Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Alex Mapunda,Iringa
Ramadhani Magoe
"Nilipokuwa nikichezea FC Leopard ya Kenya nilishuudia mchezaji mwenzangu akichomwa kisu na mashabiki wa Rashavana Fc wakati wakishangiria bao, hali ambayo ilisababisha kutokea vurugu kubwa na mchezo ukavunjika.
mimi na rafiki yangu tulikimbilia kituo cha polisi ili kuokoa maisha yetu, baada ya tukio lile wachezaji wenzangu waliniambia yale ni matukio ya kawaida  nchini Kenya kwa vile mfumo wa Kenya ulikuwa ukiruhusu mashabiki kuingia uwanjani wakati wa kushangilia bao,hata hivyo baada ya kuchomwa kisu Hoteku alikimbizwa hospitali na kupata matibabu na akapona”.
Hii ni sehemu ya historia ya maisha ya soka ya Ramadhani Magoe ambaye amevuka milima na mabonde na kuwa kivutio kikubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki tangu mwaka 1989 hadi 2012 kutokana na uwezo wake mkubwa wa kutikisa nyavu na kiburi uwanjani.
Safari ya soka ya Magoe ilianza kushika kasi akiwa shule ya msingi Myamatale msoma mjini toka akiwa mdogo ambapo baada ya kumaliza masomo mwaka 1989 alijiunga na timu ya tanesco timu ambayo aliichezea kwa misimu miwili na baadae mwka 1992 alinyakuliwa na timu ya Maji Mara klabu ambayo waliipandisha toka ligi daraja la tatu adi Fainali ya ligi daraja la pili na katika fainali hizo akapata nafasi ya kusajiliwa na RTC Kagera  baada ya wao kuridhika na uwezo wake wa uwanjani.
Aliitumikia RTC Kagera hadi mwaka 1996 hapo akatimukia Shinyanga Shooting timu ambayo aliichezea mechi mbili pekee na akakumbana na kisanga cha kuteguka mguu wakati wa mechi ya Shinyanga Shoting dhidi ya Milambo ya Tabora tukio ambayo lilimweka nje ya uwanja kwa kipindi cha mwaka mzima.
Baada ya mchezaji  wa  Milambo ya tabora kumtegua mguu alikata tamaa kabisa ya kuendelea kusakata kabumbu akachukua maamzi magumu ya kurudi kwao msoma na moyoni alijitangazia kuachana na soka kutokana na mikiki mikiki aliyokutana nayo baada ya kuteguka mguu.
Lakini mambo yalikuwa tofauti baada ya kuonana na kocha Silverster Mashiambaye alikuwa akifundisha timu ya kanisa Viwawa Fc, akanipa moyo na kunishawishi vilivyo na baadae nikatengua maamuzi yangu na nikaanza kufanya mazoezi katika timu yake ya Viwawa.
Baadae Mashi alisajiliwa na timu ya Toto Afrika ya Mwanza na wakati yupo Toto aliwaambia viongozi wa Toto kuwa Musoma kuna Mashine ya hatari sana tukaichukue ili tuimalishe kikosi chetu,wazo ambalo Toto waliikubari na waliniitaka kwenda kufanya majaribio,anaeleza Magoe kisha anaendelea;-
“Nakumbuka mwaka huo wa 1997 wakati wa majaribio tulikuwa wachezaji 6 wakaongezeka wengine 5,tukapambana na kikosi cha kwanza cha Toto Africa katika mchezo huo tuliibuka na ushindi mnono wa bao 11-0, mimi peke yangu nilipiga bao 7, wachezaji wa Toto walikasirika sana kisha wakaomba turudiane ili wapate nafsi ya kusawazisha hatukufanya ajizi tukawapiga tena bao 8 ambapo mimi nilifunga bao 4 na kupiga pasi za mwisho.
