Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Kenya huenda ikatangazwa rasmi kuwa mwenyeji wa mashidano ya dunia ya riadha kwa vijana mwaka 2017, hiyo ni baada ya mji wa Greenboro wa Marekani kujiondoa na kuachia nafasi ya wazi nchi hiyo ya Afrika Mashariki yenye kusifika duniani kwa watimuaji hodari wa mbio.
Tangu awali Kenya ilianza kupata unafuu wa ushindani baada ya mji wa Bunos Aires wa Argentina kujitoa mapema.
Kenya iliwahi kuandaa mashindano ya dunia ya mbio ndefu za Cross Country mjini Mombasa mwaka 2007. Wakati Kenya ikisubiri tangazo tu, Uganda imeshinda ombi la kuandaa mashindano ya dunia ya mbio za Cross Country kwa mwaka 2017 baada ya kuushinda mji wa Manama wa Bahrain. Wakati ambapo mji wa Doha Qatar wenyewe umeshinda kuwa mwenyeji wa mbio za dunia za mwaka 2019.


Chapisha Maoni