Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.













Na Alex Mapunda, Iringa
Keneth wane.
Keneth wane ni miongoni mwa washambuliaji bora walioibuka kwa kasi kubwa na kufifia kama mshumaa  uliowekwa kwenye upepo mkali,alitingisha soka la hapa nchini na jina lake kung’ara vilivyo akiwa na maji maji ya Songea miaka ya 1994-1997. 
Wane ambaye ni mzaliwa  wa kijiji cha chaburuma Songea vijijini Kipaji chake kilianza kung’aa  toka akiwa shule ya msingi chaburuma na baadae akajiunga na red kids timu ambayo alichezea kwa mafanikio makubwa akiwa katika umri mdogo ambapo kupitia tmu hiyo alipata nafsi ya kuchukuliwa na chaburuma Rangers timu ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja la nne mwaka 1989,timu ambayo hakudumu na baadae akatimukia posta timu  aliyochezea adi mwaka 1993.
Kujituma kwake na kucheza kwa ushirikiano na wezake huku akisifika kwa kuokoa timu  katika mazingira magumu mara kwa mara,iliwavutia Maji maji ambao mwaka 1994 wakamsajili rasmi kama mchezaji wa kutumainiwa ambapo mwaka 1997 aliachana na soka na kuendelea na shughuli zake za kwawaida.
Ubinafsi wa kocha,kupunjwa posho zao ulimfanya achukie mpira.
“niliamua kuachana na Maji maji kwa sababu kuu mbili kwanza kocha Suleman Gwaja alikuwa amekamatwa na baadhi ya wachezaji wakongwe na akaanza kutuchukia wachezaji wengine bila kuweka wazi sababu za kutuchukia, mimi baada ya kuona sipangwi kwa muda mrefu nikaamua kumwaga manyanga.
“Kuna kipindi zaidi ya wachoezaji 8 wa kikosi cha kwanza walikuwa majerui lakini kocha kwa mapenzi yake akaondoka na kikosi dhaifu kwenda mbeya na kanda ya ziwa akiwa na wachezaji pungufu hali ambayo ilinikatisha sana tamaa baada ya kutuacha songea wakati hatukuwa na matatizo.
“Vile vile wakati tuko maji maji tulikuwa tunategemea zaidi posho za uwanjani wakati wa mechi kubwa za Simba na Yanga na mara nyingi tulikuwa tunapewa elfu 20 adi 30 pesa ambayo ilikuwa kubwa sana kwa kipindi kile na ilikuwa ikitusaidia sana,lakini kilichonifanya nikasirike kuna mechi tulicheza na Simba baada ya mchezo huo tulipewa elfu 8 kila mtu huku viongozi wakijilimbikizia pesa nyingi ambazo hawakustahili kwa kweli kutonana na tukio lile mimi niliamua kuachana na maji maji na kuanza kuchukia mpira  kwa kuwa nilijitaidi kuoji kwa uongozi sikupata majibu mazuri.
Mkataba Maji Maji ulinizuia kwenda Simba na Yanga.
“mwaka 1995 Simba na yanga waliniitaji lakini tayari nilikuwa na mkataba na Maji Maji hali ambayo iliweka uzibe wa mimi kujiunga na timu hizo na nikabaki na Wanalizombe kwa kuwa timu hizo zilishindwa kuvunja mkataba wangu.
Tulienda kwa Mganga, tukachezea kichapo cha bao 5-1
“Tukio hili hadi naingia kaburini siwezi kusahau,nakumbuka mwaka 1995 tulienda mwanza kucheza na Pamba ya mwanza viongozi wa Maji Maji wakatupeleka kwa mganga wa toto Afrika ili kutufanyia dawa kwa kuwa toto na pamba walikuwa wapinzani wakubwa.
“Siku hiyo tulichanjiwa dawa na kila mmoja aliogeswa dawa Ndoo mbili na siku hiyo tulipelekwa wachezaji 7,lakini mimi sikufurahishwa na kitendo cha kuchanjwa dawa nikamua kumdanganya mganga ili asinichanje nilichokifanya nikamwita pembeni na kumwambia kuwa wakati nipo mdogo nilipatwa na ugonjwa wa ajabu na wazazi wangu wakanipeleka nchini msumbiji ili kunifanyia dawa ambapo mganga wa msumbiji alinichanjia dawa na akaniambia mtu yeyote arusiwi kunichanjia dawa hadi kitoke kibari toka kwake  baada ya kumweleza hayo mganga akaduwaa! Sana.
“Lakini baadae akaniambia kuwa hata nichanja ila atanipa ilizi ambayo nitaweka kwenye ugoko nikakubariana naye,pia baada ya kuoga dawa mganga alituagiza tukatafute kuku na kumchinja saa saba usiku na damu yake kuchanganywa na maji pia kuoga kitu ambacho tulikitekeleza.
“kilichotokea kila nikikumbuka Napata machungu Maji Maji tulilambwa bao 5-1 wote siku ile tulitoka uwanjani vichwa chini si viongozi wala wachezaji hakuna ambaye alikuwa anaitaji kuongea na mwezaji na hatukupoteza muda tukaingia kwenye Gari na kurudi Songea.
Nawadai Maji Maji elfu 15 ya usajili naomba wanilipe.
