Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Ukiikumbuka Maji Maji ambayo ilikuwa inatikisa hapa nchini Miaka ya 1980 hadi 1990 uwezi kumweka kando John Kabisama ambaye alikuwa ni miongoni mwa viungo washambuliaji bora kuwai tokea katika timu Hiyo na Tanzania kwa ujumla.
Kabisama,mzaliwa wa Mbambabei Wilayani Nyasa alianza kusakata kabumbu katika Shule ya msingi Maji Maji zamani hikifahamika kama ‘Haideli’Songea Mjini.Amezungumza na Gazeti hili na kueleza mengi kuhusu Soka:
“Nilianza Kucheza soka la ushindani nikiwa na RTC ya Arusha mwaka 1977 ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja ya kwanza na nikiwa na timu hiyo nilipata bahati ya kuitwa kwenye timu ya taifa kutokana na umahili wangu wa uwanjani kwa mara ya kwanza na ya mwisho.
“Lakini mwaka 1978 nilijiunga na Kill Tex ya Arusha timu ambayo nilidumu nayo kwa misimu miwili ambapo baadae mwaka 1983 nikatimukia AICC pia ya arusha,timu ambayo niliichezea kwa mafanikio makubwa.
‘Mwaka 1885 Maji Maji ya Songea wakanichuka Toka AICC[timu ya ukumbi wa mikutano Arusha] kutokana na kiwango changu kuwa kikubwa sana nikiwa kama kiungo mshambuliaji ambapo kwa iliyewai kuniona nikicheza anavifahamu vitu vyangu, Maji Maji niliichezea kwa kwa mafanikio makubwa sana ambapo nikiwa na timu hiyo tulifanikiwa kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa mara mbili mfululizo,mwaka 1885,1986.
“Na mwaka 1989 baada ya kuona kuwa soka nimeshalitendea haki na kucheza kwa muda mrefu nikaamua kugeukia shughuli za kawaida,anasema Kabisama kisha anaendelea:
Ajira kikwazo timu kubwa.
“Wakati nipo RTC ya Arusha Yanga  na Pan Afrika walinichukua lakini tulishindana kuhusu ajira wao walitaka nicheze mpira peke yake ingawa uwezo wa kunipa ajira walikuwa nao.
“Na kipindi kile kwa kuwa hapakuwa na ajira ya moja kwa moja katika timu tulikuwa tunategemea ajira ambayo timu inakutafutia hivyo mimi sikuwa tayari kujiunga na timu ambayo haikuwa tayari kunipa ajira nikaamua kurudi RTC ya Arusha.
Kutokea kwa kona za Maji Maji.
“ Mwaka 1987 Maji Maji tulienda nchini Zimbabwe kupambana na Power Diynamo katika Roundi ya kwanza ya Club Bingwa Afrika,nakumbuka mechi ile ilikuwa ngumu sana kwetu kwani tulifungwa bao 5-1 na bao letu lilifungwa na Abdullah Chuma.
“Mechi ya marudiano tulitakiwa kwenda Jijini mwanza ili kupambana na wapizani wetu,tulijiandaa vizuri ili kulipiza kisasi cha bao 5,lakini kilichitokea tulipata ajari mbaya sana wakati wa safari nyuma kidogo kabla ya kufika Madaba Toka Songea mjini,eneo ambalo lina kona nyingi sana ambapo kutokana na ajari ile eneo hilo hadi leo linaitwa kona za Maji Maji.
“chanzo cha ajari ile ni kwamba bosi wa basi ambalo tulitakiwa kwenda nalo mwanza alikorofishana na Dereva wake akaamua kuendesha mwenyewe,na kwa kuwa yeye alikuwa mgeni wa Bara Bara ya Songea hakuzifahamu zile kona hivyo baada ya kuzipita kona kadhaa alifikiria zemeisha ,kufumba na kufumbua tukajikuta tupo nje ya Bara Bara.
“Katika ajari ile wote Tulipona ila mimi nilikatika karibia nusu ya ulimi pamoja na maeneo ya miguu nilijisikia maumivu makali sana,lakini mtu ambaye aliumia sana nakumbuka ni Mweshimiwa Joel Bendera mkuu wa mkoa wa morogoro ambaye alikuwa mwalimu wetu lakini mungu alimsaidia baada ya wiki mbili akapata nafuu.
“Tukashindwa kwenda mwanza wenzetu wakapata ushindi wa mezani licha ya sisi tulipata ajari,maamzi yale mimi binafsi yaliniuma sana kwa kuwa nilikuwa na hasira sana na wale jamaa toka Zimbabwe.
