Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 Lionel Messi crowned UEFA Best Player in Europe as Barcelona star tops vote ahead of

BAADA ya kushinda Kura zilizopigwa na Wanahabari toka Nchi 54 Wanachama wa UEFA,Messi ametawazwa kuwa mchezaji bora wa UEFA.


DONDOO MUHIMU KWA WACHEZAJI HAO TATU BORA:
Cristiano Ronaldo (Portugal – Real Madrid)
-Ndie Mfungaji Bora wa La Liga Msimu uliopita kwa kupachika Mabao 48 na pia kufungana na Messi na Neymar katika Ufungaji Bora wa UEFA CHAMPIONS LIGI.
-Alipachika Jumla ya Mabao 61 katika Mashindano yote akiwa na Real Madrid na hivyo kumpita Lejendari Alfredo Di Stéfano na kushika Nafasi ya Pili ya Ufiungaji Bora katika Historia ya Real.
-Alipiga Bao 5 katika Mechi moja hapo Aprili 5 Real ilipoibonda Granada Bao 9-1.
-Alimaliza Msimu kwa kupiga Hetitriki 3 mfululizo dhidi ya Espanyol, Getafe na Armenia.
 Messi (second right) and Ronaldo (right) look on as Peter Schmeichel (left) chats to Luis Suarez
Lionel Messi (Argentina – Barcelona)
-Alivunja Rekodi ya Telmo Zarra ya Bao 251 za La Liga na pia kuifungia Barcelona Mabao 58 katika Mashindano yote na kuiwezesha kutwaa Trebo, yaani kutwaa Ubingwa wa La Liga, Copa del Rey na UEFA CHAMPIONZ LIGI.
-Kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI alifunga Bao 10 na kufungana na Ronaldo na Neymar kama Wafungaji Bora wa 2014/15.
-Amefungana na Ronaldo wakiwa na Mabao 77 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na ana Mabao 80 katika Mashindano yote ya Klabu ya UEFA yakiwemo Mawili aliyofunga kwenye UEFA Super Cup Jumatatu Usiku dhidi ya Sevilla.
Luis Suárez (Uruguay – Barcelona)
-Alifunga Bao 2 katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI walipoibwaga Manchester City.
-Ni mmoja wa Mastraika Watatu wa Barcelona waliopiga Jumla ya Mabao 122 Msimu uliopita pamoja na Neymar na Messi.


Chapisha Maoni