Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Wazazi wa Simon Msuva wakiwa wameshika tuzo ya mtoto wao mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Mh. Juma Nkamia
Wazazi wa Simon Msuva wakiwa wameshika tuzo ya mtoto wao mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Mh. Juma Nkamia
Simon Msuva ameibuka kidedea baada ya kunyakua tuzo ya mchezaji bora wa msimu wa 2014-2015 zilizotolewa na wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom na kukabidhiwa na mgeni rasmi Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Juma Nkamia kwenye hafla iliyofanyika usiku wa leo kwenye ukumbi wa JB Belmonte (Kilimanjaro) uliopo katika jengo la Golden Jubilee Tower (PSPF) jijini Dar es Salaam.
Msuva ambaye amechukua tuzo mbili usiku wa leo, mbali na kuwa mchezaji bora Msuva amepewa tuzo ya mfungaji bora baada ya kutupia kambani jumla ya magoli 17 kwenye msimu uliomalizika Mei 9 mwaka huu na magoli hayo yaliisaidia Yanga kuibuka mabingwa wa ligi hiyo.
Lakikini kutokana na Msuva kuwa kwenye majukumu ya timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, zawadi zake zilichukuliwa na wawakilishi wake ambaye ni baba yake mzee Msuva aliye ambana na mkewe mama yake Simon Msuva.
 
Msuva amewabwaga Mrisho Ngassa na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ kwenye kinyang’anyiro hicho cha mchezaji bora wa ligi.
Nafasi nyingine ambazo zilikuwa zikiwaniwa ni pamoja na mlinda mlango bora ambapo tuzo hiyo imenyakuliwa na Shaban Kado (Coastal union) ambaye kwa sasa amesaini kuitumikia klabu ya Mwadui FC ya Shinyanga akiwabwaga Mohamed Yusuph (Tanzania Prisons) na Said Mohamed (Mtibwa Sugar).
Shabani Kado akipokea tuzo yake
Shabani Kado akipokea tuzo yake
Tuzo ya kocha bora imekwenda kwa Mbwana Makata aliyekinusuru kikosi cha Tanzania Prisons kisishuke daraja. Nafasi hiyo ilikuwa ikiwaniwa na Goran Kopunovic (Simba SC) pamoja na Hans Van Der Pluijm (Young Africans).
Israel Mjuni Nkongo amenyakua tuzo ya mwamuzi bora akiwabwaga Jonesia Rukyaa na Samwel Mpenzu kwenye nafasi hiyo.
Mtibwa Sugar nao wamechukua tuzo ya timu yenye nidhamu iliyokuwa ikiwaniwa na Mgambo JKT pamoja na Wekundu wa Msimbazi Simba.


Chapisha Maoni