Hawezi kusahau
“mwaka 1979 tulicheza mechi ya kirafiki kati ya RTC na Yanga katika mechi ile nilipigwa kichwa cha makusudi hadi kuzimia na mchezaji wa Yanga Hamad Omari akitokea nyuma yangu na baada ya tukio hilo yanga wakamtoa nje na kumwingiza mchezaji mwingine.
“Tatizo ni kwamba tulipishana maneno ya kimpira na mimi milikuwa mwiba mkali kwa timu yake na yeye pia na hadi mwisho wa mchezo tulifungwa bao 1-0,kwa tukio lile siwezi kumsahau kwa kuwa ilikuwa makusudi.
Ushirikina Michezoni.
“Mwaka 1985 kulikuwa na pambano kali kati ya maji maji na Pan Afrika pambano ambalo ilitakiwa lichezwe siku ya Jumamosi lakini pan walichelewa kufika uwanjani kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi na pambano likahailishwa adi siku ya Jumatatu.
“Kipindi hicho Maji Maji alikuwa imemuleta mzee wa kamati ya ufundi Toka Kigoma ambaye alikuwa anahakikisha kamati ya ufundi nje ya uwanja inakwenda sawa.
“Yule Mzee tulimpa jina la Mzee Mziba jina la mchezaji maarufu kutokea kigoma,kwa kweli mimi nilikuwa siamini imani hizo lakini yule mzee nilimweshimu sana,nakumbuka alituambia kuwa kwa kuwa mechi yenu na Pan itachezwa siku ya Jumatatu mtashinda bao 3-0,na hata kama mkipata nafasi nyingine ya kufunga bao haitawezekana.
“kwa kipindi kile Pan Afrika likikuwa Tishio Mimi sikuafiki kama tungeweza kupata ushindi mkubwa kiasi kile lakini sisi tulikuja kuamini mara baada ya kumalizika ule mpambano ambapo tulishinda bao 3-0 kama alivyotuambia yule mzee.
“Mzee Mziba alikuwa akieshimika sana na Maji Maji alikuwa akisafiri na Timu kila ilikoenda kucheza na kila ambacho alikisema ndicho ambacho kilikuwa kinatokea kwa hali ile yule Mzee alipata umaarufu mkubwa sana.
“Hakuishia hapo Maji Maji ilisafiri kwenda dar kukiputa na wekundu wa Msimbazi Simba mwaka 1985 mchezo wa ligi kuu ambapo tuliweka kambi yetu katika chuo cha usafirishaji cha Mabibo Dar,baada ya Chakula cha jioni Mzee Mziba alitutembelea katika kambi yetu na akatukuta tupo katika hali ya uzuni sana akatuuliza kwanini mpo katika hali hiyo?.
“Tukamwambia tunaofu juu ya mchezo wa kesho,Mzee Mziba alicheka sana na kwa maneno ya Dharau hakatuambia mchezo wa kesho ni raisi na msiwe na wasi wasi tutashinda mechi ngumu tayari tumeshacheza,tukaenda kulala.
“Uwezi kuamini Siku ya mechi tulicheza mchezo mzuri Sana kama alivyosema yule mzee Simba walikuwa wakitafuta mpira kwa tochi na hadi dakika 90 za mchezo ulipomalizika Tuliivurumisha Simba bao 2-1,mabao ya Maji Maji yaliwekwa kimiani na Selestine Sikinde pamoja na madaraka Suleman kisha lile ya kufutia machozi la Simba nakumbuka lilifungwa na Zamoyoni Mogela.
“Lakini Mzee Mziba aliendelea kuimalisha ufundi nje ya uwanja ambapo tulikuwa tumebakisha mechi 8 ili ligi imalizike na mechi nyingi zilibaki kanda ya ziwa,Mzee wetu akatuambia msiwe na wasi wasi ila kati ya mechi 8 zilizobakia mtafungwa mechi moja tu ila sijui mechi gani.
“kweli baada ya maneno yale mechi ambayo ilifuata tulipambana na CDA ya Dodomo mechi ambayo tulifungwa bao 1-0,na kuanzia hapo hatukufungwa tena mechi nyingine hadi tukamaliza ligi,hapo nikakumbuka maneno ya yule mzee na kuamini uwezo wake.
