Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



TFF-MALINZIShirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), limetuma salamu za pongezi kwa viongozi wa mpira wa miguu nchini waliochaguliwa kuwa wabunge na madiwani katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.
Viongozi waliochaguliwa katika nafasi ya Ubunge ni John Kadutu – mbunge wa Ulyankulu – Tabora, (mjumbe wa mkutano mkuu kutoka Mwanza) na Alex Gashaza – mbunge wa Ngara (Makamu mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Kagera)
Aidha waliochaguliwa Udiwani katika maeneo yao ni Khalid Abdallah (Mjumbe wa kamati ya Utendaji – TFF),  Yusuph Kitumbo- (Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tabora), Omari Gindi- (Mwnyekiti wa Chama cha mpira wa Miguu mkoa wa Kigoma), Bathromeo Kimaro - (Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Singida) na Omar Kinyeto (Mjumbe wa mkutano mkuu mkoa wa Singida),  Golden Sanga (Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Ruvuma), Pachal Kihanga (Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa mkoa Morogoro), Yusuf Manji (Mwenyekiti wa klabu ya Yanga SC) ambao wote ni wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF.
TFF inawaomba kutumikia halmashauri zao kwa mafanikio na kutilia mkazo kuhifadhi maeneo ya wazi kwa ajili ya michezo mbalimbali hususani mpira wa miguu mashuleni.


Chapisha Maoni