Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na  Alex Mapunda,Iringa
TATIZO  la uhaba wa viwanja limejidhiirisha wazi mkoani Iringa baada ya hivi karibuni  mechi kati ya lugalo FC pamoja na Jako  FC kusimamishwa ili kupisha timu inayohaminika ina uhuru wa kutumia uwanja huo kutumia.

Mechi hiyo ambayo ilifanyika katika shule ya msingi Umoja ilivunjika mwazoni mwa kipindi cha pili ili kupisha timu nyingine ambapo hadi muda huo Lugalo ilikuwa mbele kwa bao 2-0 dhidi ya jako Fc.

Baada ya kumalizika mchezo huo kocha  wa Jako Fc Joshua michelle alisikitika sana kuhusu kitendo hicho na kuitaka manispaa kutenga maeneo zaidi ya viwanja ili kukunza na kundeleza michezo mkoani Iringa.

“nimeskitika sana tumekuja na mashabiki wetu,lakini tunaondoka bila mpira kumalizika,Sijui kwa nini,Tanzania tuna maeneo ya kutosha lakini tunashindwa kuwa na viwanja vya kutosha  vya michezo.

Pia moja ya shabiki ambaye aliudhuria kwenye mtanange huo Chris Tomas alisema kuwa  mpira wa Tanzania tutachelewa kuufikisha kule ambapo wezetu wapo kwa kuwa bado kutatua vitu vidogo vidogo tunatushindwa.

Mara nyingiImezoeleka  mpira wa miguu m unaweza kuvunjika ukitokea ugomvi baada ya timu husika kukwaruzana,timu kugomea mchezo au mwamuzi kuvurunda katika mchezo husika na si kwa sababu ya kupisha timu nyingine icheze.



Chapisha Maoni