                                                                                                       
“Baada ya msimu Kumalizika nakumbuka yule Mzee alituaga na akatuaambia ameitwa uarabuni kwaajiri ya kwenda kutoa tiba,ambapo toka alipoondoka yule mzee hakutokea tena mwingine kama yule,na mimi imani ya kuamini mpira nje ya uwanja ikatoweka.
FC Leopald walitulinganisha na timu ya shule.
“Mwaka 1986 katika michuano ya Club Bingwa Afrika tulipambana na Fc Leopald ya Kenya ambapo wezetu wakenya walitudharau sana adi walidiliki kukifananisha kikosi chetu na timu ya shule na kuhaidi watatufunga zaidi ya bao 6,
“Nakumbua katika mchezo huo nilicheza vizuri sana na baada ya mechi niliandikwa sana na vyombo vya habari vya Kenya kutokana na shughuli ambayo niliwaonyesha siku ile ingawa wakenya walitufunga bao 1-0, na ilikuwa kinyume na matarajio yao.
“Na mchezo wa marudiano mchezo  ambao ulichezwa Mjini Arusha FC leopald walitubamiza tena bao 1-0 na wakafanikiwa kusonga mbele.
Waamuzi
“Ni wavivu sana kubadilika,zamani waamuzi walikuwa wanafanya vizuri licha ya techinologia kuwa chini,lakini siku izi wanaweza kujifunza toka nje kupitia Tv pamoja na mitandao.
Mchezaji anayemhusudu
“Mcheaji ambaye namkubari sana kwa hawa wanaocheza sasa hivi hapa Tanzania na anaitendea haki nafsi ya kiungo ambayo nilikuwa nacheza ni mchezaji tegemeo wa Azam Fc Abul Bakari [Sure Boy] ,Mora amjali zaidi.
Timu ya Maji maji.
“Timu imepoteza mwelekeo kwa asilimia kubwa kutokana na kuyumba kiuchumi pamoja na kukuwa na viongozi wenye mtanzamo chanya tofauti na kipindi kile sisi tunacheza pia wanachama  waepukane na dhana potofu ya kuutegema mkoa kwa ajiri ya kuendisha Timu.
“Nakumbuka mwaka 2010 Maji Maji ilipata mdhaamini lakini aliingia mitini kwa sababu ya matumizi hasi ya pesa zake ndani ya timu,hebu tujaribu kuwa wabunifu na kutafuta mbinu za kuinasua timu na sio kufuja kidogo kinachopatikana.
“Mimi nikiwa kama mjumbe wa Maji Maji baada ya uchaguzi wa hivi Karibuni ningependa kuona Timu yetu inasonga mbele na uongozi mpya ulioko madarakani usirudie makosa yaliyofanyika huko nyuma.
Makocha wa kigeni
“Wanafaa kuleta changamoto kwa makocha wazawa lakini ifikie wakati pia makocha wazawa wawezeshwe kama wa nje pindi wanapopewa nafasi, kama Nigeri walivyoweza kufanya kazi vizuri na Kocha wao Stivin Keshi nasi tuige mfano huo.
Ushauri Binafsi
“Soka la Tanzania linakufa kwa sababu ya kuitanzama Simba na Yanga lazima Tubadilike,Tff na wadhamini wazichukulie timu hizo ni timu za kawaida.
“watu wenye machungu na mpira wajaribu kuzipa udhamini na timu zingine Sio Yanga na Simba Peke yake hatuwezi kusonga mbele.
Baada ya kustaafu
“Kuanzia mwaka 1989 -1994 nikuwa nafanya kazi katika shirika la usagishaji la taifa[national milling],kuanzia hapo nilikuwanafanya shughuli zangu za kawaida ambapo mwaka 2006 nikapata nafasi ya kuajiliwa na kampuni ya kuuza vifaa vya vipodozi pamoja na vyakula [Wadswortny Distributor],na pia ni Mjumbe wa Timu ya Maji Maji pamoja na kocha wa kambalage Veterani.
“Pia nina mke na watoto 6, Mpira umenisaidia Sana kujuana na watu ambayo ni Slaa kubwa katika maisha hata kupata kazi National Milling ni kupitia mpira ingwa soka linalipa sasa ivi kuliko enzi zetu,anaitimisha  John Kabisama mwenye umri wa miaka 58 hadi mwaka 2013, ambaye ni shabiki wa kutupwa kabisa wa Barcelona na Maji Maji ya  Songea,ambapo katika maisha yake hawezi kumsahau Beki  wa Yanga  Elisha John kutokana na alimsumbufu wake uwanjani.
mwisho


Chapisha Maoni