“Viongozi wa Toto kulingana na uwezo wetu wakatusajili moja kwa moja na  nyota yangu ilizidi kupeya maeneo yote ya ukanda wa ziwa na viunga vyake ambapo mwaka 1998 alichaguliwa kuchezea timu ya mkoa wa mwanza katika michuano ya Taifa Cup kituo kilikuwa Kagera nilionyesha kiwango cha hali ya juu sana,na tulitolewa katika fainali na mzizima United kwa bao 3-2.
“Baada kumalizika michuano ile nyota yangu iling’aa Zaidi kwa kuwa Nilichaguliwa kwenye timu ya taifa,piaYanga pamoja na Rtc Kagerawalitanga kunisajili,kiliochotekea wakati yanga wanataka kunisajili tayari nilikuwa nimeshamwaga wino RTC Kagera na wakati huo Toto afrika mkataba wangu ulikuwa umeisha,niliwambia yanga kama wanataka kunichukua wavunje mkataba wangu na Kagera kitu ambacho walishindwa na nikabakia mikononi mwa RTC Kagera.
“wakati natumikia timu ya Taifa mechi zangu za mwanzo kuchezea timu ni katika Ufunguza wa uwanja wa Taifa kwa Sasa unafahamika maarufu kama shamba la Bibi ambapo Tanzania iliziarika timu kutoka nje ikiwemo Kenya,Uganda,Zambia Pamoja na Algeria Timu ambazo tulipambana nazo katika sherehe za ufunguzi wa uwanja huo mimi nikapata nafsi za kucheza mechi za kimataifa kwa mara ya kwanza.
“ndani ya mwaka huo 1998 nilishuudia mchujo mkali sana ndani ya kikosi cha timu ya Taifa timu ambayo ilikuwa ikijiandaa na michuano ya awali ya kuuania kufuzu mashindano ya kumbe la dunia ambayo yalifanyika mwaka 2002 Korea Kusini na Korea Kaskazini.
“Nakumbuka tulichukuliwa wachezaji 100 kwenye kikosi cha Taifa baada ya mchujo tulibaki wachezaji 60,waliongezwa wachezaji wengine 30 toka Zanzibar baada ya mchujo tulibakia tena wachezaji 60,hiyo haitoshi ulipita mchujo mwingine wa wachezaji hadi tukabakia wachezaji 30 bora,hata hivyo waliongezwa tena wachezaji 10 toka mkoani Dar es salam ukafanyika mchujo wa mwisho na tukabakia wachezaji 30 ambapo mimi ingawa nilikuwa mchezaji kijana nilichulikuwa kucheza timu ya wakubwa na wachezaji wengine ambao walikuwa vijana katika mchujo huo walipelekwa katika timu ya taifa ya vijana.
“Lakini licha ya mchujo huu na kuingia kambini huku timu ikiwa na morali ya hali ya juu tulikung’utwa na Burundi jijini Dar es salam bao 1-0 bao ambalo lilifugwa  dakika ya 80 kwa shuti kali sana toka katikati ya uwanja na Tanzania tukaaga mashindano,baada ya mchezo ule mashabiki walilizingira basi Letu na wakapasua vioo kutokana na machungu ambayo waliyapata kwa matokeo mabovu ya mchezo ule na tuliokolewa na polisi nashukuru mungu hakuna ambaye alipata majeraha makubwa.
“Baada ya kuitumika RTC  kwa Msimu Mmoja mwaka 1999 mwaka ambao baba wa Taifa Rais J k Nyerere alipoteza maisha nilisajiliwa na FC Leopard ya Kenya wakati huo timu hiyo ilikuwa chini ya kocha Sundy Kayuni na wakati natua klabuni hapo Timu hiyo tayari ilikuwa imechukua ubingwa wa Kenya na wachezaji 10 wa timu hiyo walikuwa wakichezea Timu ya Taifa ya Kenya.
“Basi mvutano wa kusaka namba katika timu hiyo ulikuwa wa hali ya juu sana ,nakumbuka nilikuwa nafanya mazoezi mara 4 kwa siku kuanzia saa kumi na moja asubuhi,sasa mbili,sasa nane pia  jioni nilikuwa nikifanya mazoezi ya kukimbia kwaajili ya Stamina,kutokana na hali hiyo niliimalika Zaidi kimazoezi na nikapata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza na nilipendwa sana na uongozi wa timu.
