Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Hatimaye miamba ya soka nchini Hispania Real Madrid imemtimua kocha wa timu hiyo Carlo Ancelotti baada ya kuiongoza klabu hiyo kwa misimu miwili.

 Former Real Madrid boss Carlo Ancelotti came close to getting the sack at the end of the 2013-14 campaign 

Kocha huyo raia wa Italia, aliiongoza Madrid kutwaa taji la kombe la Hispania kabla ya kuibebesha miamba hiyo taji la kumi la klabu bingwa barani Ulaya. Pamoja na mafanikio hayo aliyoyapata msimu uliopita, mwaka huu haukuwa mzuri kwa vijana hao wa Benabeu baada ya kuambulia patupu kwa kukosa hata kombe moja japokuwa kikosi cha timu hiyo kinatajwa kuwa cha gharama ya juu. Hasira za viongozi wa klabu hiyo ziliongezeka baada ya kutupwa nje na Juventus katika hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa Ulaya huku wapinzani wao wakubwa Barcelona ikinyakuwa taji la ligi kuu na kutinga fainali ya klabu bingwa na kombe la Hispania. Rais wa Madrid Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa haikuwa rahis kumtema kocha huyo na kuongeza kuwa kocha mpya atateuliwa wiki ijayo.
 

RECENT REAL MADRID MANAGERS 

Fabio Capello - July 2006 - June 2007
Bernd Schuster - July 2007 - December 2008
Juande Ramos - December 2008 - June 2009
Manuel Pellegrini - June 2009 - May 2010
Jose Mourinho - May 2010 - June 2013
Carlo Ancelotti - June 2013 - May 2015




Chapisha Maoni