Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Mchezajii wa kilabu ya Tottenham Emmanuel Adebayor amepewa mapumziko kwa mara ya pili msimu huu lakini hatma yake katika kilabu ya Spurs haijulikani.
Mchezaji huyo wa taifa la Togo mwenye umri wa miaka 31 ameandika kuhusu matatizo ya famili yake katika mtandao wa facebook na kusema kuwa alikuwa ameamua kujiua.
Atakosa mechi ya siku ya jumapili kati ya kilabu yake na Everton mbali na ziara ya Kuala Lumpur na baadaye nchini Sidney.
''Tumempa muda wa kusuluhisha mzozo na familia yake'',alisema kocha wa kilabu hiyo Mauricio Pochettino.Ni miasha yake ya kibinafsi .Niliongea naye mapema wiki hii,ni hali ngumu kwake''.
Adebayor alijiunga na klabu ya Spurs mwaka 2011 kutoka Manchester City kupitia mkopo kabla ya mabao 18 aliyofunga akiwa na Hotspurs kumwezesha kupewa kandarasi ya kudumu.


Chapisha Maoni