Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.







AUGUSTINE LUHOLE.

MIONGONI mwa wachezaji wazuri katika safu ya ulizi ambao walipata kuwaika hapa nchini miaka ya 1980 hadi 96 ni  pamoja na Augustine Lihole ambaye alicheza kwa kiwango cha hali ya juu akiwa na Tumbaku ya morogoro,mseto ya morogoro pamoja na Lipuli ya Iringa Timu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa katika historia yake ya kusakata kandanda.
Luhole mzaliwa wa mkoani mara Wilaya ya Talime, alianza kuburuza gozi la ng’ombe toka akiwa shule za msingi ikiwemo Shule ya kawe dar,shule ya uhuru Arusha[jakalanda] pamoja na shule ya  mchikichini Morogoro lakini kiwango chake kilikuwa zaidi akiwa na umri wa miaka 16 katika sekondari ya Forest hill na alicheza katika michuano ya Umiseta kanda ya mashariki kipindi hicho timu za mtaani zilianza kumgombania kama mpira wa kona.
Lakini katika maojiano maalumu na Gazeti la championi anafafanua yafuatayo kuhusu maisha yake ya mpira:-
“nilianza kucheza mpira kwa kiwango kikubwa nikiwa na Timu ya Tumbaku ya Moro tarehe 26 mwenzi wa nne 1976, timu ambayo nilijiunga nayo lengo kubwa likiwa ni kupata kazi suala ambalo nilifanikwa na nilikuwa nilikuwa nikilipwa  elfu moja na mia nane,ambapo kipindi kile kupata kazi ilikuwa ngumu sana,timu hiyo niliichezea kwa kiwango kikubwa sana  ambapo mwa 1986/88 nikajiunga na timu ya mseto ya morogoro baada ya kutokea lidandasi katika timu ya tumbaku na baadhi ya wachezaji wakaachishwa kazi nikiwemo mimi.
“sikudumu na Timu hiyo nikajiunga na lipuli ya Iringa 1988 mwenzi wa 12 baada ya kiongozi wa lipuli Laurence kunifuata morogoro ili kunisajiri pamoja na mwenzangu Venansi moshi na kipindi hicho lipuli ilikuwa ikitafuta wachezaji wenye sifa  ili kuipandisha timu hiyo ligi kuu.
“nakumbuka tulipigana sana ili kuhakikisha Lipuli inapanda Daraja na baadae timu ikacheza vizuri hadi ikapanda daraja na ikacheza ligi kuu,nakikumbuka Kikosi bora cha lipuli  ambacho kilikuwa tishio cha mwaka 1990/92 baadhi ya wakali ambao walikuwepo ni pamoja na Kipa Ivo ng’itu,Kongo Mruge,Gula Mathias,cristopher Kienes,Ezekiel Mpande[marehemu]pamoja na Heri ngunja [marehemu]
“wengine ni Chachage Bokaza,Ikupirika nkoba,Shabani musa,Julias ngawambala,mchele mchele,Felix Jogoo chama,Agostino Luhole,Mohamed keto pamoja na Athumani Kilambo,makocha wa timu hiyo alikuwepo pasco Bela pamoja na Phiri kocha Toka Zambia.
Baada ya kuitumikia Lipuli kwa moyo mmoja baadae alichaguliwa na timu kwenda Zanzibar ili kusomea mafunzo ya ukocha baada ya kufaulu akarudi kuja kuifundisha lipuli ambapo kufikia mwaka 1996 aliondoka Iringa na kuelekea pwani ili kumtibu mtoto wake alikuwa mgonjwa,akiwa huko alifundisha timu ya kisalawe sports club na akaifikisha hadi ligi daraja la pili na kufikia 2003 akarudi mara ambako alifundisha timu ya Msoma  JK football klabu timu ambayo ilikuwa ikishiriki ligi ya mabingwa ambapo mwaka 2008 akachuliwa na polisi mara ambapo walitolewa kanda na timu toka kigoma na baadae akajiunga na timu ya Polisi Tarime Timu ambayo anafundisha hadi hivi sasa.
