Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




TAREHE 28-03-2014-13:41






 LIGI kuu ya Vodacom Tanzania maarufu kama VPL imeendelea kushika kasi  huku timu mbali mbali zikiendelea kuchuana vilivyo ili jujihakikishia zinapata nafsi za kuwakisha nchi katika michuano ya kimataifa msimu ujao huku zingine zikipigana vilivyo ili zisikumbwe na mkasi wa kushuka daraja adi ligi daraja la kwanza,hakika mvutano ni mkubwa sana.

Katika kinyanganyiro cha kuchukua ubingwa timu ambazo zimeingia katika vita hiyo ni Azam Fc pamoja na timu ya Yanga timu ambazo zimeonekana kukamiana vilivyo kwa kuwa kila timu inaitaji pointi tatu muhimu ili kujihakikishia nafasi zuri ya kuchukua ubingwa ambapo takwimu zinaonyesha kuwa kila timu ina nafasi ya kunyakua ubingwa katika ligi hiyo.

Wanalamba lamba azam Fc wanapewa nafsi kutokana kuongoza ligi hiyo kwa tofauti ya poinnti 4 huku ikiwa imecheza mechi 22 mkononi ingawa moja ya mechi ambazo zimesalia ni mechi ambazo zinaelezwa kuwa ngumu kwa kuwa moja ya mechi hizo ni dhidi ya Simba,kagera sugar pamoja na ile ya ving’ang’anizi watoto wa Mbeya City.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo wazee wa Jangwani  Dar esam Yang Africans wao wanapewa nafsi ya kutetea ubingwa wao kwa kuwa wamebakiza mechi nyingi ambapo mechi hizo sio ngumu ikilinganishwa na mechi za wapinzani wao Azam Fc ingawa moja mechi hizo ni mchezo dhidi ya wapinzani wao wa Jadi wekundu wa msimbazi simba timu ambayo  kwa misimu miwili sasa haijafanya vinzuri kutokana na migorogo mingi ambayo inafurukuta katika kalabu hiyo,kwa takwimu hizo  kila timu kati ya yanga pamoja na Azam zote zinanafsi zuri za kufunzu licha ya Mbeya City kuendelea kunyatia kwa nyuma nayo ikipigania nafsi mbili za juu.

Vile vile ligi kuu ya Vodacom Tanzania kwa msimu huu tumeshuhudia mabadiliko makubwa baada ya ujio wa kishindo wa mbeya City pamoja na kuimalika kwa timu ya Costal Union toka mkoani Tanga ali hiyo imesababisha timu kubwa hapa nchini kama mtibwa Sugar kupoteza nafsi zao kutokana na uwekezaji mdogo ambao timu hiyo imefanya kwa msimu huu  huku baadhi ya wakereketwa wa masuala ya soka wakidai kuwa benji la ufundi la mtibwa sugar halijajipanga vizuri.

Licha ya yote vita nyingine ambayo kwa upande mwingine kama TFF wasipokaa sawa inaweza ikatawaliwa na Fitina kubwa ni ile ya kuchuka Daraja ambapo kila timu inaitaji kubaki ligi kuu  hali ambayo inaweza ikasababisha kuwepo kwa mazingira  ya timu kuuza mechi au kununua mechi hii inachagizwa na udhamini mnono ambao azam Fc wameutoa kwa vilabu vyote vya ligi kuu kotokana na haki za matangazo.
Timu hizo ambazo zipo katika mstari mwekundu wa kushuka daraja ni pamoja na wauza mitumba wa Ilala ashati united wenye pointi 18 baada ya kucheza mechi 22,wafunga buti toka Arusha  JKT oljoro ambao wana pointi 15 baada ya kukiputa mara 22 huku  Rhino Rangers wakiendelea kuburuza mkia katika ligi hiyo kwa kufikisha pointi 13 mara baada ya kucheza mechi 22 hali ambayo inaashiria kuwa Tayari taa nyekundu imeshawaka kwa wageni hao ambao walipanda daraja msimu uliopita.

Kwa maana hiyo adi kufikia hivi sasa bado ni kitendawili kikubwa kujua kati ya yanga au Azam  ni nani kati ya hao atachukua kombe msimu huu, ingawa  Azam Fc inapewa nafsi kubwa ya kuchukua Taji hilo kwa kuwa tayari inaongoza kwa tofauti ya pointi nne  ambapo amefkisha pointi 47 huku akifuatiwa na yanga yenye pointi 43.





Chapisha Maoni