Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Na Sophia Mwaipyana,Mbeya

Mabigwa wa ligi ya mkoa  wa Mbeya Wenda Fc  wamesema wataakikisha  kuto uzima moto walio toka nao katika ligi daraja la tatu hadi ndoto yao ya kushiriki ligi daraja la kwanza  msimu ujaoo itakapo timia.

Timu hiyo ambayo imeshiriki ligi daraja la tatu kwa miaka mitatu mfurulizo bila kufanikiwa kupata nafasi ya kuuwakilisha mkoa wa Mbeya na kuipata nafasi hiyo mwaka huu waliyo kuwa wakiingojea kwa hamu miaka nenda mika rudi.

Timu ya Wenda Fc ambayo maskani yake ni  katika mji mdogo wa Mbalizi wilaya ya Mbeya vijijini nitimu yenye washabiki wengi mkoani hapa  kutokana na timu hiyo kuwa na uwezo mkubwa wa kulisakata kabumbu na ina wachezaji wanao jituma kama ilivyo timu ya Mbeya City.

Akiongea na Championi Ijuma  katibu wa Wenda Fc Muhamed Maurid alisema kuwa  nafasi waliyo kuwa tukiipigania kila siku na kuitamani kuipata sasa wameipata na  watahakikisha wanaitumia vizuri hadi kutimiza malengo yao ya kucheza daraja la kwanza msimu ujao.

“kwasasa tunajipanga kuanda kikosi kizuri kwajili ya ligi ya kanda ambayo itaanza hivi karibuni,namshukuru mungu ligi imeisha na wachezaji wote wazima hatuna majerui hata mmoja hivyo naimani vijana wetu wata jitoa kama walivyo jitoa katika ligi iliyo pita”

“wadau wasoka na chama cha mpira mkoa  tunaomba wazidi kutusapoti kama walivyo tusapoti kipindi cha nyuma hadi tukapata mafanikio ambayo yametufikisha hapa tulipo tunaitaji  kusonga mbele zaidi hadi tuongeze timu katika ligi kuu yani lengo letu kubwa ni kuwa kama timu ya Mbeya City ilipo sasa”

Timu ya wenda Fc imeshuka timbani mara tano na haijapoteza mchezo wake hata mmoja  hivyo kuwafanya watoke na pointi zote kumi na tano katika hatua ya sita bora.
Mwisho


Chapisha Maoni