Tulinusurika kufa mikumi
“nakumbuka nikiwa Lipuli tulitoka kucheza mpira Dar,tulipofika mikumi eneo la Iyozi Dereva alipaki gari vibaya, mwenyewe akaenda kununua mkaa baada ya muda mfupi kuna gari kubwa lilitokea gafla mbele yetu ilikatugonga na kutuburuza kwa umbali wa mita 25 na mimi nilikuwa nimekaa mbele ya gari hilo nashukuru mungu Tulitoka Salama.
Waamuzi wanaua mpira wetu
“wakati nipo lipuli Tulienda kucheza na yanga jijini Dar katika mchezo ambao ulikuwa mgumu sana katika mechi hiyo mwamuzi alitoa maamzi ya ajabu sana,nakumbuka mpira ulikuwa umetoka nje baadae ukanaswa na mchezaji wa yanga na akamimina crosi na kutufunga bao mwamuzi akaita kati,wakati hata watoto wadogo waliona kuwa mpira ulitoka nje ya uwanja,katika mechi hiyo yanga waibuka na ushindi wa bao 1-0.
“pia wakati tulipopigania lipuli kupanda daraja Tulienda Tabora kucheza na milambo na kipindi hicho milambo ilikuwa timu tishio kwa kuwa ilikuwa ikibebwa sana na mkuu wa mkoa wa kipindi hicho mzee gama alisimama kidete ili kuhakikicha timu hiyo inapanda daraja,tulianza kwa kuwafunga bao moja baadae mwamuzi akatoa penalti ya uongo na milambo wakasawazisha  ambapo kwa msimu huo milambao na lipuli zote zikapanda daraja.
Ushirikina
“nakumbuka nikiwa na Tumbaku ya moro tulicheza na pan Africa sisi tulikuwa na mzee wetu wa kamati ya ufundi,siku ya mechi aliingia chumbani ili kuhakikisha  anaweka vizuri dawa kwa ajili ya mechi kitu ambacho kilitokea ni kwamba tulichezea kichapo cha bao 4-0.
“wakati wa kubadilisha nguo yule mzee akatoka chumbani na kutuambia kuwa wakati wa mpira umefika twendeni uwanjani tukamwambi tumecheza alishangaa sana kumbe kilichotokea mzee wa kamati ya ufundi wa pan Afrika alimpiga dawa ya usingizi ili kufanikisha malengo yao ya kutufunga.
Zamani&sasa
“wachezaji wavivu pia wanapenda starehe mpira sio maigizo kama tunataka kufanya vizuri na timu ya taifa.
Anaempenda
“Elius maguri mchezaji wa simba ambaye amesajiliwa na simba ni mchezaji mwenye kipaji na atafika mbali.
Stasahau.
“tulienda shinyanga kucheza na RTC shinyanga nikiwa na Lipuli ya Iringa tukiwa kule mashabiki walifanyia fujo baadae tukahaidi kulipa kisasi kwetu pia, hata mashabiki wetu baada ya kupata taarifa walikasirika sana,kweli walipofika mashabiki wa iringa wakaripa kisasi kwa huwafanyia fujo ambapo RTC Shinganga  walisindikizwa na helkopta ya polisi hadi Ilula nje kidogo ya mji wa Iringa.
Ushauri kwa stars&Lipuli
“Timu ya Taifa ijegwe kwa muda mrefu na pawepo na shule za michezo za kueleweka ili kuwakuza wachezaji wetu tofauti na ilivyo hivi sasa haieleki wachezaji wanatoka wapi.
“timu ya lipuli ni timu ya wanairinga wote kila mmoja akumbuke  kuwa  mchango wake ni muhimu kwa Lipuli,pia nawaomba viongozi wa lipuli kuandaa mechi ya maveterani waliocheza timu hiyo kwa lengo la kuwakutanisha wachezaji wazamani wa lipuli na wachezaji wa sasa pia kutoa hamasa kwa wadau kuchangia timu hiyo.
Baada ya kustaafu soka.
“umri wangu ni miaka 55 nina mke na watoto 5,sasa ivi ni kocha pia nafanya biashara ndogo ndogo ili kujikimu kumaisha”,anahitimisha luhole.


Chapisha Maoni