Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Alex Mapunda,mwandishi. 








Ali  yusuph Suleiman ‘Tigana’
kwa wadau na mashabiki wa soka hapa nchini hasa kwa wale wenye miaka kuanzia 25 na kuendelea ukipita katika kijiwe chochote na gafla ukasikia jina la ALI Yusuph Suleiman maarufu kama ‘Tigana’ likitajwa na usimkumbuke! wakati ni shabiki wa ukweli  wa soka,hakika itabidi ufanyiwe uchunguzi wa akili kwa kuwa tutakuwa na wasi wasi juu ya uwezo wako wa kufikiri,kutokana na uwezo mkubwa ambao Tigana alikuwa nao pindi alipokuwa akisakata gozi la ng’ombe hapa nchini.
Tigana mzaliwa wa Ilala mpakani mwa mtaa wa Sadani na Newala, jijini Dar es salam alianza kusakata kandanda mwaka 1880 mwaka ambao Tanzania ilipata nafsi ya kushiriki kwa mara ya kwanza na mwisho michuano ya mataifa ya afrika nchini Nigeria katika shule ya msingi uhuru changaiko na nyota yake ikang’aa Zaidi katika timu ya vijana ya shauri moyo kids pamoja na Nambanga Fc, katika mzungumzo na gazeti hili anafafanua mengi kuhusu maisha yake ya soka:-
“Nilianza kucheza soka la ushindani katika timu ya Manyema Fc mwaka 1990 timu ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja la Tatu katika nafasi ya kiungo mshambuliaji ambapo baada ya kuonyesha uwezo mkubwa nyota nyekundu na Pan Afrika waliingia kwenye kinyang’anyiro cha kunisajili ambapo mwaka 1992 nikatua Pan Afrika timu ambayo nilichezea  kwa misimu miwili na hatimaye mwaka 1994 nikajiunga na Yanga Africans, kwa kipindi hicho nilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kucheza mpira.
“Umahili wangu na umakini hasa wakati wa kufunga pindi nikutanapo na timu pinzani uliwafanya simba wanitafute kama chakula pindi mtu awapo na njaa toka nilipokuwa Pan na walifanikiwa kuinasa saini yangu mwaka 1996 baada ya kuniwinda kwa kitambo kirefu na nilifanikiwa kuwatumikia wekundu wa msimbazi hadi mwaka 1998 hapo nilipata nafsi ya kwenda nchini Malaysia.
“Dili la kucheza mpira katika timu ya Malaysia  mimi pamoja na mwanamtwa  Kiwelo tulifanyiwa na moja ya viongozi ndani ya simba  na tulicheza kule hadi mwaka 2001 hapo nikarudi tena Simba,wakati narudi simba maelewano kati yangu na viongozi yalikuwa yameyumba kwa kuwa kipindi tupo Malaysia tulizurumiwa sana na baadhi ya viongizi ambao walitupeleka kule,na dili la kwenda kule pesa zote walichukua huku tukilipwa mishaara ambayo haikufanana na uwezo wetu wa kusakata kandanda,kuna kipindi tuligoma kucheza adi walikuja viongozi wa simba kusuluhisha mgogoro ambapo mimi sikutaka kubaki kule lakini ilitulazimu kubaki kwa vile hati za kusafiria walikuwa nazo wao ikatulazimu kuendelea kucheza kinyonge.
“kiukweli Malaysia sisi tulitoa msaada mkubwa sana kwa timu yao ambapo kabla ya kutusajili sisi timu hiyo ilikaa bila kombe kwa takribani miaka 20 lakini baada ya kutua sisi tukachukua ubingwa wa nchi hiyo,baada ya kurudi simba uhusiano wangu na viongozi uliyumba kutakana na matatizo ya fedha ya dili la Malaysia hivyo nikacheza kwa msimu mmoja na baadae nikatimukia yanga na nikaitumikia timu hiyo toka 2002 adi 2003 apo nikarudi katika timu ya mtaani kwangu Ilala Fc kipindi hicho ilikuwa imepanda ligi kuu nayo nikaitumikia kwa msimu mmoja na 2004 nikaenda kucheza soka la kulipwa uarabuni katika nchi ya Omani.
