Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Niang akipokea simu mara baada ya kuwasili kwenye hoteli aliyofikia jijini Dar es Salaam

Mshambuliaji raia wa Senegal Papa Niang ameshawasili jijini Dar es Salaam leo taayari kwa ajili ya kuanza majaribio yake ya kujiunga na klabu ya ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba  SC.
Niang leo ataunganishwa moja kwa moja na kikosi cha Simba ambacho kitafanya mazoezi yake kwenye uwanja wa Boko ambako ndipo kikosi hicho kinafanya mazoezi yake kwa ajili ya kujiandaa na mechi za ligi kuu Tanzania bara inayotarajiwa kuanza Septemba 12 mwaka huu.
Niang akiwa mapokezi akipata maelekezo kwenye hoteli aliyofikia
Katika majaribio yake, endapo Niang ataonesha kiwango cha kumvutia kocha mkuu wa Simba Dylan Kerr pamoja na benchi zima la ufundi la kikosi hicho, basi huenda akapewa mkataba wa kuitumikia klabu hiyo ambayo imekuwa ikihaha kutafuta washambuliaji wa kigeni.
Hivi karibuni Simba ilimleta mshambuliaji wa kigeni kutoka Burundi Kelvin Ndayisenga ambaye alicheza kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya URA FC ya Uganda huku akifanikiwa kuifungia timu hiyo goli moja kwenye ushindi wa goli 2-1.
Inasemekana Simba imeachana na mshambuliaji huyo baada ya kushindwa kufikia makubaliano katika masuala ya pesa ambapo Ndayisenga alitaka dau kubwa Simba wakashindwa kufikia na kuamua kumruhusu aondoke.
Jamaa akiperuzi magazeti ya bongo kujua yaliyoandikwa kwenye kurasa za magazeti hayo
Jamaa akiperuzi magazeti ya bongo kujua yaliyoandikwa kwenye kurasa za leo
Dondoo kuhusu Niang
Jina kamili: Papa Niang
Tarehe ya kuzaliwa: 5Disemba, 1988 (miaka 26)
Mahali alipozaliwa: Matam Senegal
Urefu: Mita 1.81 
Nafasi anayocheza: Mshambuliaji
Klabu alizowahi kuzitumikia:
Kwasasa: Mchezaji huru
2005-2006: ASC Thies 
2007: FC OPA
2008: AC Oulu
2009-2012: FF Jaro
2013: FC Vostok
2013-2014: Al -Shabab SC
2014-2015: FC Mounana


Chapisha Maoni