“Nilichezea FC leopard kwa misimu miwili na baadae niliamua kuondoka kwa kuwa viongozi waLeopard walikuwa wakiitaji mafanikio ya haraka na ndani ya msimu mmoja walifukuza makocha 7 na yalibuka makundi mawili ndani ya timu hiyo ambayo yasababisha mvutano mkubwa na ulipelekea viongozi kutwangana makonde kwa hali hiyo mwaka 2003 nikatimukia Coastal Stars ya Mombasa timu ambayo ilishika nafasi ya pili na ilipata nafsi ya kucheza michuano ya washindi Afrika.
“Mchuano ambayo timu yetu ilikumbana na Canon  Yaunde Toka comeroon timu ambayo ilikuwa imetuzidi kwa kila kitu,na hatimaye tulichezea kichapo cha bao 6-0 ambapo mchezo wa kwanza ambao ulipigwa Mombasa tulifungwa bao 2-0 kabla ya kuchabangwa bao 4-0 nchini comeroon,hali ambayo ilipelekea timu yetu kutolewa roundi ya kwanza.
“Baaba mchezo huo viongozi wa timu walianza kusumbua katika maripo ya wachezaji pamoja na makocha hali iliyosasabisha maisha kwenda kombo,sikuchelewa mwaka 2004 nikarudi Tanzania kukiputa na Toto Africa ya Mwaza timu ambayo nilikaa msimu Mmoja na baadae mwaka 2005 nilirudi tena Kenya kujiunga na timu ya Sonney sugar.
“Maisha ndani ya Sonney Sugar yalikuwa mazuri tulikuwa wanapewa mishahara,posho zuri na pesa ya kujikimu hasa wakati wa safari na timu yao ilikuwa na uwezo kwa kulaza wachezaji hadi hoteli ya nyota 5, hivyo wachezaji walikuwa wanajituma sana ili kupata nafasi ya kusafiri na timu kwa kuwa mpira wa kenya uwezo wako ndio silaha pekee ya kupata nafasi ya kucheza.
“Niliitumikia timu hiyo adi mwaka 2009 mwanzoni ambapo kutokana na kusumbuliwa na majeraha niliamua kurudi Tanzania na nikarudi Msoma  kuchezea timu hiyo nikiwa kama kocha mchezaji na kuipandisha timu hiyo ada ligi daraja la kwanza lakini kuna mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu yalitokea huku viongozi wa timu hiyo muda mwingine wakishindwa kusafirisha timu kwa sababu ambazo wanazijua wao zilinifanya niachane na timu.
“Wakati wa mashindano ya ligi dala ya kwanza kituo cha Kigoma timu yetu ilikumbwa na mazingira magumu katika uendeshaji wa mashindano hasa uwajani,kwanza katika mchezo wa kwanza timu ya polisi ilifanyiwa fitina na waamuzi na ikasababisha kupoteza mchezo kitu ambacho kilitokea kuna mpira ulipigwa toka winga ya kulia beki wa timu yetu akapiga mpira kwa goti mwamuzi asema ni penalti,mchezo mwingine ambao ulikuwa muhimu kwetu ambapo adi dakika ya 80 tulikuwa tukiongoza bao 2-1 dhidi ya timu toka Kagera mchezaji wetu aliweka mpira kifuani na mwamuzi akasema amenawa akaamuru ipigwe penalti ikatokea vurugu na mchezo ukastishwa na wezetu wakachukua pointi tatu.
“Baada ya matukio yale mimi nikaamua kujiweka pembeni na nikabakia na timu ya Veteran msoma nikiwa kama mchezaji,lakini baada ya matokeo yale timu ya Polisi Mara alikabidhiwa Ally Mchumila ambapo aliamua kutumia ushawishi mkubwa ili kudirudishia katika kikosi hicho nilikataa lakini baadae nilikubali na  niliifungia timu hiyo bao 3 muhimu ambazo ziliipandisha timu hiyo adi ligi daraja ya kwanza.