“Omani sikukaa sana kwa kuwa nilipewa mkataba wa mwaka mmoja ambapo ulipoisha mkataba nikarudi Bongo na mwaka 2005 nilijiunga na Timu ya Moro United maarufu kama chelsea ya bongo kipindi hicho moro walifanikiwa kushika nafsi ya pili katika ligi kuu ya Tanzania na kuwakirisha Tanzania katika michuano ya kimataifa.
“nikiwa na moro United tulifanikiwa kucheza vizuri katika mechi za hawali katika kombe la shirikisho lakini kutokana na kuwepo kwa wachezaji wachache wazoefu katika kikosi chetu tulitolewa na timu ngumu ya Etoile du Sahel ya Tunisia kwa Jumla ya bao 6-1 ambapo kwao walituchabanga bao 4-1 huku nyumbani wakitushindilia bao 2 mtungi na tukaaga mashindano.
                                                   
“mwaka 2008 niliamua kutimkia nchini Afrika kusini mara baada ya timu hiyo kukumbwa na ukata mkubwa ambapo Tajiri aliyekuwa akishikiria timu hiyo alijitoa kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi na wachezaji wengi nyota tuliamua kuondoka, nikiwa Nchini Afrika ya kusini nilisota sana kutafuta timu ya kuchezea kwa kuwa mfumo wa kujiunga na timu za nchini humo ni sawa na Barani Ulaya ambapo ili timu ikuchukue lazima uende na meneja.
“Mimi nilijaribu bahati yangu katika timu ya Mamelodi sundowns pamoja na Santos lakini niligonga mwamba kwa kuwa sikuenda na Meneja,katika Timu ya Santos wakati nilipoenda kufanya maojiano na viongozi wa timu hiyo nilitanguzana na mdogo wangu wakaniuliza huyu ni Meneja? Nikakataa kwa kweli sikuweza kupata msaada ingawa nilichezea timu hiyo kwa kipindi Fulani.
“Baada ya dili la kucheza mpira Afrika kusini kukwama mnamo 2008 mwishoni nilikwea pipa kuelekea bongo kutokana na kusota nchini Afrika Kusini kwa muda mrefu bila kupata mkataba licha ya kiwango changu kuwa juu, niliamua kuachana kabisa na soka,anasimulia Ali Yusuph Tigana kisha Anaendelea:-
Mvi Bukoba iliambatana na majonzi ndani ya Simba.
“siku ya Tukio la kuzama kwa meli ya Mvi Bukoba kila nikikumbuka napatwa na simazi kubwa sana kwa kuwa tukio lile liliambatana na matukio mengine mawili kwangu,kwanza siku hiyo simba tulitoka kupoteza mchezo wa kimataifa dhidi ya Arab Contractor katika Mjini Alexandria nchini Misri,ambapo mchezo wa kwanza walitufunga nyumbani jijini Dar es salam kwa jumla ya bao 3-1, ambapo misri tulitoka sare ya bao 2-2 tukaaga mashindano.
“baada ya mchezo mishare ya jioni tulipata taarifa kupitia kwa shirika la habari la kimataifa,CNN kwamba Meli ya Mv Bukoba imezama na watanzania wengi wamepoteza maisha kiukweli majonzi yaliongezeka mara dufu kwa kuwa tayari tulikuwa na machungu ya kuaga mashindano hapo tukapeana taarifa huku tukijiandaa kurudi Tanzania.
“hiyo ni 9 kakini 10 wakati tuliposhuka uwanja wa ndege jiji Dar es salam hapo tulinyong’onyea kabisa kwa kuwa tulipokea Taarifa ya kwamba mchezaji wa Mahili wa Soka Ramadhani Lemi alikuwa amefariki dunia’anavuta pumzi kwa majonzi kutokana na kukumbuka jinsi ilivyokuwa’kisha anaendelea kusimulia; kiukweli majonzi ambayo tulikuwa nayo ni makubwa sana basi moja kwa moja tukaenda kwenye mazishi ya mchezaji mwenzetu,mungu awaweke mahali pema peponi na wale wote ambao walipoteza maisha.
