Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Na Alex Mapunda.
 KELVIN Haule ni miongoni viungo washambuliaji wachache ambao walikuwa na uwezo mkubwa wa kufunga ambapo jina lake lilikuwa kubwa alipochezea Maji Maji Pamoja na Timu ya Taifa “Taifa Stars”.
Kelvin Haule
   Katika mazungumzo maalum na Gazeti hili ameeleza mengi kuhusu maisha yake ya soka wakati akicheza:
  “nilianza kucheza soka Tangu nilipokuwa mdogo kwa kuwa niliupenda mchezo huo,lakini nilianza kucheza soka la ushindani katika kiwanda cha nyuzi Iringa mwaka 1983,hapo nilicheza kwa kipindi cha mwaka 1 na mwaka 1984 nilijiunga na timu ya Reli ya Iringa hapo nilicheza kwa mafanikio makubwa baadae nikasajiliwa na timu ya Tukuyu stars [Mbeya]ambayo ilikuwa ikishiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara, kwa sasa Ligi kuu ya vodacom.
  “nilisakata kabumbu kwa kipindi cha miaka mitatu nikiwa na Tukuyu stars,ambapo timu yetu ilifanikiwa kushiriki michuano ya Afrika mashariki, mara baada ya timu yetu kufanya vizuri na katka michuano hiyo  tulifanikiwa kufika hatua ya robo fainali na bahati mbaya tulitolewa na Sports Club Villa toka Uganda katika mechi hiyo tulifungwa goli 4-1 na tukaaga mashindano.
  “kwa kipindi chote ambapo nilikuwa na Tukuyu Stars nyota yangu ili ng’ara sana ambapo timu mbali mbali zilikuwa zikinigombania lakini mwaka 1987 nikaamu kujiunga na Maji Maji ya  songea maarufu kama wanalizombe na hapo nikacheza kwa mafanikio makubwa zaidi na nikaiwezesha maji maji kuwa mabingwa wa ligi ya muungano mara moja mwaka  98 na kupata nafasi ya kushiriki clabu bingwa afrika chini ya Meneja wa mahili wa maji maji wa kipindi hicho Shaffy Bora.
  “ Maji maji nilicheza kwa kipindi kirefu kutokana na uongozi mzuri na mshikamano ambao ulikuwepo ndani ya timu hiyo na kufikia mwaka 2000 nikaondoka,na kwa kipindi chote hicho kuanzia mwaka 1987 – 2000 nilipata nafasi ya kucheza timu ya taifa ambapo wakati huo kiwango changu kilikua zaidi na nikafahamika nje ya mipaka ya Tanzania na umaarufu wangu ukaongezeka mara dufu.
   “Niliamua kutundika daruga rasmi mwaka 2002 nikiwa na miaka 39 nikiwa na Twiga Stars ya kinondoni timu ambayo sikuchoeza kwa mafaniko makubwa kutokana na kwenda kwa umri na kutofurahishwa na maslahi ya kipindi hicho hapo nikatundika daruga na kubakia katika timu za veterans.
Sababu za kuto kucheza Timu kubwa
  “Sikucheza timu kubwa kwa sasabu timu hizo toka kipindi hicho hazikuwa na malengo endelevu kwa wachezaji kikubwa walikuwa wanaitaji uduma ya mchezaji na sio kumjengea mchezaji maisha ya baadae,lakini nikacheza kwa mafanikio makubwa ingwa sikujiunga na timu hizo ambazo zina mizengwe na zinawajali wachezaji wa upande.
  “Kuna kipindi nitekekezwa na Yanga hotelini mwaka 1987 wakati nipo na Tukuyu Stars kwa kipindi cha mwenzi mmoja bila kujua hatima yangu ni ipi huku wakinipa matumaini ya kunipa mkataba lakini tulishinda baadae kwa kuwa Yanga waligoma kuniamishia kikazi jijini Dar es salam na wakanitaka nicheze bila kazi kwa kuwa kipindi kile kila Timu ililazimika kumtafutia mchezaji kazi nje ya soka, nikaamu kuachana nao na na kujiunga na Wanalizombe mjini Sopngea.
Anachokumbuka
  “Stasahau wakati nipovunjika mguu mwaka mwaka 1987 katika uwanja wa  CCM kirumba mwanza katika michuano ya Shimmuta,wakati ya mechi kati ya NMC-shirika la usagaji pamoja na BIT timu ambayo iliusisha makampuni ya biashara, katika mechi ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa kutokana na wachezaji wengi wa ligi kuu kusajiliwa na timu hizo.
