Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Image result for jelamba viwanjani pichaTWIGA KUFUNGA DIMBA NA IVORY COAST
Timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) inayotarajiwa kuondoka mwishoni mwa mwezi Agosti kuelekea nchini Congo-Brazzavile kwenye Fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) imepangwa kufungua dimba na timu ya Wanawake ya Ivory Coast Septemba 6, 2105.
Twiga Stars iliyoweka kambi kisiwani Zanzibar kwa takribani mwezi mmoja sasa, itacheza mchezo wake pili Septemba 9, dhidi ya Nigeria kabla ya kumalizia mchezo wake wa mwisho hatua ya makundi dhidi ya wenyeji Congo-Brazzavile Septemba 12, 2105.

Jumla ya timu nane za Wanawake kutoka Barania Afrika zinashirki fainali hizo ambazo ni Nchi za Afrika Kusini, Cameroon, Ghana, Misri (wamejitoa) kundi B, na wenyeji Congo-Brazzavile, Ivory Coast, Nigeria na Tanzania kutoka kundi A.
Timu mbili za juu kutoka kila kundi zitafuzu kwa hatua ya nusu fainali.
MALINZI AIPONGEZA GEITA GOLD SC
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ameipongeza klabu ya Geita Gold SC inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza nchini (FDL) kwa kupata udhamini wa shilingi milioni mia tatu (USD 150,000) toka kampuni ya uchimbaji madini ya Geita Gold Mining LTD.
Katika salam zake za pongezi kwenda kwa uongozi wa klabu ya Geita, Malinzi ameipongeza klabu hiyo kwa hatua waliyofikia na zaidi kumshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Geita Gold Mining Terry Mullpeter kwa kuweza kuidhamini klabu hiyo.

Aidha Malinzi amewaomba viongozi na wanachama wa klabu hiyo kuheshimu na kuenzi udhamini huo, kwa kuwa na nidhamu na kucheza vizuri ili kuweza kuendelea kuitangaza vyema Geita Gold Mining Limited.
Malinzi ametoa wito kwa makampuni mengine kujitokeza na kuwekeza katika kudhamini vilabu vya ligi za madaraja ya chini ambazo hazina udhamini katika ligi zao, zikiwemo za daraja la kwanza, la pili, na mabingwa wa mikoa.
Klabu ya Geita Gold SC inakuwa miongoni mwa timu chache zenye udhamini wa uhakika katika timu zinazoshiriki ligi daraja la kwanza mwaka huu miongoni mwa timu 24 zilizopo, ligi inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 19 mwaka huu, ikiwa kundi C pamoja na timu za Panone, JKT Oljoro, Polisi Mara, Mbao FC, Polisi Tabora na JKT Kanembwa.
VILABU VYATAKIWA KUWASILISHA NAKALA YA MIKATABA TFF
Klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zinatakiwa kuwasilisha mikataba ya wachezaji wake- nakala tatu kwa kila mchezaji kwa ajili ya kuidhinishwa na TFF, kama ilivyoelekezwa katika Kanuni ya 69(1) na (8).

Baada ya mikataba hiyo kuidhinishwa ikiwa ni pamoja na kulipiwa ada ya sh. 50,000 kwa kila mmoja, nakala moja itakuwa ya klabu, nyingine ya mchezaji na moja itabaki TFF ili linapotokea tatizo la kimkataba uamuzi ufanywe na vyombo husika mara moja.
Pia klabu ya VPL inatakiwa kuwasilisha TFF orodha ya benchi lake la ufundi, mikataba ya maofisa wa benchi husika pamoja na nakala za vyeti vyao. Kwa mujibu wa Kanuni ya 72 (3), Kocha Mkuu anatakiwa kuwa na Leseni ya CAF isiyopungua ngazi B wakati Kocha Msaidizi anatakiwa kuwa na Leseni ya CAF isiyopungua ngazi C.
Kwa upande wa timu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL), Kocha Mkuu anatakiwa kuwa na Leseni ya CAF isiyopungua ngazi C wakati msaidizi anatakiwa kuwa na cheti kisichopungua ngazi ya Kati (Intermediate).
Hakuna kocha asiyekidhi makatwa hayo ya kikanuni atakayeruhusiwa kuongoza timu yoyote kwenye mechi za ligi hizo mbili. Pia viongozi wa klabu wasiozingatia maelekezo haya, wanakumbushwa kuwa wanakwenda kinyume cha kanuni. 
IMETOLEWA NA TFF:
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER


Chapisha Maoni