“Maji Maji walinisajili kwa Elfu 30,lakini adi leo nawadai elfu 15 pesa ambayo viongozi hawakunipa kwa sababu wanazozijua wao,nawarahumu kwa ukatili huo,kwa kuwa hata wakati tulipokuwa tukisafiri kwenga kucheza nje ya mkoa wa Ruvuma tulikuwa tukipewa pesa kidogo ya kula kama ni ziara ya siku 8 mnaweza mkapewa pesa ya siku 4 au tano ikiisha basi.
“Namkumbuka rafiki yangu Dastan Mkuni alikuwa akila wali maharage badala ya nyama ili kubana matumizi kwa kuwa ugali maarage ulikuwa unauzwa bei raisi, hali hiyo iiwafanya wachezaji wengi wa Maji Maji kucheza chini ya kiwango na timu kufanya vibaya,yote hayo ni uchu wa viongozi wa kudhurumu timu.
Nawachukia wachizaji  wa hapa nchini kwa uvivu wao.
“Nimeacha Kwenda kuangalia mpira uwanja wa taifa kwa kuwa wachezaji ambao wezangu wanawasifia wanacheza vizuri naona wananichefua sana hawafanyi vile vitu vinavyotakwa katika mpira wachezaji wengi wanafanya mazoezi wakati wakiwa na kocha pekee,sio kwamba nawaonea ndio ukweli lazima wabadilike,na ukweli wenyewe soka letu tunaenda kulizika huku tukiona.
Tukio kali.
“Tukio hilo kila nikikumbuka linaniacha  hoi,wakati nipo Maji maji kuna kipindi tulizuiwa katika moja ya gesti mjini Shinyanga mara baada ya mchezo wetu dhidi ya shinyanga Shooting ambapo timu yetu ya Maji Maji ilikosa pesa ya  kuripia gesti baada ya viongonzi kushauriana waliafikiana kiongozi mmoja habaki pale gesti hadi pesa itakapolipwa na tukaondoka kuelekea Moshi kwa ajili ya mchezo mwingine na kilichotokea Yule kiongozi akatumia ujanja na kukimbia pale gesti tukakutana wote moshi.
“lakini haikuishia hapo tukiwa Kilimanjaro tukazuiwa tena katika gesi nyingine ambapo timu ililazimika kumwika poni kiongozi mwingine na kama ilivyokuwa shinyanga nae alifanikiwa kutoroka  na kurudi Songea ambapo hadi leo hii Maji Maji hawajalipa zile pesa.
Soka La sasa na zamani.
“siku hizi wacheaji wengi wanapenda starehe kuliko kufanya mazoezi ya mpira na wanasubiri adi kocha aseme Fanyeni  mazoezi tofauti na enzi zetu sisi ambapo kabla ya mazoezi ya kocha tulikuwa na mazoezi binafsi ambayo yalitufanya tuimalike zaidi ili kukuza soka letu lazima wachezaji wajitambue wanatakiwa kufanya kitu gani.
Goli bora alilowai funga.
“tulicheza na shinynga shooting mwaka sikumbuki mchezo ule ulikuwa mgumu sana kwa Upande wetu Maji Maji kwa kuwa wezetu walitangulia kutikisa wavu wetu dakika za mwanzo ,lakini kucheza kwetu kwa juhudi na maarifa hasa kipindi cha pili ilipelekea timu yetu kufanya mashambulizi ya mara kwa mara langoni kwa wapinzani wetu hali ambalo ilipelekea  kupatikana kona dakika za mwisho  na mimi bila ajizi nikakunjua mguu na kupiga mpira ambao ulienda kwa kasi kubwa na kujaa wavuni pasipo kugusa mtu yeyote huku mlinda mlango wa shinyanga akiwa ana la kufanya.
Atoa somo kwa Malizi.
“namweshimu sana kiongozi mpya wa shirikisho la soka hapa nchini kwa sasa Jamal Emelani Malizi kwa ukomavu wake katika kuongoza mpira,lakini ili aendelee kurinda heshima yake namshauri kuimalisha na kujenga shule za mpira kwa wingi nchi zima ili kupata sura mpya zenge uwezo sahhi wa kucheza mpira na kuachana mfumo wenye haibu wa sasa wa kupeana nafasi za kucheza mpira kwa kujuana  mimi naamni kama hilo litatekelezwa soka letu litapanda chati.
Ushauri kwa Wanalizombe.
“Viongozi wa Maji Maji lazima watambue kuwa mpira wa miguu kwa sasa unaitaji pesa na ushauri toka kwa wachezaji wa zamani wakilitambua hilo Timu itafanya vizuri kinyume na hapo maji maji itachelewa sana kurudi ligi kuu.
Baada ya kustaafu soka.
“Nina mke na mtoto mmoja,pia nashukuru mungu naishi vizuri na familia yangu ingwa soka halikunifanyia chochote lakini kwa sasaa naenelea na shughuli zangu za kawaida,anahitimisha wane ambaye anamkumbuka sana mwalimu wake Rashid Kato ambaye alimweka katika ramani ya soka,anaomba wadau wa soka na wapenda michezo kwa ujumla wamtafute kupitia simu namba 0712628063.
mwisho


Chapisha Maoni