“Lakini baada ya kufanya vizuri uongozi wa timu hiyo ulikosa busara na hekima wakaamua kumtimua Ally Mchumila kwa kashifa na kibaya zaidi walimleta kocha ambaye uwezo wake ni mdogo kuliko ule wa Mchumila,na mimi kutokana na kwamba nilikubari kutumikia timu kwa heshima ya mchumila nikaamua kuachana na timu hiyo na mwaka 2012 nikatangaza kutundika daruga huku bado nikiwa na uwezo mkuwa,aneleza Magoe huku hakishusha pumzi ndefu kisha anaendelea;-
Woga ulimkimbiza SC Villa ya Uganda Pamoja na Kitwe Wanderers ya Zambia.
“wakati nilipokuwa RTC Kagera kabla ya kwenda Fc Leopard ya Kenya nilisajiliwa na SC villa ya Uganda kipindi Villa walikuwa hawakamatiki nilienda hadi uganda baada ya kukaa pale kwa siku Kadhaa woga ukanijia kutokana na kwamba sikuwa mzoefu wa kucheza nje ya Tanzania na mazingira ya Uganda yaliniogopesha nikaamua kutoroka na kurudi RTC Kagera.
“Pia wakati ligi ikiwa inaendelea timu yetu ilisafiri  kucheza mechi za ligi nyanda za juu kusini katika mikoa ya Iringa,Ruvuma,Iringa,Mbeya na Sumbawanga kumbe wakati wa ziara hiyo Zambia walituma viongozi wao hapa nchini ili kunifuatilia,nakumbuka tulipiga kambi Tunduma tukijiandaa na safari ya mkwenda Sumbawanga.
“Viongozi wa Kitwe wakanifuata kambini na kunieleza nia yao ya kunisajili niliwakubaria na baadae nikaondoka nao hadi nchini Zambia nikaenda hadi katika ofsi za timu hiyo,kwa muda huo tatizo kuwa sikuwa na Vibari vya kuniruhusu kufanya kazi Zambia baadaye niliwadaganya kuwa wakati utaratibu wa kukamilisha uhamisho unaendelea  waniruhusu nirudi Tanzania na nikawahaidi kurejea Zambia baada ya siku chache kitu ambacho walilidhia.
“Baada ya kuondoka nikatokomea mitini kikubwa kilichosababisha ni woga wa kucheza nje ya Tanzania tatizo likiwa ni kukosa uzoefu  katika mechi za kimataifa na nikarudi RTC Kagera na wazo la Zambia Likapotea moja kwa moja.
Ushirikina michezoni Kenya.
“Kwa kipindi chote ambacho nimechezea timu za Kenya sijakutana na vitendo vya Imani za kishirikina wachezaji wa Kenya wanafanya sana mazoezi na uwezo wao uwanjani ni mkubwa sana kuliko Tanzania timu nyingi za hapa nchini adi zile za vijijini unakuta adi jenzi za kuvaa siku ya mechi zinalala kwa mgaga wa jadi.
Balaa amecheza ligi Mbili kwa wakati mmoja.
“wakati nachezea Sonney Sugar ya Kenya mwaka 2005-2009 kuna kipindi nilichezea Timu ya polisi mara pasipo viongozi wa Sonney Sugara kujua kipindi hicho ligi ya Tanzania ilichezwa kwa makundi na iliisha kwa muda mfupi.
“kikubwa kilichonisaidia ni ligi ya Kenya ukishachezea miaka 4 unaruhusikwa kuchaza bila ITC kwa kuwa tayari unakuwa mchezaji huru na wanakutambua kama mchezaji halali wanchini hiyo,hivyo unakuwa mchezaji wa kawida na ufuatiliwi,hapo nikapata mwanya wa kurudi Tanzania na kuchezea timu ya Polisi mara na baadae kurudi tena Kenya.
Kuchaguliwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya.
“Kocha wa timu ya Taifa ya Kenya wakati wa michuano mbali mbali ya ligi nchini humo alitokea kunogewa na kiwango changu na alisahau kuwa mimi ni Mtanzania akaongea na viongozi wa timu ya FC leopard nia yake ni kuniita katika timu ya Taifa ya Kenya baada ya kuambiwa mimi ni Mtanzania alisikitika sana.
  “Ingawa  baada ya kuanza kusakata kandanda nchini Kenya sikupata tena nafsi ya kutumikia timu ya Taifa ya Tanzania kutokana na ubovu wa techinologia ya kipindi kile sikufikiria kubadilisha uraia ili kuchezea timu ya Taifa ya Kenya kutokana na matendo ya kinyama yaliyokuwa yakifanyia uwanjani nchini Kenya.
   “Kuna kipindi nilishuudia watu saba walikufa uwanjani ilikuwa kati ya Gormahia na FC Leopard hali ambayo ilinisikitisha sana polisi wa Kenya uwanjani walikuwa wakiweka ulizi kwa wachezaji peke yao  mashabiki hata kama wakitwangana ngumi walikuwa hawaingilii adi yatokee maafa.
“Pia utamaduni wa wachezaji wa nchini  Kenya ni mgumu sana ikilinganishwa na Tanzania,mnaweza mkalala chumba kimoja kila mtu asubuhi anaamka kivyake hata salamu hakuna mnakuna mazoezini, kiasi kwamba unaweza ukaumwa usiku na ukashituka wezako wote wameondoka mara nyingi hata mazoezini tulikuwa tukiendelea na stori za kawaida bila salama.
“kwa matukio hayo moyo wangu ulikataa kubadilisha uraia ili kuchezea timu ya taifa ya Kenya niliogopa wenyeji wangeweza kunifanyia kitu kibaya kulinnga na maisha yao yalivyo.
Licha ya Masheh kuvukiza ubani Tulilabwa 6-0
“Kiukweli mpira Burudani kwa kuwa una vimbwanga vingi wakati nasakata kandanda costal stars ya Mombasa walikuja mashehe wa kiislam siku moja kabla ya kuvaana na Kanon Yaunde ya comeroon katika kombe la washindi basi usiku kuanzia saa nne walikuja wazee wa kiislamu na wakapiga dua na kuvukiza ubani hadi usiku wa manane  tukio lile lilituchosha sana wachezaji ukizingati tulilala masaa machache sana kabla ya mchezo.
   “Siku ya mechi kutokana na uchovu tulikimbizwa kama watoto wadogo katika uwanja wa nyumbani na comeroon wakatukukung’uta bao 2-0 kabla ya kutushushia vua ya mawe nchini comeroon na kutufungisha vilago pamoja na dua zetu.
Tanzania na ushirikina Damu Damu.
“sisi Tanzania tunasifika kwa kuwa na matukio ya Imani za kishirikina michezoni,nakumbuka wakati nachezea timu ya Maji Mara Tulienda katika mashindo ya kuuania kupanda daraja kwanza katika kituo cha Tabora sisi tulikuwa jukwani ambapo siku hiyo walicheza kati ya polisi Tabora  dhidi ya timu ya Boma  Ulambo ambapo adi kipindi cha kwanza kilipomalizika Polisi walikuwa mbele kwa bao 2-0.
“kipindi cha pili yalitokea maajabu ambayo kwangu yalikuwa mageni ambapo upepo ulianza kuvuma toka kati kati ya uwanja kuelekea golini kwa polisi Tabora na muda wote wa mchezo walielemewa kiasi kwamba mpira ulikuwa golini kwao,huku boma ya ulambo wakifanya mashambulizi ya mara kwa mara na wakafanikiwa kurudisha bao zote na kuongeza bao la ushindi cha kushangaza mwamzi alipopuliza kipenga kuashiria mpira umeisha na upepo ukakata huku ulambo wakaibuka na ushindi wa bao 3-2,hapo ndipo nilipoanza kuamini mambo ya ushirikina uwanjani.
