Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




UONGOZI  wa   timu ya soko la  Lipuli Fc  umewataka  wanachama wake na mashabiki  kujitokeza kwa  wingi  leo majira  ya saa 4  asubuhi katika  mkutano  wake  utakaofanyika  ukumbi  wa  VETA mjini Iringa.

Wito   huo  umetolewa na mwenyekiti wa Lipuli Fc  Abuu Changawa  wakati  akizungumza na  wanahabari leo  kuhusiana na maandalizi ya  mkutano  huo huku akiwataka wale  wote  wenye ushauri na maoni  mbali mbali  kufika ili  kueleza ndani ya  mkutano  huo .


Pia  alisema  kuwa lengo la mkutano  huo ni kujipanga  upya na  kuangalia namna  gani timu  hiyo  mwakani  anaweza  kupanda Ligi  kuu  baada ya  mwaka   huu  kupoteza  nafasi  hiyo .


Alisema  katika  mkutano  huo  pia wanachama   wa  kikundi cha Hamsha popo  wamealikwa kufika ili  kuweza  kutoa madai  yao  mbali mbali  dhidi ya   uongozi wa Lipuli Fc .

Japo  akisisitiza kuwa katika  katiba ya Lipuli Fc  hakuna kikundi cha Hamsha  popo  na  kuwa kufika  kwao katika  mkutano  huo ni mwanzo wa  wao  kujipambanua   zaidi  juu ya namna gani  wamekuwa  wakiisaidia Lipuli Fc .



Chapisha Maoni