ni kuwa na bahati ya kupata ushindi inapokutana na Simba mwezi Oktoba.

Oktoba 16 mwaka 2010 pambano la Ligi Kuu Tanzania bara lilifanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 mfungaji akiwa Jeryson Tegete dakika ya 70.

Yanga ilifanya tena hivyo Oktoba 29/2011 kwa kuifunga Simba safari hii ikiwa  uwanja wa taifa Dar es Salaam mfungaji akiwa  Mzambia Davis Mwape dakika ya 75,na msimu uliofuata kidogo vijana wa Msimbazi waligoma kufanywa wateja baada ya kukutana Oktoba 3/2012 na kutoka sare ya 1-1 na Yanga   Simba wakitangulia kufunga kupitia kwa Amri Kiemba dakika ya tatu na Yanga ikasawazisha dakika ya 64 kupitia kwa Said Bahanuzi. 

Oktoba  20,2013,Simba iligoma kwa mara nyingine kufungwa na Yanga kwenye mwezi huo baada ya kulazimisha sare ya mabao 3-3 huku yenyewe ikitoka nyuma ka mabao matatu yaliyofungwa kipindi cha kwanza na Yanga.

Wafungaji wa Yanga katika mechi hiyo walikuwa ni Mrisho Ngasa aliyefunga bao la kwanza dakika ya 14 na Mganda Hamisi Kiiza aliyefunga mara mbili dakika ya 35,47 

Mabao ya Simba yalifungwa na Beatram Mwombeki dakika ya 53Joseph Owino dakika ya 5 na Mrundi Gilbert Kaze dakika ya 83 mechi hii ikiwa maalumu ikipewa jina la Nani Mtani Jembe.

Ushindi pekee iliyowahi kuupata Simba inapocheza na Yanga ndani ya miaka mitano iliyopita ilikuwa ni Oktoba 31 ambapo iliweza kuifunga Yanga bao 1-0 mfungaji akiwa Mussa Hassani Mgosi dakika ya 26.

Katika takwimu hizi zilizowekwa na Mtandao wa Goal kila timu inacho cha kujivunia katika pambano hilo la Jumamosi Simba imekuwa na kipindi kizuri katika miaka mitano iliyopita wakati Yanga ikifurahi kukutana na Simba mwezi Oktoba kwa sababu imekuwa na bahati nao.

Lakini wakato Goal inakuwekea rekodi hizo timu husika kwa sasa zipo katika maandalizi kabambe kujiandaa na pambano hilo ambalo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka.

Yanga ambao ndiyo wenyeji wa pambano hilo licha ya kufurahia kucheza mwezi Oktoba lakini wanajivunia matokeo yao ya ushindi katika mechi mbili zilizopita dhidi ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons ambayo yamewaweka nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.

Simba iliyokuwa imeweka kambi nchini Afrika Kusini bado mambo siyo shwari kwani haijaonja ladha ya ushindi katika mechi tatu ilizo cheza ligi ya msimu huu.

Kocha wake Patrick Phiri,amesea anauchukulia mchezo huo kama fainali lengo lake likiwa ni kupata ushindi ili kurudisha matumaini ya kunyakua ubingwa.

Ikumbukwe timu hiyo haijafanya vizuri katika misimu miwili iliyopita ambapo msimu wa 2012/13 ilimaliza nafasi ya tatu na msimu wa 2013/14 ikamaliza nafasi ya nne na msimu huu imetumia fedha nyingi kwa ajili ya kusajili wachezaji wenye majina na viwango vya juu ili kuweza kushinda taji hilo lakini inaonekana bado mambo hayaja kaa sawa.

Pia timu hiyo mbali na kupata sare hizo tatu lakini haijaonyesha kiwango cha juu kiasi cha kuwaridhisha mashabiki wake ambao wanafika wachache uwanjani lakini katika mechi ya Jumamosi chochote kinaweza kutokea.

Tusubiri kipyenga cha Mwamuzi Israel Nkongo ambaye ndiye aliyepewa jukumu la kuchezesha pambano hilo takika zake 90 zitamalizika kwa timu gani ikiwa na furaha.


Takwimu muhimu  za Yanga na Simba

OKTOBA 18 uwanja wa taifa Dar es Salaam kutawaka moto wakati miamba ya soka Tanzania klabu za Yanga na Simba zitakapomenyana kuwania pointi tatu muhimu ikiwa ni mara ya kwanza timu hizo kukutana tangu kuanza kwa msimu huu.

Timu hizo mbili zimekuwa na upinzani mkubwa tangu zilipoanzishwa miaka ya 1935 na 1936,kitu ambacho kimechangia kuwepo uhasama mkubwa na kusababisha kugawana bara bara.

Takwimu kuanzia timu hizo zilipoanza kukutana zinaonyesha Yanga ndiyo kinara kwa kupata ushindi mara nyingi zaidi ya Simba ambayo inafuatia kwa mbali.

Takwimu kama hizo kwenye upande wa kunyakua ubingwa wa Tanzania bara pia zinaibeba Yanga kwa kuchukua ubingwa huo mara 24 wakati Simba ikifanya hivyo mara 18 na kufuatiwa na klabu za Mtibwa Sugar na Coastal Union ya Tanga.