“Tukio lingine bado tukiwa Tabora timu ya Maji Mara ilichezaja na Shinyanga Shooting kilichotokea katika mchezo huo waliingia nyuki uwanjani wachazaji wa Maji Mara peke yake ndio tuliwaona wale nyuki tulijaribu kumweleza mwamuzi alituona kama watu wa ajabu kwa kuwa yeye hakuwaona wale nyuki wapinzani wetu walitushambulia sana,kutokana na wale nyuki sisi tulicheza kwa woga na hadi mwisho wa mchezo Shinyanga shutooting wakaibuka na ushindi wa bao 4-3 na Nyuki wakatoeka uwanjani.
Soka la kipindi kile na Sasa.
“Soka la kipindi kile lilitawaliwa na ubabe mwingi pamoja lugha chafu uwanjani beki alikuwa akikunyajua anakunyanyua kweli muda mwingine ukizubaa mwenzako anaweza akakuchoma kidole jichoni bila sababu za msingi na sharia zilikuwa ngumu ,beki amekuchezea faulo mbaya lakini mwamuzi anaendelea na mpira.
“kitu ambacho kilikuwa kikinisaidia mimi ni kiburi na ngumi kutokana na mazoezi ambayo nilikuwa nayafanya ilikuwa beki akinizoa mara kadhaa  narusha ngumi muda mwingine mwamuzi alikuwa hatoi kadi hata kama ukirusha ngumi kwa kuangalia uzito wa faulo uliyokufanyiwa.
“lakini mpira wa sasa sheria  ziko vizuri lakini wachazaji ni wavivu kufanya mazoezi na kujituma uwanjani ikilinganishwa na sisi kipindi kile.
Jezi yake noma.
“uwezi kuamini jenzi ambayo ilikuwa ikivaliwa na mimi kipindi kile ilikuwa ngumu kuvaliwa na mtu mwingine bada ya kuchezea kwa kuwa ilikuwa ikichakaa sana baada ya kuchezea kutokana kashi kashi za uwanjani.
“mara nyingi ba
ada ya dakika 90 nikitoka uwanjani kama sio jenzi basi bukta lazima ichanike,Mabeki ambao nilikuwa nakutana nao walikuwa wakatili sana ambapo kuchaniwa jezi ilikuwa ni kitu cha kawaida kwetu sisi washambuliaji.
Adi leo anamwota Ucheche.
Aliyekuwa beki wa Timu ya Sigara ya Jijini Dar es salam Saidi Ucheche kila nikimkumbuka alikuwa anatisha muda mwingine adi nacheka peke yangu kwa kuwa Ucheche alikuwa na mwili kama nyumba,kuna siku tukiwa uwanjani alinipa vitisho akaniambia wewe dogo unajifanya mjanja leo utaona.
“basi kuna mpira mmoja ulipigwa juu mimi nikaukimbilia gafla nikasiki kishindo kama cha gari moshi nikaruka haraka kumkwepa yule bwana kwa jinsi alivyoruka vibaya endapo ningikutana nae angenitoa meno hata hivyo mwamuzi aliona ikawa faulo.
“zamani mabeki wazuri walikuwa wengi na walikuwa wakitafuna sana miguu ya washambuliaji na kikubwa ambacho kilitusaidia ni mazoezi pamoja na ujanja beki mwingine ambaye nilikuwa namweshimu ni wille Martin.
Wachezaji anaowakubari.
“wachezaji wa zuri hapa nchini kwa sasa ni wachache sana lakini naheshimu sana uwezo wa Nurudin Bakari,Athumain Idd [Chuji] Pamoja na Amri Kiemba.
Tukio kali.
