Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Sasa ni uhakika kikosi cha Taifa Stars kesho jioni kinashuka dimbani kuivaa timu ya taifa ya Iaraq.
Stars itacheza na Iraq katika mechi ya kirafiki ya mazoezi ambayo haina watazamaji.

“Itakuwa ni mechi ya kirafiki tu, ni mechi mazoezi ili kujiweka fiti. Baada ya hapo tutarajia kucheza na Libya,” alisema Kocha Mkuu wa Stars, Charles Boniface Mkwasa.

“Hii ni mechi si kwa ajili ya rank za Fifa au vinginevyo, ni kw aajili ya kujipima na kujiweka sawa,” alisema.
Iraq na Libya nao wamweka kambi katika hoteli kubwa ya The Green Park ambayo Stars imeweka kambi.
Hoteli hiyo ipo mlimani kabisa katika mji huu wa Kartepe nchini Uturuki na inamiliki viwanja vitano vya mazoezi.
Mkuu wa Msafara wa Kikosi cha timu ya taifa, Msafiri Mgoyi amesema ameridhishwa na kambi ambayo Taifa Stars wameweka.


Mgoyi amesema ameridhika baada ya Stars kuwasili katika mji mdogo wa Kartepe ambaye uko juu kabisa ya mlima.


Chapisha Maoni