Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Lionel Messi anavaa jezi namba 10.
Neymar anavaa jezi namba 10.
Wayne Rooney anavaa jezi namba 10
Washindi wa hivi karibuni wa Ballon d’Or wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia Michael Owen, Ronaldinho Gaucho na Ricaldo Kaka wote walikua wakivaa jezi namba 10.
Moja ya kukua kwa umaarufu wa jezi no. 10 ni kuwahi kuvaliwa na wachezaji bora wa muda wote Ulimwenguni, Pele pamoja na Diego Armando Maradona.
Hilo limechangia kwa kiasi kikubwa jezi hii kuwa na mvuto wa aina yake na kupendwa na mastaa wengi wa soka.
Lakini sababu nyingine ambayo ndiyo ilikua chanzo cha Pele na Maradona kuvaa jezi hiyo kubwa kabisa katika soka ilikuwa ni utamaduni wa kawaida wa kupanga first eleven.
Katika kikosi cha wachezaji 11 wa kwanza, jezi ziligawiwa kuanzia yenye namba ndogo kutoka kwa golikipa hadi kwa mchezaji wa misho namba 11 kulingana na nafasi uwanjani.
Hivyo automatic kutokana na position zao, Pele na Maradona wakajikuta wakigawiwa jezi namba 10 kama washambuliaji wa timu zao.
Mfumo wa mpira ulipobadilika na kuwa 4 4 2 uliwafanya washambuliaji wa mbele wawili mmoja kuvaa jezi namba 10 na mwingine namba 9. Hali hii ikasababisha pia jezi namba 9 kuwa pia na umaarufu wa aina yake. Inavaliwa na Luis Suarez, Samuel Eto’o akiwa Barcelona pamoja na Ronaldo De Lima.
Lakini mabadiliko hayo ya jezi yamepelekea wachezaji wengine kuchagua jezi zenye namba kubwa zaidi ya zilizopo ndani ya 11. David Beckham alichagua jezi no.23 alipotua Madrid na amestaafu akivaa hiyo.
Picha: Magwiji wa soka wenye jezi nambari 10 mgongoni


Mchezaji bora wa Dunia mara nne, Lionel Messi wa Argentina.
Mchezaji bora wa Dunia mara nne, Lionel Messi wa Argentina.
Nyota anayetegemewa kufanya maajabu kwenye kikosi cha Brazil kinachoshiriki Kombe la Dunia Brazil, Neymar Dos Santos.
Nyota anayetegemewa kufanya maajabu kwenye kikosi cha Brazil kinachoshiriki Kombe la Dunia Brazil, Neymar Dos Santos.
 Zinedine Zidane ambaye aliipa ubingwa wa Dunia Ufaransa mwaka 1998. Hapo ilikuwa kati ya Ufaransa na Korea Kusini fainali za Kombe la Dunia 2006.
Zinedine Zidane ambaye aliipa ubingwa wa Dunia Ufaransa mwaka 1998. Hapo ilikuwa kati ya Ufaransa na Korea Kusini fainali za Kombe la Dunia 2006.
Mchawi wa soka kutoka Brazil, Edson Arantes Do Nascimento 'Pele'. Neno 'Pele' linatokana na neno la kiingereza 'Pearl' lenye maana ya 'Lulu'. Mwaka 1969.
Mchawi wa soka kutoka Brazil, Edson Arantes Do Nascimento ‘Pele’. Neno ‘Pele’ linatokana na neno la kiingereza ‘Pearl’ lenye maana ya ‘Lulu’. Mwaka 1969.
London Donovan, mchezaji wa Marekani, ilikuwa mechi za kufudhu Kombe la Dunia, dhidi ya Costa Rica, Februari, 2014.
London Donovan, mchezaji wa Marekani, ilikuwa mechi za kufudhu Kombe la Dunia, dhidi ya Costa Rica, Februari, 2014.
Gwiji wa Italia 'Azzuri', Roberto Baggio.
Gwiji wa Italia ‘Azzuri’, Roberto Baggio.
Ronaldinho akikimbia na mpira kwenye mechi kati ya Brazil na Australia Kombe la Dunia 2006 lililofanyika nchini Ujerumani.
Ronaldinho akikimbia na mpira kwenye mechi kati ya Brazil na Australia Kombe la Dunia 2006 lililofanyika nchini Ujerumani.
Michael Owen akijaribu kuumiliki mpira kwenye mechi kati ya England na Paraguay katika mashindano ya Kombe la Dunia 2006.
Michael Owen akijaribu kuumiliki mpira kwenye mechi kati ya England na Paraguay katika mashindano ya Kombe la Dunia 2006.
Kaka wa Brazil, mechi kati ya Switzland na Brazil, 2006.
Kaka wa Brazil, mechi kati ya Switzland na Brazil, 2006.
Diego Maradona, anayegombania kofia ya ufalme wa soka kati yake na Pele wa Brazil.
Diego Maradona, anayegombania kofia ya ufalme wa soka kati yake na Pele wa Brazil.
Kipenzi cha watoto wa Malkia Wayne Rooney, England imeshindwa kufanya vizuri Brazil, na hivyo imeyaaga mashindano hayo huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi dhidi ya Costa Rica. Hapo ilikuwa kati ya Uruguay na England ambapo walifungwa 2-1 Juni 19, 2014.
Kipenzi cha watoto wa Malkia Wayne Rooney, England imeshindwa kufanya vizuri Brazil, na hivyo imeyaaga mashindano hayo huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi dhidi ya Costa Rica. Hapo ilikuwa kati ya Uruguay na England ambapo walifungwa 2-1 Juni 19, 2014.
Wesley Sneijder, kati ya Uholanzi na Hispania, ambapo waliwafunga Hispania 5-1 kwenye mashindano ya Kombe la Dunia nchini Brazil.
Wesley Sneijder, kati ya Uholanzi na Hispania, ambapo waliwafunga Hispania 5-1 kwenye mashindano ya Kombe la Dunia nchini Brazil. Picha na Yahoo News.




Chapisha Maoni