Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






John Alex Lwena
John Alex Lwena ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa na kipaji cha pekee kuwai kutokea hapa nchini,ambapo kwa umaili mkubwa alikuwa na uwezo wa kucheza namba zote kumi na 11 uwanjani na kucheza juu ya kiwango.
Alex mzaliwa wa Namatui huko Mpitimbi Songea Vijijini alianza kusakata kabumbu katika shule ya msingi Mpitimbi ambapo baada ya kumaliza shule ya msingi akatimukia kwa kaka yake ubaruku mbeya ambako alijiunga na timu ya Rubiga Fc huko Tukuyu.
Katika mazungumzo maalum na gazeti hili nafafanua zaidi kuhusu maisha yake ya soka;
“Nilianza kucheza soka la ushindani  nikiwa na Tukuyu Stars timu ambayo iliundwa kwa mara ya kwanza na wachezaji wengi toka Rubiga Fc wakati huo ilikuwa ikifahamika kwa jina la Limbe Kabla ya Tukuyu Stars timu ambayo tuliipandisha Moja kwa moja Toka madaraja ya chini na kufanikiwa kuchukua ubingwa mwaka 1986.
“Na baada ya uwezo wangu kuwa katika kiwango cha juu Mwaka 1989 yanga wakanichukua kipindi ambacho nilipata nafsi ya kuchezea timu ya taifa kuanzia mwaka 1989-1990 ambapo mwaka 1994 niliondoka yanga na kujiunga na timu ya Maji Maji ya songea kwa  ubadhirifu wa usajili ambao sita kuja kuusahau hadi nitakapoingia kaburini ambao ulifanywa na aliyekuwa kiongizi wa yanga bwana Mpondela.
“kilichotokea Yanga walituacha katika kikosi hicho dakika za mwisho na majina yetu wakawaingiza wachezaji toka nje hali ambayo iliniuma sana kwa kuwa hadi siku ya mwisho ya usajili majina yetu tuliyahakiki na yalikuwepo.
“Na baada ya muda wa usajili kuisha habari zikatoka kwenye magazeti kuhsu usajiri cha kusikitisha majina yetu hayakuwepo hali ambayo ilitufanya tuishiwe nguvu ambapo kwa kipindi kile ilikuwa ukiachwa kwenye usajili ililazimika kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha mwaka mmoja.
“Hayo yote yalitokea  baada ya kubadilika kwa uongozi ndani ya Yanga ambapo viongozi wapya  walikuja na falsafa ya kuwapandisha vijana wengi toka kikosi B na kutuacha wachezaji wengi ambao tulikuwa wakongwe na wazoefu katika timu ile.
“Hali mabayo ilizua mtafaruku mkubwa sana kati ya viongozi na wanachama ambao walioji kwa nini wametufanyia kitendo cha kinyama dakika za mwisho,viongozi wakakosa jibu na wakakili wamekosea baadae suala lile wakalifikisha TFF ili sisi tuingizwe kwenye usajili lakini kwa bahati mbaya Tff walikataa kwa kuwa taarifa tayari zilikuwa zimishatoka kwenye vyombo vya habari.
“Hatukuwa na jinsi lakini kitu ambacho kilitokea baada ya sisi kuachwa katika kikosi kile Yanga walinusurika kushuka daraja kutokana na kwamba walikuwa na kikosi dhaifu sana kikosi ambapo kilipoteza mechi nyingi sana katika ligi.
“Nashukuru Mungu baada ya tukio lile sikukaa sana nje ya uwanja  Maji Maji wakanichukua bila kuchelewa hawali wakaniingiza kwenye kikosi cha timu ya Mkoa wa Ruvuma  na baadae wakinisajili moja kwa moja Timu ambayo niliitumikia hadi mwaka 2002 kwa mafanikio makubwa sana na baadae nikaachana na  soka nikiwa na timu hiyo na kugeukia shughuli zangu za kawaida,anaeleza Alex kasha anaendelea;
Dini ilimzuia kwenda Oman.
“Wakati nipo yanga kuna kipindi nilikosa Nafsi ya kwenda kucheza Oman katika ligi ya Mafuta ligi ambayo matajiri wa oman walikuwa wakikusanya wachezaji wazuri toka Afrika na kwenda kuunda vikosi vyao  na walikuwa wanawalipa pesa ndefu sana.
“Lakini kutokana na kwamba mimi nilikuwa sio Mwislamu Nikakosa Fursa ya kwenda, mara baada ya kubaini jina langu lilikuwa sio la kiisilamu na wezangu walipatanafsi ya kwenda kwa kweli niliumia sana na sikuwa na jinsi kwa kuwa haikuwa bahati yangu.
Hawezi kusahau
“wakati nipo Yanga katika mechi ya pambano la watani wa Jadi Simba na Yanga nakumbuka niliumizwa Goti kwa Makusudi na mchezaji wa Simba Omari Mavisu kwa kuwa nilikuwa nampelekesha sana ali ambayo ilinilazimu kukaa nje ya uwanja kwa kipindi kirefu na katika mechi ile Simba walipata ushindi wa bao 1-0.
“kitu  Ambacho sita kuja kukisahau baada ya kukaa nje kwa kipindi cha miezi miwili kulikuwepo na mechi kali sana kati ya Yanga na Coastal Union ya Tanga wataalamu wa nje ya uwanja wa Yanga wakasema kwenye mechi ile mimi lazima nikacheze na wakasema wachazaji wengine wote nyota zao zilikuwa zimefutika na nyota pekee ambayo ilikuwa inang’aa ni nyota yangu.