“kuna mchezo ulifanyika mkoani mara kati ya Maji Mara na Duma Fc kuna tukio lilitokea katika soka hata ulaya halijawai tokea,ilipigwa cross toka winga ya kushoto  kuelekea golini kwa  Duma mshambuliaji wa Maji alipiga ule mpira ili kupasia wavu kitu ambacho kilitokea ule mpira uligonga mwamba kisha mpira ukapandisha hadi mtambaa wa juu wa goli huku ukiwa unazunguka na kaendelea kuambaa katika mtambaa wa juu adi mwisho huku wachezaji wa timu zote mbili waliruka vichwa pale golini baadae mpira ukadondoka upande wa mlingoti wa pili wa goli na mabeki wakaokoa,tukio hili liliwashitua sana watu.
Makundi 4 ya wachezaji.
“Mpira haushuki kama roho mtakatifu mpira ni mazoezi na akili ya mchezo,katika mpira kuna wachazaji wale ambao wanafanya mazoezi ya kocha na mazoezi Binafsi   aina ya wachezaji hao katika mechi  mazozini hawachezi vizuri lakini wanatisha katika mashindano,kundi lingini ni wachezaji wanaotegemea mazoezi ya mwalimu mechi za mazoezini huwa wanakimbiza sana lakini katika mechi za mashindano marazote wanachemka.
“kundi la tatu ni wachezaji wenye uwezo wakunyang’anya mpira uwanjani  na kumiliki mpira wachezaji ambao ni wachache hapa nchini,na kundi la mwisho ni wachzaji wenye nguvu na uzito wa kutocha ili kujua uzito wa mchezaji uwanjani unafahamika pindi wachezaji wanapopgongana hapo ndipo mchezaji anaju amegongana na mtu mwepesi au mzito na ikatokea timu yenu ina wachezaji wachache wenye uzito mkubwa ushindi kwenu ni maigizo.
“Asilimia kubwa ya wachezaji tulionao hapa nchini kwa sasa wapokatika kundi la pili ni wachezaji ambapo wanategeea mazoezi ya mwalimu pekee vile vile hawana uzito wa kutosha wala uwezo wa kunyang’anya mipira kwa timu pinzani kitu ambacho kinasababishwa na mazoezi hafifu na wengi wao wamejiingiza katka suala la ulevi na wanawake.
Makocha.
“TFF wanadhamana ya kuzalisha makochawa kutosha bila upendeleo na pasipo kujali maeneo huku mikoani wapo watu wegi ambapo wanaitaji kupata mafunzo na vyeti bora vya ukocha,bado makocha wengi tuliopo hapa nchini tumepata kozi ya hawali ambapo tuna vyeti vya kawaida katika mpira.
   “Ili kufikia mafanikio katika soka letu lazima tukamilike katika idara zote hasa idara ya ukocha ambapo mara nyingi tunashuudi wanaletwa walimu toka nje ambao hawana msaada kwetu,TTF lazima walione hilo.
“ushauri kwa timu ya Taifa & mkoa wa Mara.
“Timu ya taifa japo kuwa kwa kiasi furani inajitahidi kucheza lakini bado hawafanyi vinzuri nawashauri TFF warudishe taifa Cup kama ilivyokuwa kipindi kile ilisaidia sana kupata wachezaji wa timu ya taifa pia wakuze vijana toka chini ili kuendana na kasi ya soka la kisasa.
“Na ili kuendeleza soka la mkoani mara viongozi warudishe Imani kwa wananchi kupenda soka kwa kufanya yale yanayotakiwa katika mpira kwa usahihi,bila hivyo ligi kuu tutaisikia kwenye Tv,Radio na Magazeti.
Baada ya kustaafu Soka.
“nilizaliwa mwaka1971 hadi kufikia 2013, nina mke na  watoto 6,nafanya biashara ndogo ndogo pia mimi ni kocha,kikubwa nashukuru mungu maisha yangu ingwa ni ya kawaida ila ni mazuri yote hayo yametokana na mpira,hivi ndivyo anavyoitimisha Magoe katika simulizi ya maisha yake ya soka baada ya  maojiano maalum na gazeti namba moja la michezo na burudani hapa nchini nazungumzia Championi.
Mwishoo!!!!!


Chapisha Maoni