Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Na  Alex Mapunda
……………………………………………………………………………………..
Mbwana Makata.
MBWANA makata ni miongoni mwa mlinda mlango bora ambaye alifanikiwa kutikisa soka la Tanzania miaka ya 1985-92 hapa nchini akiwa na club ya Tukuyu stars na Yanga ya jijini Dar es salam.
Makata ambaye ni mtoto wa kwanza katika familia yenye watoto 7,alizaliwa katika kijiji cha makolora mkoani Tanga,wiki hii amekutana na MWANDISHI WETU na kifanya maojiano maalum, kuhusu maisha yake ya soka.
“Nilianza kucheza mpira tangu nilipokuwa shule ya msingi Makolola,Mkoania Tanga,na nilipata nafasi ya kushirika mashindano mbali mbali licha ya umri wangu kuwa mdogo,lakini nilianza kucheza soka la ushindani mwaka 1981 nikiwa na Reli ya Iringa hapo ndipo kipaji changu kilipoanza kuvuma kwa kuwa nilidumu nao kwa kipindi cha miaka 3  na 1984 uongozi wa timu ya waziri mkuu ya dodoma wakanisajili na nilicheza katika kikosi chao nikiwa kama golikipa namba 1,na tukafanikisha kuifikisha mbali timu hiyo.
“Kutokana na uwezo wangu wa kujituma na kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu pindi niwapo langoni,mwaka 86,nikanyemelewa na Tukuyu Stars ya Mbeya,timu ambayo niliichezea kwa mafanikio makubwa sana kwa kuwa kupitia tukuyu stars uwezo wangu wa kucheza soka ulijulikana hadi nje ya mipaka ya Tanzania kutokana na tukuyu stars ilipata nafasi ya kushirki michuano ya kimataifa yeye akiwa kama golikipa namba 1,mara baada ya timu hiyo kufanikiwa kulitikisa soka la Tanzania kwa kutwa ubingwa mwaka 1986.
“Hata hivyo nafasi yangu ya kubaki tukuyu stars ilififia kwa kasi sana kutokana na timu ya soka ya Yang Africans toka jijini Dar es salam kunisaka kwa udi na uvumba licha ya kwamba timu hiyo ilikuwa na magolikipa mahili sana hapa nchini ikilinganishwa na timu zingine na mnamo mwaka 1988 nikajiunga rasmi na Yanga.
“Nikiwa Yanga nilipata upizani mkubwa sana toka kwa Joseph Fungu na Juma Pondamali ambao kwa hakika walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kulinda lango lakini nilicheza kwa kujiamini huku nikifanya mazoezi mara kwa mara na mwisho wa siku tukawa tunapokezana Kucheza katika mechi mbali mbali za ndani na Kimataifa.
Kuondoka Yanga
“Kipindi kile club zilikuwa hazitulipi mshahara tulikuwa tunapata posho,ila zilikuwa zinamtafutia ajira mchezaji,mimi nilitafutiwa ajira City council,kakini kuna lidandasi lilitokea mwaka 1992,hali ambayo ilipelekea kupunguza wafanyakazi na moja ya watu ambao walikumbwa na zahama hiyo ni Sisi wachezaji ambao tulikuwa tunafanya kazi katika eneo lile kiukweli baada ya tukio lile maisha yangu ya soka yalikuwa magumu sana ndani ya yanga.
“Na hasa hukizingatia tukio lile lilikuwa limetokea muda mfupi mara baada ya kurejea toka kwenye maumivu mazito ya enka,ambayo yalinifanya nisipate nafasi ya kucheza mara kwa mara, nilikuwa nikitegemea posho ambayo ilikuwa haikidhi maitaji yangu,na kipindi kile tulikuwa tunapata posho kubwa katika mechi za Simba na Yanga ambapo tulikuwa tunachukua elfu 19 adi 20,lakini kwa mechi za kawaida tulikuwa tunachukua elfu 3 au 4.
“Sikufanya ajizi kwa usalam wa maisha yangu mwaka 1992 nikajiunga na Rtc Kagera timu ambayo ilinihaidi kunipa ajira ya kudumu,hata hivyo mambo yalienda kombo mnamo mwaka 1993 nikaamua kutundika Daruga na ukawa mwisho wa maisha yangu ya kucheza soka.
Baada ya kutundika daruga
“Mwaka 1993-1998,niambua kuachana kabisa na mambo yanayohusu soka nikaamua kujikita katika biashara ili kujijenga kiuchumi,nilikuwa nikisafirisha bidhaa kama vile vipodozi,viatu, sukari na vitu vingine vingi katika maeneo mbali mbali,na nilifanikiwa kuiingizia kipato kikubwa na nikawa naishishi vizuri na familia yangu,lakini mwaka 1998 baadhi ya viongozi na wadau mahili wa soka wakanishauri kujiunga na mafunzo ya ukocha kutokana na mchango mkubwa ambao niliutoa kwa taifa pindi nilipokuwa mchezaji.