“kwa kipindi hicho nilikuwa hata kutembea siwezi lakini mtaalam mmoja akanichanjia dawa kwenye goti kabla ya mechi na wakanitaka kuingia mchezoni dakika 20 kabla ya mchezo kumalizika ili kugusa mpira na kuziweka sawa nyota za wezangu.
“Na mechi ile yanga waliichukulia kwa uzito mkubwa kwa kuwa kama tungefungwa au kutoa sare Tungetolewa kwenye mbio za kuuania ubingwa mwaka 1990 kweli dakika 20 kabla ya mtanange kumalizika wakaninyanyua kwenye benchi na kuingia uwanjani.
“uwezi kuamini kitu ambacho kilitokea kwa mara ya kwanza nilikuwa natembea vizuri na nikawa na uwezo wa kukimbia uwanjani,mara baada ya kuingia uwanjani na mimi kugusa mpira hazikupita dakika tano tukapata bao ambalo lilifungwa na Keneth Mkapa bao ambalo lilidumu hadi dakika ya mwisho ya mchezo.
Ushirikina Michezoni
“unafanywa sana na nchi zote za kaafrika,kila mtu na imani yake lakini kwa viongozi wa timu hadi hivi sasa hayo mambo yapo na bado yanaendelea.
“Nakumbuka wakati nikicheza wakati mwingine ilikuwa inatulazimu kuruka geiti au kuruka ukuta kwa kutumia ngazi kwa imani za ushirikina  mambao ambayo yanafanywa sana hasa na Timu kubwa Simba na Yanga.
Mechi anayokumbuka
“Naikumbuka Sana Mechi yangu ya kwanza  ya kimataifa kati ya Tukuyu Stars na Sports club Villa katika michuano ya afrika mashariki na kati sisi tukiwa wawakirishi wa nchi,
Mechi ambayo ilikuwa ngumu na Villa wakaibuka na ushindi wa bao 4-0.
“siwezi kuisahau mechi ile kwa kuwa wachezaji wengi ambao tulikuwa tukichezea tukuyu stars ilikuwa mechi yetu ya kwanza ya kimataifa licha ya kwamba tulicheza vizuri katika mchezo ule lakini Villa wakatutundika bao nne kutokana na uzoefu wao katika mashindano ya kimataifa.
Mchezaji anayemkubari
.
“Niyozima ananikosha sana ni moja ya viungo bora tulionao katika ligi ya hapa nyumbani ambapo tunaweza kufananisha na viungo wa zamani wa hapa nchini.
Namba zote uwanjani zilikuwa mali yake
“Nlilikuwa na uwezo wa kucheza namba zote nikiwa uwanjani na nilikuwa na nguvu na uwezo nkubwa wa kukimbia na mara nyingi nilikuwa napangwa nafasi ya winga kwa kuwa nilikuwa na uwezo wa kupiga mashuti kwa kutumia miguu yote miwili kama Ronaldo,na nilikuwa jasiri kutokana na mazoezi magumu ambayo nilikuwa nikiyafanya.
“kwa mabeki ambao waliwai kukutana na mimi awawezi kunisahau katika maisha yao kwa kuwa mbinu zote za beki nlikuwa nazifahamu na nilikuwa nakiwaumiza vichwa.
“Kuna kipindi wakati nipo Tukuyu Stars wakati tunapigania kupanda Daraja katika ligi ya kanda mlinda mlango wetu alikuwa ameumia mimi nikachukua jukumu la kusimama golini,kwa kweli nilicheza kwa umahili mkubwa sana na kutokana na uwezo wangu kuwa nzuri sikuruhusu bao lolote siku ile, ambapo tuliibuka na ushindi wa bao 3-0.
Nidhamu
“Nidhamu ndio kila kitu katika mpira mimi nakumbuka pindi nacheza sikuwai gombana na viongozi au wachezaji wezangu kwa kuwa nilikuwa na nidhamu lakini viongozi wa timu mara nyingi wanatumia nidhamu vibaya kwa wachezaji hasa wakati wa usajiri kama kuna pesa ulikuwa unawadai ikifikia wakati wa usajili ukiwadai wanatishia kukutema ambapo mara nyingi wachezaji wengi wanapoteza sana pesa zao wakati wa usajili.
“Lakini kuna baadhi ya wachezaji toka wakati wa enzi zetu hawakuwa na nidhamu lakini walikuwa na uwezo wa hali ya juu sana mfano Saidi mwamba wakati tunacheza nae alikuwa mlevi wa kupindukia, nakumbua alikuwa anatoroka kambini kwenda baa na kuletwa akiwa amebebwa na kuna wakati mwingine alikuwa anawatukana adi viongozi wa club.
“lakini alikuwa na uwezo wa hali ya juu sana kiasi kwamba licha ya nidhamu yake kuwa mbovu lakini akikosekana yeye uwanjani ilikuwa ngumu sana kupata ushindi tofauti na wachezaji wa sasa wengi wao hawana nidhamu lakini kucheza mpira hawajui.
Baada ya kustaafu
Sasa  ninafanya kazi Tanesco kabla ya hapo nilikuwepo Sido nikifanya kazi ya kuchomelea vyuma,nashukuru mungu maisha yangu yanaenda vizuri ingwa soka sikunufaika nalo chochote kiuchumi zaidi ya kunionyesha dira ya maisha kwa kufamaniana na watu wengi.
“kwa sasa nina miaka 43 hadi 2013 naishi Songea,nina mke na watoto wanne.anahitimisha John Alex Lwena.


Chapisha Maoni