Nilikimbia na laki moja ya Dewji.
“wakati nipo Pan Afrika kuna kipindi tulicheza mechi ya kirafiki na wekundu wa msimbazi Simba,mchezo ambao nilicheza kwa kiwango cha hali ya juu sana hali ambayo ilipelekea viongozi wengi wa simba kunimezea mate ambapo baada ya mchezo ule, aliekuwa mdhanini wa simba Azim Dewji aliwatuma watu wake kunitafuta ambapo walikuja hadi nyumbani na wakanichukua na kunipeka ofisini kwake.
“siku ya kwanza kuingia ofisini kwa Dewji niliogopa sana kwa kuwa sikuwai fikilia kama kuna siku nitafanikiwa kuingia ofisini kwake kwa kuwa Dewji alikuwa Tajiri mkubwa,baada ya kuingia ofisini kwake alinipokea vinzuri na akaniambia kuwa ameridhika na uwezo wangu wa uwanjani na alinitaka kusaini Simba,nilijifikiria sana kabla ya kumjibu kwa kuwa Pan Afrika walikuwa wamenifadhili mambo mengi sana hivyo nilifikiria juu ya kusaini simba bila kuwalipa fadhira zao,kwa woga nilimkubalia dili la kusaini Simba.
“basi Dewji akanipa kitita cha shiringi laki moja pia akiniambia kuwa anasafari ya kwenda uingereza  hivyo akirudi tutakamilisha kila kitu,kiukweli moyoni nilikuwa njia panda na uamzi ambao nilipanga kuuchukua baada ya kufikiria kwa kina ni kuchezea Pan Africa kwa kuwa tayari nilikuwa na mkataba nao.
“Dewji baada ya kutoka Uingereza alinitafuta sana ili kusaini mkataba Simba kwa kipindi hicho aliwatuma watu wake lakini nilikuwa nikiwapiga chenga kwa kuwa kipindi kile mawasiliano yalikuwa magumu nilifanikiwa adi msimu uliponza nikavaa uzi wa Pan Afrika.
Ushirikina.
“ulikuwepo,upo na utaendelea kuwepo kama timu zetu hazitaamua kuchana na Imani hizo hasa hapa nchini,baadhi ya timu zetu suala la kutumia madawa siku za mechi ni ishu ya kawaida sana,Mimi binafsi siamini Imani hizo kwa kuwa mpira ni Mazoezi nchi zote ambazo nimeinda kusakata kandanda la kuripwa Imani hizo hakuna wao ni mazoezi pamoja na mbinu za kocha.
Mechi kali.
“moja ya mechi ambayo naikumbuka katika michezo yote ambayo nimewai cheza katika maisha yangu ya soka ni mchezo kati ya Yanga na Timu ya Bulawayo Ilenders ya nchini Zimbabwe katika klabu bingwa Afrika,mechi ya kwanza ilifanyika Jijini Dar esalam ambapo mchezo ulimalizika kwa sare ya bao 2-2 matokeo ambayo yaliwakatisha tamaa viongozi wengi wa Yanga kwa kuwa ilitakiwa kwenda nyumbani kwao.
“safari ya kwenda katika mchezo wa Marudiano viongozi wengi wa yanga waligoma kwenda meneja pekee alikubari kusafiri na timu hadi Bulawayo,ambapo siku ya mechi mashabiki wa Ilenders walitupa presha sana  ambapo kila mmoja wao alikuwa ameshika bango ambalo lilisomeka 5-0 na uwanja wa Bulawyo ni mkubwa sana na siku hiyo ulitapika,basi mimi sikuwakawiza kipindi cha kwanza nikawapiga bao,uwanja wote ulikuwa kimya hapo ndipo tukapata nafasi ya kucheza kwa Amani.
