Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Na S ophia Mwaipyana,Mbeya

SANAA ni moja ya kazi ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuwainua wasanii kiuchumi na kulitangaza taifa nje ya nchi kupitia sanaa.

"Ngoma za asiri ni  moja ya kazi za kisanaa ambazo zinamtoa mtu kimaisha, zinainua uchumi wananchi kupitia wasanii, na zinaelimisha na kudumisha mila na desturi za ki Tanzania" ndivyo anavyosema msanii chipukizi wa nyimbo za asiri Asnah Litimba, 

Katika makala ya leo kwa mara ya kwanza na penda kuzungumzia msanii ambaye amekuwa akitamba katika radio mbali mbali Mkoani Mbeya na nyimbo za asiri za kabira la wa Yao.

Msanii huyo si mwingine bali anatambulika kwa jina la Asnah Litimba mkazi wa Masasi Wilayani Mtwala ambaye kwa sasa anaishi jijini Mbeya akifanya kazi zake za ujasiliamali katika eneo la Sido Mwanjelwa.

Asnah anasema kuwa jambo kuu ambalo limemsukuma kujiingiza katika sanaa ya muziki wa nyimbo za asiri hasa kabira la wayao ni kutokana na kabira hilo kutokujulikana sana kwenye nyimbo za asiri.

Anasema kuwa imekuwa ikimuumiza sana kwenye matamasha mengi na hata kwenye kumbi za starehe, maharusi na kwingineko nyimbo za rugha ya kiyao hazipigwi na kuonekana kama vile hakuna wasanii.

Msanii huyo alisema nyimbo za asiri zinamafundisho makubwa ukilinganisha na nyimbo za kizazi kipya ambapo wasanii wengi wamekuwa wakiimba nyimbo zenye ujumbe wa mapenzi na kuchangia kuharibu maadili kwa vijana nchini.

“Unajua nyimbo za asiri zimebeba ujumbe wa kuelimisha jamii husika kufuata maadili ambayo yalikuwa yakifanywa na mababu zetu tofauti na nyimbo za kileo” anasema Asnah.

Aliongeza kuwa kila kabira lina nyimbo zao za asiri na katika ujumbe mara nyingi nyimbo hizo zinazungumzia mambo yaliyomkuta, walikotoka, wanakoelekea na nanma ya kuepuka au kujikinga kwa jambo furani.

Alisema kuwa katika albamu yake ambayo ndiyo ya kwanza imebeba nyimbo (10) na kuzitaja baadhi yake kuwa ni ‘Husi milonga, Mtame pasi, na Mwanangu mwali.

Aidha alisema kuwa wimbo wa husimilonga unaelezea yaliyomkuta na ambayo yanaweza kumkuta mtu mwingine wakati wimbo wa Mtame pasi unazungumzia mabinti kutokumpenda kijana bira kumpeleleza au kuwauliza wazee ili kupata ushauri.

Pia katika wimbo wake wa Mwanangu mwali unazungumzia namna ya kumtunza mume ndani ya ndoa ili waweze kuitunza ndoa yao vizuri na kulea watoto wakiwa wanandoa walioshibana.

Anasema kuwa kipaji chake cha uimbaji alianza toka alipocheza ngoma ya unyago huko Mtwara na kudai kuwa hadi sasa ananyimbo zaidi ya 100 ambazo ni mchanganyiko wa makabira mengine ambayo amewahi kuishi nao.

Akizungumzia namna watu walivyozipokea nyimbo zake Asnah anasema kuwa kwa mara ya kwanza alipofanyiwa mahojiano na kituo kimoja cha radio jijini Mbeya watu wengi walipiga simu wakitaka kujua namna ya kupata CD za nyimbo zake.

Alisema kuwa watu kutoka mikoa jirani ambako kituo hicho cha radio kinafika walimpongeza sana kwa kazi yake na kumtaka asirudi nyuma licha ya kutokuelea lugha ya kiyao.

Akitoa wito kwa wasanii Asnah alisema kuwa ni vyema wasanii wenye vipaji vyao wajizatiti katika nyimbo za siri kwani nazo nimekuwa zikikonga nyayo za mashabiki wengi nchini.

Alitoa mfano kwa wasanii kutoka Bostwana wanaojulikana zaidi kama Makhili khili na kusema kuwa wasanii hao wamejipatia umaalufu ndani na nje ya nchi ikiwemo Tanzania licha ya watu wengi kutoelewa lugha wanayozungumza.

Msanii huyo aliongeza kuwa nyimbo za asiri zimekuwa zikipendwa na watu wengi toka nchi mbali mbali siyo tu kwa sababu ya ujumbe bali hata mavazi, uchezaji wa aina yake na ndiyo maana Makhili khili walijipatia umaalufu duniani.

Mkoani Mbeya kumekuwepo na ongezeko la wasanii wa nyimbo za asiri hasa kwa kabira la wasafwa huku msanii ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kwenye maharusi na kumbi mbali mbali za sherehe ni Awilo Orijino.

Japo wapo wengi wasanii wa kabira la wasafwa ambao wametoa nyimbo zao ingawa wanafanana vionja vya nyimbo hizo ikiwa ni pamoja na baadhi ya ujumbe na mistari ya nyimbo pamoja na upigaji wa ghita lakini Awilo amekuwa juu sana ukilinganisha na wengine.

Pia makbira mengine yameanza kujitokeza katika Mkoa huu ikiwa ni pamoja na Kabila la wanyakyusa ambapo baadhi yao wamecheza na kuimba ngoma ya asiri ya Mang’oma na Kapote.

Ngoma ya mang’oma inaendana kabisa na uchezaji wa wasanii wa Makhili khili lakini tatizo kubwa ni kwamba wanakosa namna ya kujitangaza na kupata wafadhili ambao wanaweza kuwasaidia ili waweze utoa kitu bora.

Kwa wale ambao wameshafika Mkoani Mbeya na kusikiliza au kuona nyimbo za siri za Mkoa huo wanavyocheza na kuimba ni dhahili kuwa sanaa ya muziki kama bongo fleva haiwezi kufua dafu kutokana na ustadi wa uchezaji na uimbaji wa nyimbo hizo.

Tanzania kuna makabira mengi ambayo yananyimbo zao za asiri lakini kumekuwepo na ukilitimba kwa baadhi ya makabira kuona aibu au wanajiona kama kucheza nyimbo za asiri ni ushamba au ni udhalilishaji lakini huku moyoni wakizipenda.

Tumeona namna makhili khili wanavyovaa na kama ungekuwa udhalilishaji basi wasingejipatia umaalufu ule na kuweza kutembelea nchi mbali mbali ndani na nje ya bara la Africa.

Iwapo wasanii wangekuwa pia wanaimba nyimbo zao kwa kutumia pia mavazi ya asiri hata kama wanaimba nyimbo za bongo fleva bado wangeweza kujinyakulia sifa nyingi na kujitambulisha kuwa ni watanzania.

Katika makala haya napenda kutoa wito nikiungana msanii Asnah kwa kusema tudumishe mira zetu kwa kufuata maadili kupitia nyimbo za asiri uchezaji wa asiri na kadhalika ili tuitukuze Tanzania ndani na nje. 

MWISHO



Chapisha Maoni