“Nililidhia kwa moyo mmoja na  nilifanikiwa kupata mafunzo ya ukocha ambapo timu yangu ya kwanza kufundisha ilikuwa ni Mji Mwapwa ya Dodoma ambayo niliipandisha hadi ligi kuu bara na nikadumu nayo kwa misimu 3 na mwaka 2000 nikajiunga na timu ya Idd Azan mweshimiwa mbunge ambayo nilidumu nayo kwa kipindi cha miaka 4,na timu hiyo ikauzwa na ikafahamika kwa jina la Pan Afrika,na mwaka 2004 nikaamu kuondoka kwa kuwa timu hiyo ilikuwa imeshapata kocha mwingine.
“Safari yangu ya ukocha ilizidi kuwa ndefu na mwaka 2004  nilipata nafasi ya ukatibu mkuu wa kamati ya ufundi ndani ya chama cha soka cha kinodoni,ambapo nikiwa hapo nilifundisha timu ya Copa coca cola ya kinondoni chini ya umri wa miaka 17,na nikafanikiwa kuchukua ubingwa wa michuano hiyo.
“Kikosi changu cha chini ya umri wa miaka 17 cha kinondoni kimetoa wachezaji wengi sana wenye uwezo wa kusakata kabumbu hapa nchini kwa sasa akiwemo chiritoph Edwald[simba] na Tino Agostino [prisons] ambao wanafavya vyema kwa sasa katika soka la Tanzania,
“Lakini pia mwaka 2008,nilipata nafasi ya kuwa kucha wa mkoa wa kisoka wa Kinondoni katika michuano ya Taifa Cup,ambapo sisi kidondoni tulifanya vizuri sana katika michuano ile na tulikuja kutolewa na wezetu wa Ilala timu ambayo ilikuwa na wachezaji wengi wa ligi kuu akiwemo Musa Hasani Mgosi na Mohamed kijuso,chini ya kocha mwezangu Jamhuri kiweru na wakatawazwa mabingwa.
“Sikuishia hapo baada ya michuano ya Taifa cup kumalizika nilijiunga na wanakishamapanda Toto Afrika ya Mwanza ambayo niliifundisha kwa mafanikio makubwa ikilinganishwa na mwenendo wa timu hiyo kwa misimu mingine lakini mimi niliifikisha nafasi ya Tano ya ligi kuu ya vodacom Tanzania,lakini nikiwa bado niko Mwanza nilipata nafasi ya kuifundisha timu ya mkoa wa mwanza mwaka 2009,tukafanikiwa kushika nafasi ya Tatu,na hapo nikaondoka Mwanza nikajiunga Tanzania prisons ya Mbeya.
“Prisons nilifundisha kwa kipindi cha msimu mmoja na baadae nikaachana nao na nikapata nafasi ya kuchukua kombe la Taifa cup nikiwa na timu ya mkoa wa Mbeya,Mbeya Irozi mwaka 2011 hapo ndipo Nikachukua jukumu la kuonpdoka mbeya na kujiunga na Jkt Oljoro toka mjini Arusha,timu ambayo naifundisha hadi hivi sasa na nimemaliza nayo ikiwa katika nafsi zuri, ligi kuu Vodacom Tanzania bara         katika msimu wa ligi uliomalizika hivi karibuni kwa Timu ya Yanga kunyakua ubingwa wa ligi hiyo.
Ushirikina michezoni
“Kwa kipindi kile nacheza suala la ushirikina lilikuwa likichukua nafasi kubwa kwa vilabu vikuwa na timu zingine kuliko sasa,ingawa imani hizo hazina msaada wowote katika soka kwa kuwa mpira ni mazoezi,kipaji,kumsikiliza mwalimu, mbinu pamoja na pesa.
“Nakumbuka mwaka 1988 nikiwa na Yanga siku chache kabla ya  mchezo wetu wa mwisho na Costal Union ya Tanga walikuja waganga wapatao 10,Toka mikoa Tofauti kwa ajiri ya kutufanyia dawa ili kupata ushindi katika mechi yetu na wachezaji wote tulilazimishwa kushiriki tukio lile kuanzia saa 3 usiku hadi saa 8 usiku lakini licha ya kutumia dawa zile Tulikung’utwa bao 1-0,na Wagosi wa kaya wakatangazwa kuwa mabingwa wa Tanzania kwa mara ya kwanza na sisi tukamabulia nafasi ya pili.
“Kikosi cha yanga ambacho kilikosa ubingwa mara baada ya kutumia Kikombe toka kwa wataalam wa miti shamba ni kama ifuatavyo Golini nilikuwepo mimi mwenyewe,2 Lawrenc MwaluSako,3 Fred Felix,4 Godwin Aswile,5 Said mwamba6,6 Issa Athuman,7 Abuu Bakari,8 Athuman China,9 Abeid Mziba,10 Edga Fungo na 11 ni Celestin Sikinde ambao walipelekwa puta na Costal Union mwaka 1988.