“kipindi cha pili Said maurid SMG aliwakimbiza na akawatundika bao la pili bao ambalo liliwachanganya sana mashabiki wao na ikaperekea wachezaji wao wacheze kwa presha kubwa,dakika za mwisho tulipata penalty ambayo ilizua vurugu kwa mashabiki adi ilipelekea mpira kumalizika bila sisi kupiga penalty ile,mashabiki walikuwa wakirusha chupa ngumu uwanjani kiasi kwamba ilikuwa kila tukisogea kupiga penalty walizidi kurusha chupa nyingi Zaidi ambapo mwamzi bada ya kuona hali tete Zaidi akamua kumaliza mpira.
“kingine ambacho kilitokea baada ya kumalizika ule mchezo mashabiki walituzuia kutoka dimbani ilikuwa kila tukitoka wanarusha chupa na kitu ambacho tulikifanya tulichukua makoti yetu na kuweka kichwani huku tukitimua mbio kuelekea katika chumba cha kubadilishia nguo,nakumbuka siku ile tulipigwa sana chupa za mgongoni na mashabiki.
“baada ya mchezo huo nakumbuka tulipangiwa na Mamelodi sundowns toka nchini Afrika ya kusini ambapo katika mchezo huo mimi na Said mwamba tulifungiwa kwa madai ya utomvu wa nidhamu basi yanga ikapoteza mbele ya waafrika kusini na ikaaga mashingano.
Kituko
“ilikuwa kali ya mwaka wakati wa mchezo wetu na timu toka Bulawayo kipindi cha pili kipa wetu Doe mokey  kuna kitu alikisema adi leo bao sijaelewa kama alikuwa akitutania au kweli,Mokey alituita na kutuambia kuwa mimi naacha kusimama langoni kwa kuwa goli naliona kubwa sana kuliko la kule wachezaji wote tuliduwaa kwa kuwa aliongea huku akitukazia macho,wezangu wakamjibu wewe usitutanie mbona mwenzako amesimama hapo hapo hakulalamika?akaendelea kusisitinza kuwa hawezi kusismama langoni,baada ya kumsii kwa muda allikubari kuendelea na mchezo,lakini kusema kweli siku ile alisurubiwa sana langoni kwa kuwa aliokoa michomo ya hatari sana adi kuna kipindi alilalamika vidole vilikuwa vikimuuma.
Daraja la tatu la zamani sawa na ligi kuu ya sasa.
“kwa wachezaji ambao wamecheza mpira miaka ya 1980 adi 1990  watakubaliana na mimi kuwa ligi kuu ya sasa ni sawa na ligi daraja la tatu  kipindi kile kwa kuwa kipindi kile mpira ulikuwa na ushindani wa hali ya juu sana,timu ya ligi daraja la tatu kipindi kile ikikutana na timu ya ligi kuu kwa sasa hakuna utofauti, vijana wasasa wanashiriki mambo mengi yasiyokuwa ya lazima badala ya ucheza mpira.
Yanga walipotezea dili langu la Ulaya.
“wakati wa nchezo wetu kule Bulawayo kuna waarabu walikuja pale kwa ajili ya kusaka wachezaji,na baada ya kutuona sisi walilidhika na kiwango chetu na waliwaita vingozi wa yanga na wakafikiana juu ya sisi kwenda Ulaya katika kisiwa cha Spuras ili kufanya majalibio,baadae  nilitofautiana kidogo na uongozi wa timu hiyo hadi wakanifungia wakidai kuwa nilikuwa na utomvu wa nidhamu wakapotezea dili langu la kwenda Ulaya mimi hata sikuuliza.
“Mimi nadhani kucheza kwangu simba ilikuwa tatizo kwa Yanga kwa kuwa kipindi hicho pambano kati yetu na simba lilikuwa limekaribia,  mimi na mwenzangu walitutuhumu kuwa tumepokea pesa Simba ili kufungisha Timu kitu ambacho mimi nilikishangaa sasa na wala sikuwai fanya ,na kwa bahati mbaya Simba walitufunga Bao 1-0.