 
“katika mechi hiyo kwa upande wetu NMC tulishinda goli 2-1 magoli ambayo nilifunga mimi mwenyewe,lakini Vegasitus Limbu alinichezea rafu mbaya sana na akanivunja mguu,niliumia sana lakini mungu akajalia nikaudumiwa vizuri na kurejea uwanjani.
Mechi ninayoikumbuka
  “Naikumbuka sana mechi  ya clab Bingwa afrika raundi ya Tatu, kati ya Maji Maji na Fc Leopard ya Kenya ilikuwa ni mechi kali na ngumu sana kwa upande wetu ambapo mchezo wa kwanza ulifanyika jijini Arusha katika uwanja wa Amri Abeid,walituchalaza goli moja mtungi hali nambayo ilikatisha tamaa ya kusonga mbele.
“katika mechi ya marudiano nchini Kenya katika uwanja wa Moi Kasalani mechi ikianza kwa mashambulizi ya kila upande wakati wote wa mchezo na hadi mwamzi anapuliza kipenga cha mwisho FC Leopard 0,Maji Maji mtungi na tukatupwa nje kabasa ya mashindano.
kelvin haule
 Timu za Tanzania kufanya vibaya
  “wachezeji wengi wanaochezea timu zetu za hapa nyumbani hawana uzoefu mkubwa wa kushindana tofauti na wachezaji wa timu za wezetu ambao wanacheza mechi nyingi kushinda hapa nyumbani hilo ni tatizo kubwa Tff lazima walifikile.
  “vile vile hapa Tanzania wachezaji wanaibuka tu kutokana na kucheza mitaani na kucheza timu kubwa ambazo zinatuwakilisha katika mashindano ya kimataifa,kwa wenzetu wanakuzwa katika shule za michezo toka wakiwa wadogo,hali ambayo inapelekea timu zetu kufanya vibaya kimataifa.
Tofauti,FAT-TFF.
kipindi cha Fat wachezaji wa Timu ya taifa Tulikuwa tunacheza katika mazingira magumu sana hasa kwa upande wa vifaa,mara nyingi tulikuwa tunabeba vifaa toka nyumbani ikiwemo viatu na muda mwingine ilitulazimu kufanya mazoezi bila vifaa vyote.
  “lakini saizi ingwa kuna matatizo kipindi kile yalizidi ila tulikuwa tunafanya vizuri kutokana na kwamba wachezaji wa zamani walikuwa wazalendo na walichulia soka kama sehemu ya maisha yao.
Wachezaji anaowakubari
  “nawakubari sana Shomari kapombe,saimon msuva pamoja Salum Habubakari[shua Boy] ambao ni chipukizi na wapo katika viwango vya juu kwa hivi sasa.
  “pia navutiwa na kiwango cha mcheji wa kigeni wa Azam FC toka Ivory Cost kipre Tchetche, ambaye ni moto wa kuotea mbali.
Mafanikio katika Soka
  “kiuchumi mpira haujanisaidia sana kwa kuwa kipindi kile hapakuwa na maslai kwa wachezaji zaidi ya kupata pesa ya kula,ila nimefanikiwa kufahamiana na watu mbali mali na kufahamu maeneo mengi katika nchi nyingi.
Ushauri kwa timu Maji Maji
  “viongozi wa timu ya maji maji wasiongoze timu na kutegemea watapata pesa katika Serikali ya mkoa ilo wafute na wawe wabunifu kwa kutafuta njia mbadala ili kuongoza timu hiyo kwa manufaa ya wanamaji maji.
  “wadau wa soka wapo mbali na timu yao ikilinganisha na zamani,lazima warudishe mawazo yao kwa timu ya Maji maji ili kurudisha maji maji ya ezi zangu ambayo ilitikisa soka la Tanzania.
Maisha baada ya Soka.
  “nafanya biashara ndogo ndogo za ujasiliamali ambazo zinaniingizia kipato pia ni Makamu mwenyekiti wa chama cha soka songea mjini [SUFA] pia ni katibu wa chama cha makocha mkoa wa Ruvuma, ingwa sina mafanikio makubwa naishi vizuri na fanilia yangu.
  “  sasa nimeoa na nina watoto watatu wote wa kiume kwangu mimi ni faraja kubwa sana
na naishi nao kwa amani.


Chapisha Maoni