Rekodi nzuri kwa Simba katika mapambano yake na Yanga ni kupata ushindi wa mabao mengi kama ilivyofanya mwaka 1977 iliweza kuifunga Yanga mabao 6-0 na Mei 6 mwaka 2012 iliipa tena kipigo cha aibu cha mabao 5-0,uwanja wa taifa Dar es Salaam.

Simba imekuwa makini kwa kutumia vizuri madhaifu yawapinzani wao inapo wakuta wamechoka na kufunga mabao mengi yanayowapa rekodi nzuri kwenye historia za timu hizo.

Takwimu za Goal za miaka mitano iliyopita kuanzia 2009 zinaonyesha Simba na Yanga zimekutana mara 11 ikiwa ni mechi maalumu pamoja na zile za Ligi Kuu ya Tanzania bara.

Katika idadi hiyo Simba inaongoza kwa kushinda mara nne na Yanga  ikipata ushindi mara tatu na mara nne zikienda sare lakini kizuri kwa Yanga ni kuwa na bahati ya kupata ushindi inapokutana na Simba mwezi Oktoba.

Oktoba 16 mwaka 2010 pambano la Ligi Kuu Tanzania bara lilifanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 mfungaji akiwa Jeryson Tegete dakika ya 70.

Yanga ilifanya tena hivyo Oktoba 29/2011 kwa kuifunga Simba safari hii ikiwa  uwanja wa taifa Dar es Salaam mfungaji akiwa  Mzambia Davis Mwape dakika ya 75,na msimu uliofuata kidogo vijana wa Msimbazi waligoma kufanywa wateja baada ya kukutana Oktoba 3/2012 na kutoka sare ya 1-1 na Yanga   Simba wakitangulia kufunga kupitia kwa Amri Kiemba dakika ya tatu na Yanga ikasawazisha dakika ya 64 kupitia kwa Said Bahanuzi.

Oktoba  20,2013,Simba iligoma kwa mara nyingine kufungwa na Yanga kwenye mwezi huo baada ya kulazimisha sare ya mabao 3-3 huku yenyewe ikitoka nyuma ka mabao matatu yaliyofungwa kipindi cha kwanza na Yanga.

Wafungaji wa Yanga katika mechi hiyo walikuwa ni Mrisho Ngasa aliyefunga bao la kwanza dakika ya 14 na Mganda Hamisi Kiiza aliyefunga mara mbili dakika ya 35,47

Mabao ya Simba yalifungwa na Beatram Mwombeki dakika ya 53Joseph Owino dakika ya 5 na Mrundi Gilbert Kaze dakika ya 83 mechi hii ikiwa maalumu ikipewa jina la Nani Mtani Jembe.

Ushindi pekee iliyowahi kuupata Simba inapocheza na Yanga ndani ya miaka mitano iliyopita ilikuwa ni Oktoba 31 ambapo iliweza kuifunga Yanga bao 1-0 mfungaji akiwa Mussa Hassani Mgosi dakika ya 26.

Katika takwimu hizi zilizowekwa na Mtandao wa Goal kila timu inacho cha kujivunia katika pambano hilo la Jumamosi Simba imekuwa na kipindi kizuri katika miaka mitano iliyopita wakati Yanga ikifurahi kukutana na Simba mwezi Oktoba kwa sababu imekuwa na bahati nao.

Lakini wakato Goal inakuwekea rekodi hizo timu husika kwa sasa zipo katika maandalizi kabambe kujiandaa na pambano hilo ambalo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka.

Yanga ambao ndiyo wenyeji wa pambano hilo licha ya kufurahia kucheza mwezi Oktoba lakini wanajivunia matokeo yao ya ushindi katika mechi mbili zilizopita dhidi ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons ambayo yamewaweka nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.

Simba iliyokuwa imeweka kambi nchini Afrika Kusini bado mambo siyo shwari kwani haijaonja ladha ya ushindi katika mechi tatu ilizo cheza ligi ya msimu huu.

Kocha wake Patrick Phiri,amesea anauchukulia mchezo huo kama fainali lengo lake likiwa ni kupata ushindi ili kurudisha matumaini ya kunyakua ubingwa.

Ikumbukwe timu hiyo haijafanya vizuri katika misimu miwili iliyopita ambapo msimu wa 2012/13 ilimaliza nafasi ya tatu na msimu wa 2013/14 ikamaliza nafasi ya nne na msimu huu imetumia fedha nyingi kwa ajili ya kusajili wachezaji wenye majina na viwango vya juu ili kuweza kushinda taji hilo lakini inaonekana bado mambo hayaja kaa sawa.

Pia timu hiyo mbali na kupata sare hizo tatu lakini haijaonyesha kiwango cha juu kiasi cha kuwaridhisha mashabiki wake ambao wanafika wachache uwanjani lakini katika mechi ya Jumamosi chochote kinaweza kutokea.

Tusubiri kipyenga cha Mwamuzi Israel Nkongo ambaye ndiye aliyepewa jukumu la kuchezesha pambano hilo takika zake 90 zitamalizika kwa timu gani ikiwa na furaha.


MATOKEO:
Jumamosi Machi 7
Coastal Union 2 Kagera Sugar 2  
JKT Ruvu 0 Azam FC 1


Chapisha Maoni