Kutokea kwa ‘Tigana’
“wakati nilipokuwa Mdogo watu walikuwa wakiniita Ali Kanada kwa kuwa nilikuwa nikivaa Tsherti ambayo iliandikwa ‘Kanada’  mara kwa mara hasa pindi nilipokuwa nikicheza mpira katika timu yangu ya Utotoni ya Shauri Moja Kids,lakini baada yakiwango changu kukua na kufanya vizuri watu wengi wakaanza kuniita jina la Tigana jina ambalo nililichukia sana kwa kuwa sikuelewa maana yake.
“na kadili nilivyokuwa nikilichukia na watu walizidi kuniita baada ya kuona kero nilimfuata mwalimu wetu wa timu na kumwambia kuhusu jina lile yeye alicheka sana alafu akaniambia kuwa jina la Tigana lina maana na akaniahidi kuwa tutaangalia mkanda ili kujua kuhusu jina hilo.
“Basi mwalimu aliniita pamoja na wezake akatuwashia mkanda kati ya Blazil na Ufaransa ilikuwa ni mechi ambayo ilichezwa miaka ya 70,ilikuwa ni mechi zuli sana na kocha akanionyesha kiungo wa ufaransa  ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Jean Tigana kiukweli alikuwa mchezaji mzuri sana mimi awali sikuwai sikia kuhusu mchezaji huyo ambaye alikuwa mwembamba na sifa kama za mimi.
“Basi kuanzia siku ile nikawa nafanya mazoezi mara kwa mara na kusikiliza mafunzo ya kocha huku nikifuata nyayo zake na nilikuwa nikisikia jina hilo nilikuwa nafurahi sana kwa kuwa walikuwa wakinifananisha na yeye.
Red Stars walinizuia kucheza msimu mzima.
“mwaka 1992 nyota nyekundu pamoja na Pan Africa wote waliniwinda ili kunisajili,nyota nyekundu pamoja na Pan wote walituma watu wao kunitafuka, lakini mimi mwenyewe nilikuwa na mapenzi na pan na nilikuwa siipendi nyota nyekundu.
“kuna jamaa mmoja wa nyota nyekundu alikuwa akikaa mtaani kwetu alikuwa akinifuatilia sana akanichukua mimi na kaka yangu adi ofisini kwa timu yao, mimi nikamwambia kaka yangu kuwa tuwadanganye mimi nimesaini Timu nyingine hivyo nitashindwa kusaini kwao,kweli nikawaambi kuwa tayari nilikuwa na mkataba sehemu nyingine hivyo itaniwia vigumu kusaini kwao.
“uongozi wa Nyota nyekundu walinipa mkataba na wakaniambia kuwa wapo tayari kurudisha fedha za timu ambayo mimi nilikuwa nimechukua,kaka yangu baada ya kuona Nyota nyekundu wanatoa pesa alilainika akanishawishi kusaini mimi sikuwa na mtetezi nikasaini Mkataba.
“Baada ya kufanya mazoezi siku nne nikakutana na kiongozi wa Pan nikamweleza kuwa nimesaini Nyota akanichukua adi ofisini kwao na wakanipa mkataba na wao wakahaidi kurudisha fedha ambazo nilichukua toka Red Stars,kwa kuwa nilikuwa na mapenzi na Pan afrika nikasaini mkataba pia nikahama mtaa ambao nilikuwa na nikaa mara ya kwanza niaamia mtaa wa Namanga msasani kwa mama mkubwa ili viongozi wa Nyota Nyekungu wasinione.
“kitu ambacho kilinifanya nisicheze kwa msimu mzima ni kwamba viongozi wa Pan waliwafuata Nyota na kuwatukana huku wakiwakebei kuwa hawana pesa hivyo nyota nyekundu wakagoma kupokea pesa toka Pan na wakasema kuwa wanamtaka mchezaji wao,kwa hali hiyo ilinilazimu kusugua bechi adi timu ilipopanda ligi kuu hapo nikapata nafsi ya kuanza kuchezea Pan Afrika katika mechi za mashindano,pia kwa kipindi hicho pia nilikuwa nikichezea timu ya mtaani hapo ya Namanga Fc.
