Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



TIMU ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imeitandika Benin  mabao 4-1 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,mchezo ambao kiemba amecheza kwa kiwango cha hali ya juu.

Nadir Ali Harob ‘Cannavaro’ wa Yanga ndiye alianza kabla ya sAmri Kiemba wa Simba kuongeza la pili pia mabao mengine mawili ya stars yalifungwa na Thomas Ulimwengu kutoka TP Mazembe na Juma Luizio anayekipiga Zesco ya Zambia.
 
bao la kufutia machozi kwa upande wa Benin limefungwa na suanon fadel dakika ya 90

 
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Mwadini Ali, Shomary Kapombe, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Said Mourad dk75, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba/Salum Abubakar ‘Sure Boy’dk58, Haroun Chanongo/Said Ndemla dk77, Mrisho Ngassa/Juma Luizio dk60 na Thomas Ulimwengu/Khamis Mcha ‘Vialli’ dk86.

Benin; Farnoue Fabien/ Allagbe Saturnin dk46, Tossavi Eric, Ore Fortune/Dalmeida Sessy, Badarou Nana, Ogouchi Jean, Adeoti Jordan, Mama Seibom, Sessegnon Stephanne, Pote Mickael, Djigla David/Suanon Fadel dk49 na Dossou Jodel/Adudou Mohammed dk53.  


Chapisha Maoni