Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





ALEX MAPUNDA MWANDISHI
 
Mbui Yondani.
 Mbui Yondani ni miongoni mwa washambuliaji wapiga mashuti hatari sana ambao waliwahi tokea hapa nchini na kamwe hawezi kusahaurika kwa mshabiri na wadau wa soka hapa nchini hasa kwa Timu ambayo zamani ilikuwa kiboko ya vigogo hapa nchini nazunguzia  Reli Morogoro .
Yondani ambaye ni mzaliwa wa mtaa wa Kirumba Polisi Jijini Mwanza ambaye ni Baba yake mdogo wa Beki  mahili wa Yanga Kelvin Yondani, alianza kusakata kabumbu wakati akiwa mdogo katika shule ya Msingi mwenge iliyopo Jijini Humo.
Katika Mazungumzo maalum na Gazeti hili ameeleza kwa kina kuhusu historia yake ya soka;
 “Licha ya kucheza mpira katika timu ya Uwanja CCM Kirumba pamoja na Basuko,nilianza kucheza soka la ushindani mwaka 1988 katika timu ya Coop United ambayo ni timu ya watoto wa mjini hapa Mwanza timu ambayo wamepitia wanasoka wengi wa mkoani Mwanza.
“Mwaka 1989 nilijiunga na Reli ya Morogoro timu ambayo ilikuwa tishio kwa vigogo hapa nchini nazungumzia Simba na Yanga,wakati nipo Reli nilipata nafasi ya kuchezea timu ya Taifa kwa mara ya kwanza mwaka 1992 kutokana na kiwango changu kuwa juu sana kwa kipindi hicho,nakumbuka tulicheza kwenye michuano ya Challenge  ambapo Tanzania tuliwakilishwa na Kaka Kuona pamoja na Victoria,Hayo ni majina ya timu ya Taifa Sisi tuliwakilishwa na timu mbili kwa kuwa tulikuwa waandaaji .
“Baada ya kupata nafasi ya kuitumikia Timu ya Taifa mwaka 1993 nikasajiliwa na Simba  ya Jijini Dar Es Salam,Timu ambayo niliichezea kwa msimu mmoja lakini kutokana  na mizengwe,kocha alikuwa anawapanga wanchezaji kulingana na mapenzi yake hata kama wewe ni mzuri,Na ni ukweli usiopingika kipindi kile  nilikuwa mchezaji wa kiwango cha juu sana,
“Baada ya kuona kwamba Simba naweza nikaua kiwango changu  mwaka 1994 nikatimukia Milambo ya Tabora,lakini kutokana na maisha magumu ya huko Tabora,Timu yangu ya Zamani Reli ya Morogoro wakaamua kunirudisha, hapo nilicheza kwa miaka miwili 1996 hadi 1998.
“Mwaka 1998 hapo nilifikia juu ya kustaafu soka  na kuangaika kuhusu  maisha yangu kwa kuwa kwa kipindi chote hicho sikuwa vizuri kiuchumi, nikaacha kucheza Soka la ushindani nikachezea Mwanza Veterani Pamoja na Pamba ya mwanza ambapo Mwaka 2002 nikaacha kabisa kujihusisha na Mambo ya soka hapo ndipo nikatundika Daruga Rasmi.
Nakumbuka.
“mwaka 1990 wakati nipo Reli ya Morogoro tulicheza na Timu ya soka ya Maji Maji ya Songea,katika pambano hilo ambalo lilikuwa kali sana kutokana na Maji Maji kuwa na kikosi imara hadi kipindi cha kwanza kilipomalizika nakumbuka tulifungana bao 1-1,
“Kipindi cha pili mchezo ulianza kwa kasi sana ambapo dakika za mwisho nilipokea Pasi safi nje ya 18 na bila kufanya ajizi nilifumua Shuti kali ambalo lilipeleke mlinda mlango wa Maji Maji kuchanika mikono na kuachia mpira ukaingia Wavuni.
“Mimi mwenyewe nilishangaa sana tukio lile mara baada ya kumkuta bwana Shaib Kambanga Disko usiku baada ya mechi akiwa amefungwa bendeji,nikampa pole na akanieleza kuwa hakuwai pata mkwaju kama ule,tukaendelea kuburudika.
“Nakikumbuka kikosi cha Reli ambacho kilikuwa kiboko ya Vigogo na Timu zingine hapa nchini,ambacho akitakuja sahaurika hapa nchini ambapo langoni alikuwepo Athumani Msumari,safu ya ulinzi iliimalishwa na  James Charles[marehemu],Abdallah  Mkali[marehemu],Gasper Lupindo[marehemu] pamoja na Fikiri Magoso. Viungo alikuwepo Mtwah Kiwelu,Boniface Njohore pamoja na Dankani Butinini huku safu ya ushambuliaji ikiongozwa na mimi mwenyewe  Mbui Yondani,Msafiri Khamis Bila kumsahau Living Stone.
Hawaezi kusahau
“Mwaka 1991 mechi ya ligi kuu kati ya Reli na Bandari ya Mtwara mimi na beki wa Bandari tuliruka juu kuuania mpira mara baada ya kuingizwa majaro zuri toka winga ya kulia bahati mbaya tukaukosa mpira na tukagongana Vichwa na tukadondoka vibaya sana.
“Katika tukio lile mwenzangu alipata fahamu baada ya siku ya Tatu,mimi japokuwa nilirudi uwanjani kuendelea na mchezo usiku uliofuata sikupata usingizi nilipata maumivu ambayo sikuwai kuyapta tangu nilipozaliwa kwa Baba na Mama, ambapo baada ya siku chache niliendelea na mchezo.
Ushirikina
