Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Na Sophia Mwaipyana,Mbeya

SAMU MKONO
Miaka ya nyuma  mikoa mingi ilikuwa na timu zilizo kuwa zina shiriki ligi kuu katika mkoa wa kigoma uliyo barikiwa kuwa na mastaa wengi wa muziki  uliwakilishwa na timu ya Mbanga Fc.
Ambayo ilikuwa ikiweka kambi katikati ya mji wa Kigoma paleeee ujiji na walikuwa wakitumia uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika ilikuwa timu iliyo sheheni vijana hodari sana miaka hiyo.
Samu Mkono ni kati ya wachezaji waliyo itumikia timu hiyo  huku akipitia  timu nyingi kutokana na umahiri wake katika soka .
JELAMBA ilikutana na Samu Adamu maarufu kama samu mkono  jina alilo pewa na golikipa  wa Tukuyu Stars   kipindi kile ilipokuwa ikitikisa katika soka Emmanuel Mwasile.
“Nilianza soka toka nikiwa darasa la tano katika shule ya msingi Ikuti  iliyopo mkoani Mbeya na baada ya hapo nikaenda  shule ya sekondari Mbalizi na nikachanguliwa kushiriki katika mashindano ya umisenta yaliyo fanyika Arusha na tukawa washindi watatu  kanda ya nyanda za juu kusini”
“Nakumbuka  wachezaji tuliyoenda nao nipamoja na Fred Mbuna yeye akitokea Iringa  na alikuwa msaada mkubwa sana katika timu yetu ya nyanda za juu kusini kwani nakumbuka alifunga magoli mengi”
“Lakini wakati nipo kidato cha kwanza nilikuwa naichezea timu ya  Mbalizi Rangers kwani mkuu wa shule yetu alikuwa ndiyo meneja wa timu hiyo ,hivyo alinichukua na kunisajiri huko”
“Mwaka 1998 hadi 1999 nikachezea Tazara mwaka 2000-2003 niliichezea Tukuyu Stars  mwaka huo huo nilienda Mbanga Fc  mwaka 2004 nikaenda Zanzibar hadi mwaka 2006 nikatua Tanzania Prisons ambapo nikacheza hapa mpaka 2010”
“Nikiwa Tanzania Prison mwaka 2008 niliitwa katika timu ya Taifa lakini bahati mbaya nilivyo fika kambini Shinyanga  ndiko kocha Maximo alikokuwa ameweka kambi niliumia kifundo cha mguu hivyo nikarudi bila kucheza hata mechi moja”
“Niliumia sana  kuona nimeshindwa kwenda kuitetea Nchi yangu  ila nilikubariana na hali  nikarudi nilipo pona nikaendelea kucheza   katika timu yangu”
Kwanini Tanzania Prisons  imepoteza ubora kama zamani
“Daah  unajuwa kipindi chanyuma wachezaji wengi tulikuwa na uwezo vipaji  ila tulijisahau kuandaa kizazi ambacho kilitakiwa kitupokee sisi pale tutakapo choka nazani hapo ndipo tulipo kosea ndiyo maana sahizi tunashindwa kurudi katika ile hali ya zamani”
Ushirikina katika soka
“Ushirikina upo  nakumbuka  kunasiku tulikuwa tunaenda kucheza Kahama  tulisafiri na waganga watatu katika basi tulivyo fika njiani mganga akasema tushuke kila mtu akachume majani ya mti ndiyo tuendele na safari tulifanya hivyo kasha tukaendelea na safari”
“Tulivyo fika kahama mimi niliumwa kwahiyo sikwenda uwanjani na chumba nilicho kuwa nimelala kilikuwa karibu na Yule mganga akaja kaniambia  hii mechi ni ngumu kwahiyo naenda uwanjani ila inabidi uweunaingia chumbani kwangu uangaliage vitu vyangu”
“Kule chumbani alikuwa ametega vitu vyake na alikuwa amewasha mishumaa hivyo iliisije kunguza vitu kanambia niwe naangalia   nikafanya kama alivyo niagiza  nilienda kama mara mbili nikakuta kilakitu kiko sawa ile naenda mara ya tatu nikakuta ile mitego yake  imelipuka kumbe kule mpira ulikuwa umeisha na tumefungwa goli 3 ile wakati natafakari akawa amerudi akasema nilikuwa nimesha ona kilicho tokea huku”
“Baada ya hapo  tulikuwa tunaenda  kucheza Morogoro  kwahiyo  wale waganga wote waliachwa kule iliwarudi kwani walishindwa kazi natulivyo fika Morogoro   tulitoka sale ya goli 1-1”
Mbanga Fc ilikuwa ni timu ya aina gani
“Ilikuwa timu nzuri kwasababu aliyekuwa anaimiliki alikuwa anatoa huduma vizuri kwa wachezaji hadi viongozi na kambi tulikuwa tukiweka  pale pale  ujiji na uwanja wetu wa nyumbani  ulikuwa ni Like Tanganyika”
