Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Kamati ya ndani ya uendeshaji wa mashindao ya kombe la Kagame nchini Tanzania (LOC) imewasilisha malalamiko kwa katibu mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye juu ya vitendo vya utovu wa nidhamu viliyoonyeshwa na timu ya Gor Mahia.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa tarehe 18 Julai, Kocha mkuu wa Gor Mahia Frank Nuttal alionyesha inshala ya matusi kwa kidole, jambo liliopelekea kuzua zogo na washabiki wa mpira waliokuwepo uwanjani kushuhudia mchezo huo.
Wakati wa mapumziko pia timu ya Gor Mahia hawakupita mlango mkubwa wa kuingilia vyumbani, badala yake walitumia kuingilia na kutokea upande wa Kaskazini mwa uwanja wa Taifa, mlango ambao ni maalumu kwa wafanyakazi wa kituo cha runinga cha Supersport.
Lakini katika hali ya kushangaza jana katika mchezo wake dhidi ya Khartoum walirudia kutumia mlango ule ule kwa kuvunja kitasa cha mlango ili waweze kupita kuingia uwanjani kitu ambacho ni kinyume na kanuni na utaratibu wa mashindano.
LOC imeitaka CECAFA kuichukulia hatua kali timu ya Gor Mahia kutokana na vitendo hivyo ilivyovifanya vya kuharibu miundombinu ya uwanja wa Taifa, ambao unatumika kwa ajili ya michezo mbalimbali ya kimataifa.


Chapisha Maoni