Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Sentahafu wa Borussia Dortmund Mats Hummels ameweka wazi kuwa hana mpango wa kutimka klabuni hapo msimu huu.

Hata hivyo, beki huyo mwenye umri wa miaka 26, mshindi wa kombe la dunia, ameshindwa kuihakikiashia timu hiyo iwapo atakuwa na maisha marefu kwao baada ya kusema atakuwepo hapo angalau kwa mwaka mmoja zaidi.

Habari hizo za Hammels zinakuwa ni pigo kubwa kwa Manchester United ambao tangu mwaka jana wamekuwa wakihangaika kupata saini yake.

Hemmels mwenyewe anasema ni jambo la kuvutia kuwindwa na timu kama Manchester United lakini kwa sasa bado anahitaji kuendelea kukaa Ujerumani.

Huku washkaji zake  Mario Gotze na Robert Lewandowski wakiwa wameshatimka Borussia Dortmund katika vipindi tofauti, Hammels anaona kwa upande wake si jambo sahihi kuitosa klabu hiyo msimu huu.
Mats Hummels of Borussia Dortmund is greeted by fans waiting outside a hotel in Singapore on Wednesday
Mats Hummels wa Borussia Dortmund akiwasabahi washabiki wa timu hiyo huko Singapore siku ya Jumatano
Hummels smiles as he talks to the media during a press conference at the Fullerton Hotel in Singapore
Hummels akifurahi kwenye mkutano wa waandishi wa habari kwenye hotel ya Fullerton huko Singapore
The World Cup winner trains with his teammates in Tokyo on Monday on their Asian tour
Hummels akiwa mazoezini na wachezaji wenzake huko Mashariki ya mbali
SALUTI5


Chapisha Maoni