“Upo hasa kwa virabu vikubwa Simba na Yanga mara nyingi hasa katika mechi za watani wa jadi lakini kwa timu zingine kama Reli sikushuhudia suala lolote la ushirikina tulikuwa tunafanya mazoezi na kumtegemea mungu.
“Siamini hata kido imani hizo sio kweli ,wakati nipo  Simba kuna mambo mengi yalikuwa yanafanyika wakati wa mchezo lakini tulikuwa tukichezea kichapo kama kawaida.
Simba walinibebesha Gunia la Misumari.
“Mwaka 1993 wakati nikiwa Simba,nilikosa bao la wazi wakati zikiwa zimesalia dakika 3 mpira kumalizika,katika kombe la Caf kwa sasa shirikisho,kati ya Simba na Timu Toka Msumbiji,nakumbuka ilikuwa CCM Kirumba Mwanza mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana.
“Baada ya mechi ile sikuwa na amani,wenye timu walinitazana kwa jicho baya  huku wakinituhumu kuwa mimi ni mpenzi wa Yanga na kwamakusudi nikaamua kuwakosesha Simba ushindi kiukweli iliniuma sana.
“Basi kutokana na tuuma ile na licha ya kwamba kiwango changu kilikuwa kikubwa masikini ya mungu sikupewa nafasi hata ya kusafiri na timu kwenda nchini Msumbiji katika mechi ya marudiano waliniacha Bongo.
“Kuanzi hapo nilichukiwa sana hadi nikahasirika kisaikorojia  lakini ukweli ni kwamba mimi sikuwa na mapenzi na Yanga na kukosa Bao ni suala la kawaidi kwa mchezaji sio makusudi.
Waamzi.
“Viwango vyao vipo chini sana hawjiamini pindi wawapo uwanjani kutokana na  kupokea Takrima toka pande mbili hali hiyo inapelekea wachezaji kuchezeana rafu mbaya na mwamzi anajifanya haoni.
“Mfano kuna tukio lilitokea Hivi karibuni la Haruna Moshi Boban kumchezea Rafu mbaya Kelvin Yondani [Yanga]mwamzi badala ya kutoa kadi nyekundu akatoa kadi ya njano huu ni uzembe mkubwa kwa waamzi wetu lazima wabadilike.
Katiba.
“TFF lazima wafanyie mabadiliko ya katiba ya soka hapa nchini hasa kipengere cha uchaguzi badala ya wanachama wachache kumchagua kiongozi wa chama wa ngazi ya chini au ya juu badala yake achaguliwe na umaa, ili kuepuka tatizo la watu wachache wenye pesa wasiojua mpira kuchukua madaraka kwa kuwaonga wapiga kura.
“Kuna kipindi nilijisikia aibu sana wakati nilipoenguliwa mwaka 2005 katika nafasi ya ujumbe Ilemela na wakampa mtu kutokana na vijiela vyake ambaye hajue chochote kuhusu mpira kunishinda mimi.
Wachezaji anaowakubali
“Namkubali sana Haruna Niyonzima kiungo wa Dar Es Salam Yang Afrika yupo Vizuri kwa ukanda huu wa afrika mashariki na kati, lakini sio kwamba napendelea ni ukweli wenyewe Mtoto wa kaka yangu Kelvini Yondan Anafanya vizuri katika nafasi ya Ulinzi kwa hivi sasa hapa nchini.
Kipa Msumbufu.
“Mwameja huyu ni balaa mimi nadiriki kusema kuwa hakuna mlinda mlango ambaye hadi hii leo amefikia uwezo wa Mwameja.
“Mimi alikuwa akinisumbua sana hakiri,mara nyingi mazoezini alikuwa anawaita na kuwawekea mpira eneo la penalti na kuwaambia atakayefunga penalti tano nampa fedha,lakini matokeo yake unaishia tatu au mbili,mimi sikuwai shuhudia Mwameja akifungwa Penalti 5.
Ushauri kwa Timu ya Taifa.
“Hata ashuke Yesu, kwa mfumo wanaoutumia Taifa Stars na haina ya wachezaji walionao kushiriki kombe la dunia ni ndoto,lazima yafanyike mabadiliko makubwa sana ili kunusuru soka letu.
“Mimi kipindi nacheza nilikuwa na nguvu sana hizo nguvu za Thomas Ulimwengu ambaye ni nchezaji mwenye nguvu kwa kipindi hiki hata robo kwangu hatii ndani,wachezaji wa kipindi chetu  walikuwa na vitu vingi sana ni mchezaji gani? Wa sasa ivi ana uwezo wa kumwamisha beki kwenye Reli na kupasia wavu,hakuna.
“wachezaji  wenye vipaji vya kweli tunawacha na badala yake tunawakumbatia wachezaji wasio na akiri ya uwanjani,Tff wanakijua cha kufanya.
Baada ya kustaafu.
“Kwa sasa nina miaka 47 hadi 2013,nina mke na watoto wawili ,najisughulisha na ufugaji wa ng’ombe wa Maziwa pamoja udalali wa kutafuta Bidhaa Mbali mbali Zinazopatikana hapa Mwanza kwenda Dar  na mke wangu ajishughulisha na ufugaji wa Kuku wa kisasa maisha yetu Sio mabaya.
“kwa kweli sikunufaika na mpira kiuchumi ila kuwa maarufu na kufahamiana na watu imenisaidia sana kufanya shughuli zangu kwa uraisi,Anahitimisha Yondani ambaye ametokea katika ukoo wa wachezaji wa ukweli wa soka na watoto wake muda wote anawahamasisha kuhusu mpira,na wanacheza vizuri.


Chapisha Maoni