Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



 
Na Sophia Mwaipyana,Mbeya

Mkocha  msaidizi aliyekuwa anawaanda  wachezaji wa maboresho katika  timu yaTaifa Salum Mayanga atangaza majina  ya wachezaji 16 ambao wamechaguliwa kujiunga katika timu ya Taifa.
 
Kikosi hicho ambacho kiliweka kambi ya taifa  Tukuyu wilayani Rugwe mkoania Mbeya  ambao waliingia na wachezaji 34 kambini mwezi ulio pita tarehe 22 na kufikia tamati leo.
 
Akiongea na wandishi wa habari leo asubuhi katika ukumbi wa Hill view aliwataja wachezaji hao kuwa ni mlinda mlango Benedict Mlekwa toka (Mara),walinzi wakati wawili Emma  Simwanda ( Temeke), Joram Mgeveje (Iringa).
 
Walinzi wa pembeni Omari Kindamba (Temeke), Edward Mayunga (Kaskazini Pemba),Shirazy Sozigwa (Illala) na viungo wa ulinzi ambao ni Yussuf Mlipili (Temeke) na Said Ally (Mjini Magharibi).
 
Pia aliwataja viungo wa ushambuliaji kuwa ni Abubakar Mohamed (Kusini Unguja), Hashimu Magona (Shinyanga) na viungo wa pembeni ni Omari Nyenje (Mtwara), na Chunga Zito (Manyara).
 
Kwaupande wa safu ya ushambuliaji  ni Mohammed Saidi(Kusini Pemba),Ayubu Lipati (Ilala),Abdurahman Ally (Mjini Magharibi) na Paul Bundara (Ilala) na wachezaji wa chini ya umri wa miaka 20 (U20), Mbwana Musa (Tanga) na Bayaga Fabian (Mbeya).
 
Alisema kuwawachezaji walio chaguliwa wataondoka  leo kuelekea Dar es salaam kwajili ya kuungana na wachezaji wengi kwajili ya kunda kikosi cha Taifa.
 
Naambao hawaja changuliwa katika kikosi hicho watabaki katika uwangalizi wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF).



Chapisha Maoni