Tukio gani  baya kwako katika maisha ya soka
“ Niule mwaka nilipokuwa nachezea Tukuyu Stars  nilikuwa nimekaa mda sana bila kucheza kwasababu nilikuwa nimeumia mguu lakini siku hiyo nikaingia uwanjani ilikucheza na  Afc  baada ya kuairishiwa mechi mara ya kwanza kwasababu golikipa wao alifia uwanjani  kwahiyo walipo kuja mara yapili nikapangwa kucheza”
“Ile nimecheza kidogo nikaurukia mpira narudi chini nikavunjika mguu tena ilikuwa karibu na pale alipo angukia  Yule golikipa wao aliye kufa  kwahiyo niliwaza sana kuwa yawezekana na mimi ningeenda kama mwenzangu”
Kwanini hukudumu Tukuyu Stars
“Nitimu ambayo niliipenda na nilifanya vizuri sana kutokana na mwalimu wangu  West Gwiva  nilikuwa nampenda sana kwani nilikuwa namwelewa sana”
“Ilashida ilikuja pale uwongozi wao ulinibania mimi kwenda kucheza Simba  yani ilikuwa hivi viongozi wa simba waliongea na viongozi wangu kuwa wananiitaji  lakini viongozi waliwaambia kuwa eti mimi bado mdogo na nimewaomba waendelee kunilea kimchezo hadi miaka miwili ipite”
“Kumbe wao hata hawakunihusisha katika hilo swala sasa siku moja nikiwa mapumziko dar –es-salaam nilikuwa uwanja wa taifa naangalia mpira nikakutana na kiongozi wa samba”
“Akaniita kaniambia wewe dogo vipi Simba wanakuhitaji wewe unasema bado mdogo hujui huku kama utalipwa vizuri nilibaki namshangaa kwani zile habari kwangu zilikuwa ngeni “
“Kwahiyo ndiyo akanieleza kuwa tuliongea na viongozi wako kuwa tukusajiri huku  wakasema eti umesema undelee kuwa pale hadi miaka miwili  ili waendele kukulea kwani bado mdogo toka hapa sikutaka tena kurudi Tukuyu nikaenda zangu Mbanga Fc kigoma kwani walikuwa wananiitaji”
Ilikuwaje siku ya kwanza kucheza na timu kubwa
“Msema kweli mpenzi wa mungu kiukweli mwalimu wangu  aliniandaa sana kisaikolojia na kweli mechi yangu ya kwanza kucheza na timu kubwa ilikuwa ni Simba na Tukuyu Stars mwalimu alijuwa kama nitacheza katika kikosi chakwanza  hivyo alitumia mda mwingi kunijenga “
“Najioni ilopo fika mwalimu aliniita nakuniambia mechi ya kesho nimechi ya kawaida sana  kwahiyo ichukulie kama mechi nyingine lakini nahisi bila mwalimu wangu  West Gwiva ningelala na hofu kubwa  ila kwa ajili alivyo nijenga wala sikuogopa na nilicheza kwa kujiamini sana”
Kwanini uliachana na mikikimiki ya soka ukiwa bado unanguvu
“Nikweli   kilicho fanya niachane na soka mapema ni mguu kwani hadi leo unanisumbua kwahiyo toka nivyo umiaga mguu ukawa kikwazo kikubwa kwangu kwani kila mara ulikuwa unanisumbua  nikaona bora nipumzike”
Mafanikio uliyo yapata kupitia soka
“Heshima kazi mdogo wangu  leo hii mimi niko kazini kutokana na mpira kwahiyo mafanikio niliyonayo kwasasa chanzo chake ni mpira ,pia kutembea sehemu mbalimbali na kufahamika”
Ilikuwaje hadi ukaitwa Samu mkono
“Nakumbuka hili jina lilizaliwa nikiwa nachezea Tukuyu Stars kunagolikipa mmoja alikuwa anaitwa  Emmanuel Mwasile  aliniita hivyo kutokana na nilivyo kuwa namlinda akiwa golini kwahiyo alikuwa ananiambia jamaa unanilinda kama mkono vile  kwani mkono  tunatumia kufanyia kujikingia nakila kitu”
“Kwahiyo toka hapa nikawa naitwa Samu Mkono  ukija hata hapa kazini ukisema Samu Adamu utaambiwa hatumfahamu ila ukisema Samu Mkono hata mtoto anakuleta nyumbani”
Ushauri wako
“Wachezaji wajitahidi kufuata maelekezo ya mwalimu iliwaweze kuwa wachezaji wazuri wacheze mpira wa kimataifa  kama Sammata”
Maisha yako ya sasa
“Kwasasa mimi ni askari magereza na ninaendelea na shughuli zangu ndogondogo “

“   Ninamke na watoto watatu   nawapenda sana  kwani mke wangu mama Norin alikuwa akinipa sapoti sana kipindi nilipokuwa nacheza mpira ingawaje enzi hizo ndiyo tulikuwa bado tuko katika uchumba lakini yeye alikuwa ndiye mshauri wangu wakwanza  na kunifariji pale ninapokuwa katika matatizo”
MWISHO


Chapisha Maoni