Hatasahau
Siwezi kusahu nilipoumia Enka nikiwa na Yanga mwaka 1989,kati yetu na Reli Moro,ambapo nilitolewa nje dakika ya 20 ya mchezo mara baada ya kuumizwa vibaya na Dankan Butinini,na nafasi yangu ikachuliwa na  mlinda mlando mwezangu Sahau Kambi ambaye naye aliumia kabla ya mchezo kumalizika na nafsi ikachuliwa na Joseph Fungo ambaye aliimili adi Dakiki 90 ya mchezo.
“Hiyo katika mchezo ule Yanga walitumia magolikipa watatu kutokana na sisi kuumia,tukio lile liliniweka nje ya uwanja kwa kipindi kirefu hadi likatishia uwezo wangu wa kucheza mpira ndani ya Yanga lakini baadae nikapona Vizuri na kulejea uwanjani.
Kumbukumbu
“Naikumbuka sana mechi yangu ya kwanza ya kimataifa nikiwa na Tukuyu Stars katika kombe la Afrika mashariki na kati  dhidi Sports Club Vila ya Uganda [nakivugo stadium],mwaka 1987,mechi ambayo tulitundikwa bao 4-2 kwa kweli ilikuwa mechi ngumu sasa kwetu na mimi Nilikuwa mechi yangu ya kwanza kuchieza nje ya Tanzania.
“kutokana na ugeni wa mashindano Tukatolewa katika hatua ya makundi na kurudi nyumbani kwa kuwa katika mashindano hayo tulifanikiwa kushinda mechi moja pekee zidii ya timu toka Somalia.
Tofauti TFF-FAT.
“Kwa sasa Tff imejitaidi kututoa Toka kwenye soka la ubabaishaji na kutuleta kwenye soka la kisasa kwa kuwa Shirikisho hilo lina kamati mbali mali za kutatua migogoro michezoni Tofauti na FAT ambayo maamuzi yalikuwa yakichuliwa na watu wachache.
“Kipindi kile wachezaji walikuwa wanajituma sana ndio maama tulikuwa tunafanya vizuri lakini kwa sasa uongozi unajitaidi ila Tatizo wachezaji kutokujitoa kwa moyo.
“Na pia ili kukuza na kulifikisha mbali Soka letu TTF inatakiwa itumie nguvu katka kuhakikisha vilabu vyetu vianaachana na kumilikiwa na wanachama na badala yake ziendeshwe kwa mfumo wa Kampuni.
Wachezaji wa kigeni
“Wana umuhimu mkubwa sana kwa kuwa wanaleta changamoto kwa wachezaji wa ndani,lakini timu zetu zijitaidi kusajili wachezaji wenye uwezo sio kupoteza pesa kuokota wachezaji wasio na tija ambao tunaweza kuwapata hapa hapa nchini.
“Nawakubari sana  Kipre Tchetche na Aruna Niyozima,kwa uwezo wao wa kisoka wanajitaidi sana kucheza kama watanzania wanavyotaka kwa viwango vya wachezaji wa nje.
Wachezaji Anaowakubari
“wachezaji wengi ni wazuri lakini wafuatao ni zaidi nikiwatenga katika makundi 4,kwa upande wa mlinda mlando Juma  K Juma[Simba] anafunika,beki Kelvin Yondani[Yanga],kiungo Amri Kiemba [Simba]ni mchezaji wa hali ya juu sasa kwa sasa hapa nchini akifuatiwa na Abuubakari[Sure Boy] wa Azam FC  lakini poul Nonga[Jkt Oljoro]anacheza vizuri sana katika safu ya ushambuliaji. 
Dawa ya Soka la Tanzania
“Ili timu zetu zifanye vizuri ndani na nje ya Tanzania lazima pawepo na udhamini wa kueleweka kwa kuwa pesa ni Tatizo kwa timu zetu, walao timu ya kwanza adi ya 9 ziwe na udhamini wa kudumu.
“Pia lazima wachezaji wakae kammbini muda mrefu na makocha wapewe muda wa kutoisha wa kukaa na wachezaji ili kujenga timu kwa muda mrefu.
Maisha baada ya soka
“Sasa ivi nimeoa na nina watoto watatu,japokuwa soka halikunifaidisha kiuchumi zaidi ya kupata sifa na kufahamiana na watu wengi lakini kazi yangu ya ukocha inanisaidia kuendesha maisha yangu na naishi vizuri.
“Kwa sasa sijishughulishi na kazi yeyote zaidi ya ukocha kwa kuwa Kazi hiyo ni ngumu na ukijiusisha na mambo mengi sni ngumu sana kufanya Vizuri,anaeleza Mbwana Makata ambaye alikuwa anasumbuliwa vilivyo na Abeid Mzimba wakati alipokuwa mchezaji katika nafasi yake ya ugolikipa.
mwisho


Chapisha Maoni