Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Alex Mapunda,Iringa
UKARABATI wa uwanja wa Maji Maji Mkoani Ruvuma umeshakamirika na Tayari TFF imetoa mkono wa Baraka kwa  Maji Maji kutumia uwanja huo kwa mechi za nyumbani.
Akizungumza na Chanzo cha Gazeti hili toka Songea Meneja wa timu ya Maji Maji God Mvula alisema uwanja huo umeshakamirika kwa Asilimia mia na siku ya ufunguzi wa ligi kuu ya Vodacom  tarehe 12 watapepetana na JKT Ruvu toka Pwani katika uwanja wa Maji Maji.
“Uwanja umekamirika na sisi tumekamirika tupo tayari kwa kazi ili pupeperusha vyema bendera ya mkoa wetu,kila mechi kwetu ni fainali”alisema Mvula.
Kwa upande mwingine kocha mpya wa timu ya Maji Maji toka Finland Mike Keeney Holonton anaendelea vizuri na mazoezi ya timu hiyo na wachezaji wote wanafurahia mafunzo yake.
kwa upande mwingine,TIMU ya Liuli Stars toka ziwani Nyasa inatarajia kuingia kambini mwishoni wa wiki hii ili kujiandaa na ligi Daraja la tatu Mkoa.
Licha ya kuingia Kambini timu hiyo imekumbwa na ukata na inawaomba wadau na wapenzi wa timu hiyo kwa nchi zima kutuma michango yao ili kusaidia timu.
“Kuna watu wamehaidi kutuchangia baada ya kupata taarifa zetu kupitia Gazeti la Championi wiki zilizopita,pia Helman Maklasi ameshatutumia Elfu Hamsini,tunaomba na wengine waendelee”alisema muddy Songambele kocha wa timu hiyo.


Chapisha Maoni