Timu ya taifa.
“sijisifii ila kutokana na uwezo wangu mkubwa wa kusakata kandanda nimefanikiwa kutumukia kikosi cha timu ya taifa kwa misimu mingi sana,ambapo ifuatayo ni baadhi ya miaka ambayo naikumbuka nimechezea timu ya Taifa,mwaka,1993,1994,1996,1998,2001 pamoja na mwaka 2005 ambao ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kuitwa timu ta Taifa.
Tukio kali
Anacheka kisha anaendelea; ”katika mchezo wa soka kama timu yenu ikipata ushindi wachezaji ufarijika sana,sasa kilicochotokea  baada ya kumalizika kwa mchezo wetu mjini Bulawayo kati ya yanga na wapinzani wetu Said Maurid alinitonya kuwa kuna zawadi  ya mchezaji bora  twende tukachukue ambapo yeye alikuwa nyota wa mchezo ule na aliniambia kuwa zawadi hiyo ni boksi moja la castle leager.
“mimi nilifurahi sana na nikamwambia SMG asitoe taarifa kwa mtu mwingine adi baada ta kuchukua kile kinywaji,kweli tukaenda kwa uongozi wa siku ile na tukakabidhiwa mzigo wetu tukaondoka nao baada ya kuondoka Said Maurid yeye alikuwa hatumii pombe mimi nikachukua lile furushi nikaenda nalo chooni nikafungua haraka na kuitoa castle nne na nikafungua moja nikaaza kubugia huku nikipita kuimba huku nikiwatonya wenzangu kwa ishara kuwa waende chooni kuna mzigo.
“wachezaji wezangu wakaenda chooni kuvamia ule mzigo ambapo kuna wengine walichua mbili mbili wengine moja pi wapo ambao walikosaka, sherehe ikaendelea  mpaka tulipokwea pipa kuelejea nyumbani Tanzania.
Tulisafiri kwa basi na timu ya Taifa adi Zambia.
“mwaka 2003 timu yetu ya Taifa la Tanzania sisi tukiwa wachezaji tulienda kwa usafiri wa Basi toka Dar es Salam adi Zambia isipokuwa wachezaji watatu ndio walienda kwa usafiri wa ndege akiwemo Juma Kaseja pamoja na Pawasa kiukweli tulichoka sana kwa kuwa tulikaa kwenye basi kwa muda mrefu Sana.
“siku ya mechi wachezaji wa timu ya taifa ya Zambia walicheza mpira mzuri sana kushinda sisi kwa kuwa tulikuwa bado na uchovu wa safari ingawa juma kaseja alicheza vizuri sana siku ile hata hivyo zambi walitutungua bao 2-0 na wao wakasonga mbele sisi Tukarudi nyumbi mikono kichwani.
Wachezaji  nyota.
“Tegete wa yanga alikuja vizuri sana lakini kwa sasa amejilemaza kiwango kimepungua pia mchezaji wa kimataifa wa Rwanga beki mbuyu Twete anafanya vizuri.
Ushauri.
“rais Malinzi ajitaidi kutekeleza majukumu yake kama inavyotakiwa kwanza nampongeza kwa mpango wake wa kuzunguka nchi zima kusaka vipaji kwa ajili ya timu imara ya Taifa,pia  wasimamie uwepo wa shule za michezo za ukweli ili kuhakikisha soka letu linafika mbali kimataifa.
Maisha baada ya soka.
“Umri wangu ni miaka 43hadi 2013, nina cheti cha ukocha nafundisha timu ya Daraja la kwanza ya Frend Rangers ,pia nafanya biashara ndogo ndogo,na nina watoto watatu”,Anaitimisha Ali Yusuph Maarufu kwa jina la Tigana ambaye alifanikiwa kutikisa soka la hapa nchini kwa kucheza simba na Yanga pia timu ya Taifa ya Tanzania.
mwisho


Chapisha Maoni